Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Philipo Augustino Mulugo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. PHILIPO A. MULUGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa fursa niweze kuchangia Wizara hii ya Elimu lakini before that nitoe kwamba ni mdau wa elimu na ni mwalimu na ninamiliki shule. Kwa hiyo, nitakayoongea hapa nayaishi kwa kila siku. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla ya hapo ni lazima tuelewe kabisa kwamba Awamu hii ya Sita toka tumepata uhuru ukienda huko vijijini, kama Mbunge na-declare kabisa kwamba tumepeleka fedha nyingi sana kwa ajili ya shule zetu za msingi na sekondari. Hata kwenye kata yangu nilikozaliwa Udinde Kata ya Udinde, nimepewa milioni 600 na Serikali na wananchi wamejenga shule na wamenipa heshima inaitwa Mulugo Sali. Sasa hii ni heshima kubwa nitakufa lakini jina litabaki. Kwa hiyo, lazima nimshukuru Mheshimiwa Rais, kwa kazi kubwa anayoifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimshukuru sana Mheshimiwa Waziri, Pfofesa Mkenda na Naibu Wake Kaka Kapinga, wanavyoshirikiana vizuri siku hizi na shule binafsi. Tumekaa baadhi ya vikao mara mbili mara tatu tofauti kabisa na miaka ya nyuma ilikuwa mkiandika barua Wizara ya Elimu mkae na shule binafsi wanaogopa kabisa kukaa. Sijajua walikuwa wanaogopa nini? Nadhani Mheshimiwa Profesa Mkenda, umekuwa na GB kubwa sana na unatusikiliza kwa unyenyekevu mkubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumekaa na wewe na wadau wa nchi nzima wametoka mikoani kuja pale Morena, umetusikiliza matatizo yetu yote na mengine unaendelea kuyatatua. Lakini nikuambie ukweli sio siri wanaokuangusha ni watu wako wa chini. Ulikuja wewe ukaja na Katibu Mkuu baada ya hapo kuanzia Kamishina na ngazi nyingine za huku chini yale tuliyoongea no implementation. Yaani hamyatejkelezi yale sasa sijui wanaokuangusha ni akina nani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ile kauli ya kusema kwamba hao ni wanasiasa tu kwa kweli hii kauli nchini hapa huwa ninakwaza sana. Hata juzi imejitokeza pale Kariakoo, yaani wizarani wanamuona waziri kama ni mwanasiasa, kama vile akisema jambo watu wa chini huku hawawezi kutekeleza. Jamani hili jambo ni baya sana kitaifa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, juzi Mheshimiwa Waziri Mkuu amekemea hata mambo ya TRA pale Kariakoo. Nimeshakuwa Naibu Waziri najua pale wizarani Maafisa wa kawaida wengi wanamwambia tu waziri si mwanasiasa huyo. Jamani hili jmbo tulikomeshe kwa sababu waziri ana mamlaka makubwa kwenye wizara yake. Naomba hili jambo yaani ni jambo baya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lazima tulifanyie utafiti tuone kwamba ni kweli viongozi wengine huku chini wanadharau mamlaka ya waziri. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri, nikupongeze na endelea kuwa na moyo huo huo. Vilevile, lazima nikushauri mambo mawili matatu ili twende vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, nipongeze mfumo huu wa Sera mpya na Mtaala mpya wa elimu, kama mwalimu naona umekaa vizuri. Nimepitia sana nimesoma, vipo vitu vidogo vidogo ambavyo tutaendelea kushauri na uzuri mimi na wewe ni rafiki yangu siku hizi tunaongea. Zamani ulikuwa hupokei simu zangu lakini siku hizi unapokea simu zangu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninafurahi Profesa Mkenda hata ukimuita hivi njoo mnaongea nae, canteen unaongea nae ni mtu mzuri sana. Sasa lazima tukushauri ili wizara yako ikae vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, cha kwanza, katika mtaala huu mpya wa elimu na sera msisahau mambo ya kiutawala. Mmekwenda kwenye practical, kwenye madarasa, sekondari, elimu ya awali na msingi lakini mmesahau kwenye utawala huku ambako ndiko mnakosimamia elimu. Huku na kwenyewe kumeoza kabisa. Mwingiliano wa TAMISEMI na Wizara ya Elimu yaani huku ndiko kumeoza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Profesa jitahidi una shule za msingi karibu 16000 nchini. Tungekuona unafanya ziara unatembelea shule za msingi uone maisha ya kule chini wanavyokuwa wamekaa wale watoto lakini uone majukumu yanavyoingiliwa na TAMISEMI. Yaani Wizara ya Elimu wewe huonekani kabisa, kule wanaonekana Maafisa wa TAMISEMI tu yaani Wizara ya Elimu imepokonywa kabisa mamlaka yake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naona kuna utofauti mkubwa sana. Sheria Namba 25 ya Mwaka 1978 inasema “Mtaaluma Mkuu katika nchii hii ni Kamishina wa Elimu” ambae unae wewe pale ofisini kwako na una maafisa wako pale. Sasa wachukueni Maafisa wa TAMISEMI basi muwarudishe Wizara ya Elimu. Kwa sababu huu ugatuaji umetuletea shida mno na hasa kwenye utitiri wa mitihani. Yaani kule chini Mheshimiwa Waziri, kuna mitihani ya kata mara mbili kwa wiki, mitihani ya wilaya mara moja kwa mwezi, mitihani ya mkoa mara tatu kwa miezi minne. Sasa kwa mfano sisi shule binafsi kwa nini mnatuingilia? Tuacheni na mitihani yetu. Sisi mitihani yetu inaweza kuwa bora kuliko mitihani yenu mnayoifanya pale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, TAMISEMI wasimamie shule zao kwa sababu TAMISEMI ina shule zao na sisi shule za private mnatupotezea muda kutuletea mitihani ambayo tunakuja kufanya kwenye Mock. Mbona kwenye Mock tunatii na tunachangia na kwenye NECTA wanatuletea mitihani lakini jamani mpaka mitihani ya kata kweli? Yaani Afisa Mtendaji wa kata anawaambia shule za private siku fulani kuna mtihani halafu tunabaki kutoa hela tu na hizo hela wazazi hawaoni kwa sababu tunatoa shule. Mngekuwa mnatuambia mapema tuweke kwenye joining instruction.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tunachangia shule za kata shilingi 100,000 kila wiki. Jamani maisha gani haya? Mitihani ya wilaya kila mwezi yaani wanabaki tu wanafaidi kwenye computer, photocopy kuna posho wanapata ndio maana wanang’ang’ania ile mitihani. Fanyeni mitihani yenu kule chini kama shule za TAMISEMI. Ndio maana nakwambia Mheshimiwa Waziri kwenye utawala hapa msiache. Tunapokwenda kufanya mabadiliko kwenye elimu naomba twendeni na jambo la kupata chombo huru cha kusimamia elimu kwenye nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, huku kwingine kote Mheshimiwa Waziri utaweza lakini usipofanya jambo hilo mkachukue basi hawa wadhibiti ubora wa elimu Tanzania hawa basi wabadilisheni hao kiwe ni chombo huru kiwe na mamlaka kama ilivyo TCU kwenye vyuo vikuu, kama ilivyo NACTE kwenye vyuo vya kati. Sasa shule ya awali, shule ya msingi na sekondari hawana msimamizi yaani hawana Baba na Mama kabisa. Tena sisi private ndo tumbaki kama yatima hivi. Yaani unafikiri jambo sijui niende Wizara ya TAMISEMI, sijui niende kwa Mheshimiwa Profesa Mkenda lakini husikilizwi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunalia mambo ya tozo hapa nani wa kutusikiliza? Hamna. Waziri wa Elimu, huwezi kuzitoa tozo, najua Sheria huwezi kuzitoa tozo. Waziri wa TAMISEMI, ndiye anayetoza tozo kule chini kwa sababu mlilazimishwa mkatupa leseni za biashara. Kwa hiyo, nyie mmezi-term hizi shule kama biashara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii na-quote kwa sababu Afisa wako wa Baraza la Mitihani siku ametoa ranking anasema “hapa tunafanyia watu biashara” Mungu wangu. Watoto wetu ni watanzania hawa hawa wanapokuwa wamefanya vizuri kwenye private ni watoto wa ndani hawa hawa, wanakwenda kuajiriwa Serikalini huko huko watapata uelewa mkubwa na GB kubwa kwa kufanya kazi za Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nilikuwa naomba Waheshimiwa Wabunge, tumsaidie Mheshimiwa Waziri afanye mabadiliko haya lakini baadhi ya mabadiliko Mheshimiwa Waziri hawezi. Sheria Namba 25 ya Mwaka 1978 inaniambia kama private nakwenda kusajili shule yangu kwa kamishina ananipa kibali, ananipa cheti lakini sikuambiwa kama ni biashara. Bila hivyo, shule hizi zisingeanzishwa ndio maana unaoana siku hzi hata uwekezaji wa shule umedolola kabisa. Nani anatamani kujenga shule saa hizi? Tuliojenga tumejenga kama ni kula hasara tumekula hasara. Mheshimiwa Waziri, tuwe creative, jambo ni kubwa mno nendeni huku chini mkaone mambo yanavyokuwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, bado niendelee kuisisitiza jambo lingine kuhusu ranking, Mheshimiwa Waziri, ranking duniani kote, uliongea vizuri sana lakini kwa sababu Mheshimiwa Waziri anapoongea huwezi kumpinga wala huwezi kusema mwongozo kwa sababu tu unatoa taarifa. Jamani Profesa ulitusomesha vizuri pale lakini uliongelea upande wako mmoja. ungetukaribisha na sisi wadau wa elimu kama zinavyofanya wizara nyingine, kwamba kabla hamjaamua mambo mnakaa na wadau wanaokuwa kwenye sekta hiyo mnakaa pamoja mnasema jamani tuondoe ranking au msiondoe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo shuleni watoto hawasomi kabisa wanacheza madarasani. Hakuna ushindani kwenye taaluma. Tunakwenda kuleta watoto mbumbumbu baada ya miaka 10 mtakuja kuniambia. Mimi nadhani sasa shule za private ndio zinakuwa maabara za kuangalia mfano kwamba hawa kumbe ndio wanakwenda hivi. Kwa sababu kama alivyosema Mheshimiwa Waitara, kwenye private kuna kila kitu, Tunagharamia kila kitu kiwepo ili nyie watu wa Wizara za Serikali muige kule tupate Watoto ambao ni wazuri lakini sasa hivi ninyi mnashindana na sisi. Ngoja tutoe hiki ili hawa wa–suffocate, ngoja tutoe hiki ili hizi shule zife. Tutakufa sawa hakuna shida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu Serikali ikiamua tutakufa lakini baada ya hapo tutapata vijana ambao ni mbumbumbu kwa miaka ijayo. Mheshimiwa Waziri na wote humu mnajua ndio maana nilishasema siku moja, asimame mtu hapa aseme mimi mtoto wangu anasoma shule za Serikali. Sio kwamba na-challenge shule za Serikali lakini nataka nikupe changamoto ili uweze kuboresha shule zako. Ndio maana hata Serikali mmeweka baadhi ya shule kuwa ndio shule za mfano zipo, twendeni huko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikuombe sana lakini lingine ni kuhusu nyaraka za Serikali, ni utitiri, mwenzangu jana Mheshimiwa Rweikiza ameongea hapa. Nimesoma hapa yaraka 110 za Serikali yaani kama vile Sheria haifanyi kazi. Yaani kila bada ya miezi sita mpaka ukute waraka shuleni. Siku moja nilikwambia pale Mheshimiwa Waziri, mbona Wizara yako haitulii? Angalia wizara nyingine zilivyotulia hatuna malalamiko ni machache machache lakini Wizara ya Elimu kila siku mnataka kukwaza watu. Yaani hauwezi kutulia, huwezi kumfundisha mtoto kuanzia darasa la kwanza mpka form four angalau anakwenda katika mwelekeo wa elimu hii. Katikati pale anavurugwa, mara ondokeni boarding kuna wakati nashangaa sana siijui nani aliyewashauri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa leo ni darasa, kuna waraka unaosema kwamba daradsa la nne ni lazima wamalizie pale plae na mmetoa na namba ya kumalizia shule pale pale halafu mmetoa nan amba ya kumalizia shule shule palepale halafu mwezi wa saba mnasema waondoke, itakuwaje sasa? Nina shule Mbeya mtu anakuja kutoka Tunduma amekuja pale St. Marcus shuleni kwangu halafu sasa mwezi wa saba arudi Tunduma. Kule Tunduma aliko kule Chapwa hakuna English medium atakwenda wapi? Atahamia wapi? Lakini ulishampa namba ya NECTA afanyie mtihani pale pale kwenye kile kituo. Sometimes mnafanya vitu ambavyo hamshirikishi Mheshimiwa Waziri. (Makofi)

MWENYEKITI: Ahsante sana.