Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Ng'wasi Damas Kamani

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. NG’WASI D. KAMANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kupata nafasi ya kuchangia kwenye wizara hii Muhimu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kwa kutoa shukrani za dhati kwa Serikali ya Awamu ya Sita. Rais wetu Dkt. Samia suluhu Hassan, tangu alipoingia madarakani kati ya sekta ambazo aliziangalia kwa jicho la tatu ni sekta hii ya elimu. Mapema Kabisa alitoa msimamo wake na maelekezo kwamba anataka maboresho yafanyike lakini hakuzungumza tu alienda kwa vitendo. Ametenga fedha nyingi amakwenda kuboresha maisha ya wanafunzi vyuoni, ameongeza wigo wa elimu bila malipo. Kwa hiyo, sisi vijana na watanzania kwa ujumla tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais, kwa maboresho haya ambayo ameyafanya kwenye elimu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Mheshimiwa Waziri wewe pamoja na Wizara nzima, Naibu Waziri wetu, Katibu Mkuu na watu wako wote tunawashukuru sana na kuwapongeza. Kwa sababu rasimu hii ya maboresho ambayo mmetuletea kwa kweli inatia moyo. Kimekuwa ni kilio cha muda mrefu sana cha watanzania kwa ujumla na hata Wabunge ambao ni wawakilishi wa wananchi, kwamba tuna maboresho ya haraka sana yanahitajika kufanyika kwenye mfumo wetu wa elimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru hata Sera yetu ya elimu bado na yenyewe ina recognize kwamba tunayo changamoto kwenye mfumo wetu wa elimu. Hii rasmu ambayo mmetuletea imekuwa exhaustive, inatia moyo kwamba tukienda kweli katika utekelezaji huu na mkiendelea ku-incorporate mawazo ya Wabunge wengi ambayo wanaendelea kutoa basi naamini kesho yetu ni bora zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kuchangia kwenye masuala machache tu, la kwanza; nilishauri katika mchango wangu wa kwanza nilipoingia Bungeni hapa kwamba, tunahitaji kuwa na agenda ya Kitaifa. Nitoe mfano kwenye nchi za wenzetu kwa mfano China, wao walikuwa na agenda kwamba ifikapo mwaka 2025 wangependa industrial product zote asilimia 75 zinazokuwa consumed duniani zote zitoke China na kwa kiasi kubwa nasema wamefanikiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tunazungumzia Tanzania ya viwanda, tukizungumzia kilimo, kiwanda kinachozalisha watu ambao wanakwenda kwenye sekta hizi ni Wizara hii ya Elimu ndio inatutayarishia watu hawa. Nafikiri kwa namna ambavyo tumeandaa hii rasmu yetu na kwa namna ambavyo na quote mwanzo kabisa wa sera ambayo ni rasimu inasema “Serikali imekusudia kuleta mapinduzi ya kiuchumi ili kuibadili Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa Kati ifikapo mwaka 2025” na inasema inatarajia kuleta maendeleo ya haraka ya rasilimali watu kwa kutayarisha idadi ya kutosha ya watanzania walioelimika na kupenda kujieleimisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya ni mawanda mapana sana tusiogope kuota. Tunapenda Tanzania tuione wapi ili Wizara hii ya Elimu itusaidie kuandaa watu hao. Tunapenda Tanzania leo hii tukizungumza duniani kama tunataka nini tuje tukipate Tanzania na wizara hii ndio wakati wake huu na hasa muda huu ambao tunafanya mapitio mtuandalie watu wa kwenda katika mlengwa huo. Kama tunasema tunataka Tanzania ya viwanda tunatakiwa tuanze kuanzie level ya chini kuanda watu hawa ili mwisho wa siku tuone Tanzania kweli ikielekea huko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe sana na wala hatutakuwa tumeji–stretch sana tunatia hatari ya kuwa jacks of all trades and master of none. Lazima tuweze ku–master. Sasa hivi Afrika inaongelea eneo huru la biashara Afrika. Lazima tuseme sisi Tanzania tukinda katika hii free movement of good, free movement of people tunataka Tanzania tuwe na speciality ipi? Ndio wakati sasa hivi wa kuandaa kupitia mabadiliko hata.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili; niombe sana sana Wabunge wengi wamechangia sana juu ya suala la lugha. Lugha yetu ya kitanzania ni lugha ya kiswahili na ni lugha ambayo tunaipenda we are very proud na lugha yetu lakini ni lazima tuangalie mabadiliko ya kidunia tunayoenda nayo. Sasa hivi tunakwenda kwenye dunia ambayo ni free movement of people, sio Afrika tu lakini dunia nzima kwa ujumla. Sasa tuki-incorporate lugha ya kiswahili peke yake tunamtenga mtanzania na dunia nyingine. Ni muhimu sana. Tuendelee kuitunza lugha yetu lakini tuendelee kuangalia lugha ambazo zitamfanya mtanzania aende katika dunia nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwapongeze kwa sababu katika rasimu hii mmekwenda mbali. Mmetoka katika debate ya Kiswahili na kiingereza mmekwenda kwenye kiarabu, kifaransa na kichina. Niwapongeze kwa sababu huko ndiko dunia inakotaka twende, kwenye hilo mmefaulu. Niombe mmesema anaetaka kufundisha kiswahili aombe kibali aruhusiwe anaetaka kufundisha kiingereza aombe kibali aruhusiwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani tunahitaji kufanya marekebisho katika hayo. Kwa sababu kama tunataka tuifungue Tanzania na kimsingi hii ni direction amekwisha tuonesha Mheshimiwa Rais anataka Tanzania tusikae kama kisiwa twende duniani. Sasa tukisema tu kwamba kuna baadhi ya wanafunzi watafundishwa kiswahili peke yake tunawatenga watu hawa na hawawezi kwena duniani, nadhani katika hili tuliangalie upya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine katika marekebisho haya tunayofanya stakeholder namba moja ni mwalimu. Yaani hatuta achieve chochote kama tusipoangalia maboresho katika hali za walimu. Wabunge wengi wamezungumzia katika kuboresha hali zao za kufundisha na mazingira yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi niko concerned zaidi kama tunapokwenda kwenye mabadiliko haya ambayo kwa kiasi kikubwa sasa yanakwenda kumfanya mwanafunzi aweze kupambana na mazingira yake. Je, anaemfundisha kwenda kupambana na mazingira yake yuko well equipped kumfundisha mwanafunzi ili akitoka akapambane na mazingira yake?

Mheshimiwa Mwenyekiti, hawa walimu tulianzisha mfumo wa competence based lakini as we speak mpaka leo less than 40 percent ya walimu walioko wameweza kupewa elimu ya kutosha kuweza kurudisha hizo knowledge kwa wanafunzi. Je, tunapokwenda kufanya maboresho haya, walimu tulionao wanakwenda kupata hizo knowledge kwa mfumo upi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, si hivyo tu, bado tuna upungufu mkubwa sana wa walimu. Tumewekeza sana kwenye miundombinu, tumewekeza sana kwenye kuboresha mazingira ya wanafunzi kusoma lakini bado tuna upungufu mkubwa sana wa walimu. Kama ambavyo tuliifanya agenda ya kitaifa kwamba tunatenga bajeti ya kutosha kwenda kuongeza madarasa, tunatenga bajeti ya kutosha kwenda kuongeza madawati, ningependa pia tuifanye agenda ya makusudi kwamba tunatenga bajeti ya kwenda kuongeza idadi ya walimu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuna sekta inayoweza kusimama kama kiwanda kinachotuzalishia wataalamu hakitasimama na kiwanda hiki si kingine ni Wizara hii ya Elimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa pia kutia msisitizo. Nashukuru kwa sababu rasimu hii imeanza kuonesha msisitizo wa mafunzo ya TEHAMA kuanzia level ya chini kabisa elimu ya awali mpaka mwisho. Lakini sasa dunia ya leo inakwenda kwenye information technology zaidi, dunia ya leo inakwenda kwenye artificial intelligence. Ni muhimu sana kuanzia elimu ya chini tuanze kuwafundisha wanafunzi wetu information technology. Tena sio vile vitu vya awali ambavyo tulikuwa tunajifunza mwanzoni kwamba, label hii ni CPU, hapana. Tunahitaji kwenda ndani zaidi kwa sababu dunia ndiko ilikofika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi kimsingi the future is closer than we think. Kwa sababu wenzetu sasa hivi wanakwenda ku–substitute kabisa binadamu kuweka mashine. Sasa sisi tunawaandaaje watu wetu kwamba tunakwenda kuwa substituted tuanze kutumia mashine. Ni lazima tuangalie kwa karibu sana na napenda tusiweke msisitizo huu vyuoni tu, tuanzie kwenye elimu ya chini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikupe tu data ndogo, mwaka 2015 wanafunzi waliokuwa wanamaliza shule za sekondari walikuwa ni wanafunzi milioni 1,648,000+ lakini mwaka 2019 sasa hivi wamemaliza wanafunzi milioni 2,185,000 hawa ni wanaomaliza elimu ya sekondari. Lakini wanaotoka vyuoni, mwaka 2015 walitoka wanafunzi 65000 tu kutoka milioni 1,600,000 wakatoka vyuoni wanafunzi 65,000, 2019 kutoka milioni 2.1 wakatoka vyuoni wanafunzi 87,000 hao zaidi ya wanafunzi milioni mbili wako wapi? Maana yake tumewaacha kwenye level za chini. Kama tunaanza kuwekeza lazima tuwekeze kuanzia level ya chini ili yeyote anayeweza kuishia chini basi atoke akiwa na skills za kutosha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa pia kuzunguzmia wanafunzi wetu Watoto wa kike. Tulipitisha hapa katika Bunge lako Tukufu Sheria ambayo inatoa adhabu ya miaka 30 kwa watu ambao watawapa ujauzito Watoto wetu wa kike ambao wako shuleni. Sheria hiyo ilikuwa ni nzuri na na malengo yalikuwa ni mema. Lakini Sheria ile pia ilipata resistance kwa kiasi fulani kwa sababu wanaharakati waliona kwamba tunatoa adhabu upande mmoja wakati wakosaji wanaweza kuwa wawili au huyu binti akijifungua basi huyu bwana yuko gerezani hivyo huyu mtoto atalelewa vipi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nachelea kusema kwamba tulishindwa kuangalia kitu kingine ambacho kingeweza kuwa matokeo ya jambo hili. Kitu hicho ni kama kifuatacho;

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi tafiti zinaonesha kuwa watoto wa kike wana invest zaidi kwenye kutokuonekana na mimba kuliko kuonekana na mimba. Kwa maana ya kwamba watoto wa kike sasa hivi wanatumia vidonge vya uzazi wa mpango, watoto wa kike wanatumia vidonge vya kutoa mimba ili asionekane na mimba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tukiangalia katika hii rasimu mpya uliyotuletea hakuna elimu ya kujitambua. Tumesahau kumuelimisha mtoto wa kike, kujitambua kuwa na self-awareness, kuwa na self-respect ili asiweze kuingia katika vitendo hivyo ku–begin with. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naona kama tuna risk sana kuwa na wanawake ambao watakuwa na matatizo ya cancer za uzazi, watoto ambao hawana maadili japokuwa mimba hatuzioni. Ninaomba sana katika hii rasimu mpya ambayo tunaitengeneza tuiangalie upya ili tuweke elimu ya kujitambua turudishe watoto wa kike katika maadili ya kitanzania, turudishe watoto wa kike katika kujitambua kwamba hili jambo si sahihi kuanzia mwanzo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kusema hayo naunga mkono hoja.