Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa fursa hii ya kuchangia kwenye mjadala huu wa hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nisichelewe kutoa pongezi kwa Mheshimiwa Rais wetu kwa kuweza kuchukua hatua za kimapinduzi katika sekta hii ya elimu ambayo tumekuwa nayo muda mrefu lakini kila wakati tumekuwa tunashangaa kwa nini hatuoni wajasiriamali wakijitokeza, hatuoni watu wakifanya mambo ambayo yametokea maeneo mengine duniani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninampongeza Mheshimiwa Waziri wa Elimu na Naibu wake pamoja na Katibu Mkuu na uongozi mzima wa Wizara hii. Kabla sijasema lolote niseme kwamba niliposoma hotuba ya Mheshimiwa Waziri nilikuwa nasisimka sana kwa sababu kuna vitu vingi ambavyo kusema kweli ni ubunifu na ni vitu ambavyo vitahitaji nguvu ya kifedha kutekeleza katika kipindi cha miaka hii inayokuja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nilipoangalia upande wa maduhuli, maduhuli yaliyokusanywa mpaka mwezi Machi, 2023, yalikuwa ni shilingi bilioni 338.2 ambayo ni asilimia 54 ya kilichokuwa kimekadiriwa ambacho ni shilingi bilioni 624.7. Kwa hiyo nikajiuliza kwa nini wakaendelea kuweka maduhuli makubwa hivyo kwa mwaka unaokuja, wameweka shilingi bilioni 667.3, ongezeko kubwa tu, lakini kwa jinsi ambavyo naona maduhuli yamekusanywa mwaka huu naamini hawataweza kufikia level hiyo na pengine wangepunguza hayo maoteo ya maduhuli.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niende kwenye hoja zangu; kwanza ni kweli kwamba tunaona kwamba kuna upungufu wa watumishi katika sekta ya elimu na sekta ya afya pia tunajua tuna upungufu mkubwa sana wa elimu. Lakini kwanza tujue kwamba tatizo siyo kwamba hakuna walimu Tanzania, walimu wapo, tatizo ni bajeti. Bajeti ina ukomo, ina constraints, huwezi kuweka pesa zote mahali pamoja na wakati kuna mahitaji mengi kwenye sekta nyingine za kilimo, maji na kadhalika na kote kunahitaji fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo bajeti ina ukomo na kwa sababu Serikali haiwezi kusema tunaajiri leo kila mtu anayetaka walimu 200 au 300 wapate. Kwa hiyo mimi na- sympathize sana na uongozi wa Serikali, kwamba tumeji- overstretch sana, tumejiongeza sana kwa kuingiza concept ya universal primary education na universal health care, siyo kitu ambacho hakina gharama, gharama zake ni kubwa. Nchi nyingi zilizoendelea hazijaweza kufanya mambo haya makubwa ambayo Serikali yetu inafanya, ndiyo sababu kweli tunatakiwa tuipongeze tumeji-overstrain lakini bado tunaendelea na ndiyo tunajikongoja hivyohivyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tuangalie kwa mfano katika upungufu wa walimu, mimi nafikiri kwamba tujiongeze zaidi. Kwanza kuna tatizo moja la kwamba walimu wale walio mtaani bado hawajapata uzoefu. Sasa kwa sababu hiyo mimi nina-suggest kwamba wale ambao wanatakiwa wastaafu kwa miaka 60 tuongeze kidogo ule muda wao wa kustaafu hata wakifika 65, lakini wale wana uzoefu na tukiwa- refresh kidogo wanaweza wakaendelea kufundisha, hasa yale masomo ambayo ni magumu kidogo kufundisha kama masomo ya sayansi, hesabu na kadhalika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hiyo, hatukujifunza wakati wa Covid watu walijifunza namna gani? walitumia artificial intelligence. Mahakama imeweza kutengeneza mfumo ambao unatafsiri Kiswahili kwenda Kiingereza hapo kwa papo. Kwa hiyo, wakitoa ile hukumu ya Kiingereza na ya Kiswahili inatoka hapohapo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo kuna mambo mengi yametokea duniani jamani, huku tunakoenda kweli ni kutumia teknolojia kufundisha, siyo lazima kuwe na mtu asimame pale. Kutakuwa na robot anafanya hesabu zake, kutakuwa na mtu mmoja anaangalia tu vizuri watu wamekaa wanasikiliza na baadaye kusaidia ku-interact. Otherwise mimi naamini katika miaka mitano inayokuja mtashangaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, artificial intelligence inakwenda mbali sana na internet inakwenda mbali sana. Kwa hiyo, hakuna sababu ya kujibana sana, tujue kwamba kuna uwezekano wa kupunguza gharama za uendeshaji, siyo tu kwenye elimu lakini pia kwenye afya kwa kutumia mifumo hii ambayo inajitokeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwamba Serikali pia imeona umuhimu wa kutia mkazo kwenye shule za awali, shule za awali mnajua hazikuwepo, zilikuwepo za kudanganya danganya hizi za private na nini, lakini shule za awali proper hazikuwepo na ninashukuru sana Wizara imeweza kutupa shule moja ya mfano pale kwenye Kata ya Kahe Magharibi kule Vunjo, lakini ukiangalia ile shule ilivyowekwa ni shule ambayo kweli watoto wengine wakienda wanaona wivu kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, kuna mkakati gani sasa wa Serikali kuhakikisha kwamba kwenye kila shule ambayo ni ya msingi kuna shule ya awali ya kuanzia wale wadogo ili kuweza kutekeleza sasa huo mkakati ambao pia watu wengi wanasisitiza kwamba uelewa wa mtoto unakuzwa kuanzia akiwa na miaka miwili au mitatu, siyo miaka mitano halafu hatajua kitu kabisa. Naomba hilo liangalie kwa sababu ni jambo ambalo ni la msingi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hiyo, kutekeleza hii mitaala mipya siyo kitu cha kufanya kwa siku moja, ni kitu ambacho kitahitaji muda wa mpito. Hatuwezi kusema mwaka huu tunaanza, hapana, hakitakwenda. Kwa sababu tunahitaji kuwaandaa hawa walimu na kuwa reskill na kuwa retune hawa walimu ambao tunao. Kwa sababu lazima tuwape nyenzo mpya za kufanyia kazi. Lazima tuwape elimu mpya namna gani kwa mfano mtoto mdogo unaanza naye, waangalie kipindi cha Ubongo Kids, mimi naangalia kipindi mpaka nashangaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, yule mtu anayetengeneza Kipindi cha Ubongo Kids ambacho kipo kwenye runinga nyingi za hapa kwetu, utaona kitu gani wanafanya, unaona wanafundisha watoto mpaka unashangaa unasema hata mtoto wangu akipita hapa akiangalia ataelewa maana ya utu ni nini na wanauliza maswali, na hiyo issue ya continuous assessment unaona kabisa pale inafanyika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo ninashukuru sana kwamba pamoja na hiyo nafikiri Serikali iangalie namna gani itaingiza kipindi hiki cha mpito kabla haijaanza kutekeleza.

Maandalizi gani, tunahitaji bajeti kubwa, hii bajeti waliyonayo Wizara hii ni ndogo kwa kipindi hiki ambacho tunakwenda. Kwa hiyo naamini kwamba watapata nyongeza zaidi ili waweze kujiandaa na waandae walimu na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la VETA. Wanasema wanajenga vituo vya VETA kwenye Wilaya. Wilaya yetu ina Jimbo moja Moshi Municipal halafu ina Halmashauri ya Moshi Vijijini ambayo ina Majimbo mawili. Sasa unaposema unatoa VETA moja inaenda pale Mjini Moshi basi. Kwa hiyo yale Majimbo mengine hayana kituo cha VETA ni makubwa watu chungu nzima. Unajua mtu anakwenda kusoma VETA ukamwambia achukue transport kila siku aende Mjini kusoma inakuwa vigumu sana, gharama zinakuwa kubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo mimi naomba tuangalie upya, kwamba pale ambako una Majimbo matatu au mawili kwenye Wilaya basi tuangalie namna gani tuta- allocate hivyo vituo vya VETA ili viweze kunufaisha watu. Hakuna sababu ya kuwa na kituo cha VETA ambacho kukifikia yule mwanafunzi lazima atumie shilingi 5,000, itakuwa ni kazi ngumu, kama kule kwangu ni vigumu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo namuomba Mheshimiwa Waziri aangalie hilo suala ili aweze kuona kwamba kweli wasituwekee kila kitu pale Mjini, Mimi sichukii kuwekwa Mjini lakini ukweli ni kwamba nataka tujue kwamba distribution spatially itakuwaje, in terms of spatial benefits.

Mheshimiwa Mwenyekiti, halafu nashangaa tunavyozungumza ufundi stadi. Hivi hakuna vyuo vya kilimo? Kwa nini hatuna vyuo vya kilimo vile ambavyo tunachukua kwenye hii kada ya kati? Kama vipo, ni vichache. Watu watajifunza saa ngapi? Au kilimo hatujifunzi? Au tutajifunzia huko huko tulikozaliwa? Sasa hivi kimekuja kilimo cha umwagiliaji, kilimo ambacho ni chenye tija, kinaendeshwa na watu wanaofundishwa na wakajua faida zake nini? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naamini kwamba tunapozungumzia Vyuo vya VETA, tujaribu kuweka vyuo vya kufundisha kilimo kwenye ngazi ya chini kabisa kuanzia hata darasa la saba au hata kuanzia darasa la tano kwenda juu huko, na wale wanaobobea zaidi wanakuwa ndio wataalam, mabwana shamba na kadhalika, tunawapeleka, lakini usitaje tu vituo hivyo. Tena vinahitaji hela sana hivyo vya VETA. Hivi vya kilimo hata havihitaji nyenzo nyingi sana, ni vitu vichache. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu kingine kwamba pengine kwenye suala zima la bajeti hii niliangalia kwamba, pengine ili kuleta tija kwenye elimu, walimu kuendelea kuripoti kwa TAMISEMI au kusimamiwa na TAMISEMI, naona hiyo, kwanza unapoteza kabisa mwelekeo wa walimu hapa. Ila kama wenzangu walivyosema, walimu kusema kweli ingefaa waangaliwe na wawe graded na Wizara ya Elimu, wasibakie tu kwenye sera lakini walimu wawe pale kwa sababu tutajua jinsi ya kuwafundisha na kadharika nakadharika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.