Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Afya

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Afya

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, nawapongeza sana Wizara kwa hotuba ya Bajeti, lakini zaidi kwa ile programu ya mentorship ambapo tuliwaona madaktari ambao wataenda kila Wilaya kufanya mafunzo kwa mwezi mmoja.

Pili Mheshimiwa Waziri ameeleza kuhusu wahudumu wa ngazi ya jamii (CHWs), hata hivyo naomba awaondoe shaka wahudumu waliopo, na hii ni kwa kuzingatia message hii ambayo nimetumiwa na mmoja wa CHWs.

"Habari za kazi! Naomba mnisaidie kwa Wizara ya Afya, Aaziri alitangaza kuwa wahudumu wa afya ngazi ya jamii watatangaza kwa vijana waliofika kidato cha nne, na watawalipa. Sasa wahudumu waliojitolea tangu mwaka 1986 na wapo je, hawa Wizara inawafanyia nini inapowastaafisha, mimi mwenyewe nimefanya tangu 1992 kwa kujitolea, na Wilaya ya Mufindi wapo kila Kijiji."

Mheshimiwa Spika, nadhani ipo sababu ya kuwaondoa shaka hawa waliopo.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.