Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Afya

Hon. Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Afya

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Spika, nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Rais, Waziri wa Afya Mheshimiwa Ummy Mwalimu na wote wanaomsaidia wakiwemo madaktari na wauguzi wote wa Wilaya ya Nyasa.

Mheshimiwa Spika, maoni yangu; kwanza fedha inayotengwa itolewe kama ilivyokusudiwa; pili, Serikali iweke jitihada kubwa katika kutoa kinga na pia kutoa mafunzo ya ujuzi kwa mabwana na bibi afya ili kuifikia jamii kubwa zaidi. Lakini kuhusu kuwatumia waliomaliza kidato cha nne ni vema kuwatumia waliopata ujuzi wa vyeti vya fani za utabibu na afya pamoja na kuwaongezea ujuzi huo unaohitajika. Hao wapo wengi huko vijijini.

Tatu, Wilaya ya Nyasa inaomba vifaa tiba muhimu x-ray, utra sound, ambulance na fedha za vifaa vya vituo vya afya na zahanati zilizikamilika Vituo vya Afya Kingirikiti na liparamba.

Mheshimiwa Spika, nne, Hospitali ya Wilaya ya Nyasa imeshaanza kutoa huduma za afya ya kinywa. Changamoto ni hakuna vifaa tiba kabisa. Tunaomba ahadi ya kupatiwa shilingi 50,000,000 tuliyoahidiwa; tano, Wilaya ya Nyasa ina upungufu mkubwa wa watumishi wa afya, ni vema Wizara iwaongeze watumishi wa afya.

Mheshimiwa Spika, sita, kwa nini Serikali isifikirie kuwa na mfuko maalum wa tozo angalau shilingi mia moja tu kwa ajili ya kupunguza changamoto ya kifedha hasa katika kuboresha huduma za afya vijijini na kwa magonjwa maalum kama saratani, figo na kadhalika, tukubali kukata kupitia mafuta au mawasiliano. Najua changamoto zake, lakini tukiamua inawezekana. Tusijifungie kwenye bima ya afya tu. Afya ya mtu ni utu na heshima ya uhai. Inaumiza sana kuona mtu anapoteza maisha kwa ajili ya kukosa uwezo wa kifedha. Umuhimu wa uhai hauchagui hali ya kiuwezo wa kifedha.