Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Afya

Hon. Dr. Florence George Samizi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Afya

MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI: Mheshimiwa Spika, ninapongeza kwa juhudi zote zinazofanywa na Serikali katika kuimarisha afya nchini. Ombi langu tunaomba wale wataalamu waliohitimu katika Kituo cha Sekomu Lushoto, Tanga, kama Mental Health and Rehabilitation Officer, wapo kama 143 nchi nzima, watambuliwe kwenye Muundo wa Kazi au Work Scheme ili waweze kuajiriwa kwa utaalamu wao. Kwa sasa wanafanya kazi kwa taaluma au madaraja mengine kama Maafisa Tabibu ngazi za Wilaya ambayo sio yao kwa sababu ya kukosa muundo huu.

Mheshimiwa Spika, ahsante na naomba kuwasilisha.