Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Afya

Hon. Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Afya

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa fursa na nianze moja kwamoja kwa kumpongeza sana Waziri wetu wa Afya, Mheshimiwa Ummy Mwalimu kwa ripoti nzuri aliyowasilishwa. Ile ripoti ilikuwa imejaa kila kitu nami nimepata uelewa mkubwa sana wa vitu ambavyo Wizara ya Afya inafanya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nirudie kumpongeza Mheshimiwa Ummy Mwalimu, Naibu wake Dkt. Godwin Mollel, Katibu Mkuu Dkt. Shekalaghe, Mganga Mkuu wa Serikali Dkt. Tumaini Nagu, Taasisi zote zilizopo chini ya Wizara ya Afya, Madaktari wote nchini na manesi na wafamasia kwa kazi nzuri wanayofanya. Kusema ukweli Udaktari ni kazi ya wito na hawa watu wanatutendea haki sana. Hongera sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nisitoke hapa bila kumpongeza Rais wetu, Rais wetu ameona umuhimu wa hii Sekta ya Afya na ametoa pesa za kutosha kabisa kusaidia Watanzania ili wapate huduma. Nampongeza Rais kwa sababu kwenye bajeti hii ambayo wanatuomba tuwapitishie, Mheshimiwa Rais ametenga shilingi 1,235,000,000,000 ikiwa ni nyongeza. Mwaka jana hii bajeti ilikuwa ni trilioni…

(Hapa umeme ulikatika)