Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maji

Hon. Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maji

MHE. DKT. ANGELINE S. L. MABULA: Mheshimiwa Spika, nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia afya njema, aidha, namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutupa Rais mwenye maono na anayewapenda na kuwajali watu wake. Kazi nzuri iliyofanyika katika kuondoa kero ya maji sehemu mbalimbali ni jambo la kujivunia kama Watanzania tukizingatia kuwa maji na uhai.

Mheshimiwa Spika, mbali na sekta ya maji Mheshimiwa Rais amefanya maajabu katika sekta zote za miundombinu, elimu, afya, ardhi, kilimo na kadhalika. Mwenyezi Mungu amjalie afya njema na aendelee kulitumikia Taifa letu.

Mheshimiwa Spika, ninampongeza sana Waziri wa Maji yeye binafsi, Naibu Waziri, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu na timu nzima ya Wizara kwa kazi nzuri ya kumtua mama ndoo, mwenyezi Mungu awajalie afya njema muendelee kulitumikia Taifa letu.

Pili, ninakushukuru sana kwa kuweka katika bajeti Mradi wa Kabangaja wa chanzo kipya cha maji utaondoa adha ya maji Manispaa ya Ilemela.

Mheshimiwa Spika, ombi langu, wakati tunasubiri kukamilika kwa mradi mkubwa wa chanzo cha maji cha Butimba, naomba sana kupatiwa visima virefu angalau kumi tu kwa kata zilizoko pembezoni (peri urban) mwa mji ambazo hazina maji ya bomba kabisa wanatumia visima visivyo rasmi, itapendeza nao wakapata maji ya visima. Maeneo husika ni eneo la Kata za Nsumba, Kiseke; Lutongo, Kayenze; Lugeye, Sangabuye; Ilekako, Bugogwa; Isanzu, Bugogwa; Bulyanghulu, Shibula; Ibaya, Shibula; Wiluhya, Kahama; Magaka, Kahama; na Nkoronto, Bugugwa.

Mheshimiwa Spika, naomba sana Wizara ione namna ya kuwasaidia wananchi wa Ilemela ambao ziwa liko hatua chache kutoka makazi yao lakini hawana maji.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha na ninaunga mkono hoja.