Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maji

Hon. Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maji

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Spika, naomba nianze mchango wangu kwa kumshukuru sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi nzuri inayofanyika kwenye sekta ya maji. Kwenye Wilaya ya Hanang inategemewa miradi mikubwa ambayo inaenda kutatua kero kubwa ya maji kwa wana-Hanang.

Mheshimiwa Spika, miradi ya maji Hanang; Wilaya ya Hanang ina Mradi wa Mogitu - Gehandu, Gawlolo, Mureru, Ziwa Bassotu, Bwawa la Bassotughang, Basodesh, Gijetamhog, Mamlaka ya Mji Mdogo wa Katesh na vijiji vingine ambavyo jumla zimechimbwa visima 24 na utaratibu unafanyika wa kuchimba visima vingine 16 ili jumla tutakuwa na visima 40 ndani ya miaka mitatu. Wana-Hanang wanaendelea kusubiri kwa hamu kukamilika kwa miradi hii ili maji yawafikee wananchi.

Mheshimiwa Spika, maombi mahsusi; Bwawa la Gidahababiye ambalo usanifu wake umekamilika muda mrefu tupate fedha ya kuujenga, imekuwa ni ahadi ya muda mrefu sana, pia mnaweza kushirikiana na Wizara ya Kilimo ili litumike kwa ajili ya umwagiliaji.

Kuhusu miradi inayoendelea ikamilike kwa wakati hasa Mamlaka ya Mji wa Katesh ambayo ili mradi ukamilike inahitajika tu 570,000,000 ukizingatia mpaka sasa tumeshatumia zaidi shilingi bilioni tano kwenye mradi huu.

Mheshimiwa Spika, kasi ya ujenzi wa mradi wa Ziwa Bassotu ni ndogo sana ikilinganishwa na mahitaji, tuendelee kutenga fedha za kutosha ili uweze kukamilika; na tupate gari ili kurahisisha utendaji kazi kwa RUWASA ndani ya Wilaya.

Mheshimiwa Spika, naomba kuunga mkono hoja.