Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maji

Hon. Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maji

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru wewe na Mheshimiwa Rais kwa kutoa shilingi bilioni 100 kwa Mradi wa Maji Geita Mjini, mkandarasi yupo, tatizo kwa mwaka mzima sasa hakuna kazi ya kuonekana imeanza kufanyika.

Mheshimiwa Spika, zipo taarifa za kuchelewa kuanza kwa mradi sababu ya fidia ndogo sana ya vibanda vya wavuvi nane na nyumba moja, naomba Wizara ilifanyie kazi.

Mheshimiwa Spika, naomba kumkumbusha Mheshimiwa Waziri ahadi yake ya ukarabati wa Bwawa la Kasamwa, aliahidi ndani ya Bunge na wananchi wa Kasamwa wanategemea utekelezaji wa ahadi yako.

Mheshimiwa Spika, umekuwepo mradi wa maji katika Kata ya Bulela ambao awali uliwekwa kwenye bajeti ya maji, Wizara kupitia RUWASA shilingi milioni 510; fedha hizi kwa miaka mitatu sasa bado haujatekelezwa, kata hii ina kituo cha afya, shule ya wasichana ya bweni na josho.

Mheshimiwa Spika, Kata za Nyanguku na Ihanamilo visima vinakauka kiangazi kwa kuwa ni vifupi. Naomba Mheshimiwa Waziri maeneo haya yafanyiwe kazi.