Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maji

Hon. Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maji

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Spika, napenda kumpongeza sana Mheshimiwa Rais kwa uamuzi wake wa busara wa kuendelea kutenga fedha za ujenzi wa Bwawa la Kidunda, bwawa ambalo ni faraja kubwa kwa wakazi wa Mkoa Dar es Salaam na Pwani kupata maji kwa wakati wote.

Mheshimiwa Spika, nampongeza sana Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Makatibu Wakuu na watendaji wote wa Serikali kwa kazi nzuri kuhakikisha kuwa Mkoa wa Dar es Salaam tunapata maji safi na salama isipokuwa changamoto yetu kubwa ni kupungua kwa maji na mabomba kupasuka na kupoteza maji mengi sana; naiomba Serikali iendelee kupambana na changamoto hizo.

Mheshimiwa Spika, naomba Serikali ikamilishe miradi ya maji ya Dar es Salaam pamoja na Mradi wa Visima vya Maji vya Kimbiji na Mpera sasa ukamilike na maji yasambazwe kwenye Wilaya ya Kigamboni yote na Temeke, Mbagala pia Jimbo la Ukonga.

Mheshimiwa Spika, ushauri wangu Serikali ikafanye utafiti wa maji tuweze kuchimba visima virefu maeneo ya Mvuti Dondwe nao wananchi wa Ilala wapate chanzo kipya cha maji. Ni matumaini yangu chanzo hicho kitawasaidia sana.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja naipongeza sana Serikali kwa utekelezaji na juhudi zake, endeleeni hivyo Mungu atasimama nasi.