Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maji

Hon. Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maji

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Spika, naipongeza Wizara kwa kazi nzuri mnayoifanya. Wizara ina viongozi wasikivu katika kusikiliza hoja za Wabunge kuanzia ngazi ya Wizara, Mikoa na Wilaya.

Mheshimiwa Spika, mchango wangu utajikita katika maeneo mawili; kwanza ni kuhusu Mradi wa Makonde. Tunaipongeza Wizara ya Maji kwa kuanza kutekeleza mradi huu ambao unanufaisha wakazi wa Halmashauri za Nanyamba; Newala na Tandahimba. Mradi huu kwa usanifu wa sasa unaonekana inaishia kwenye baadhi ya maeneo tu na kusema kuwa sehemu zingine itakuwa Phase II. Tunaomba kazi hiyo ifanywe kwenye Phase I ukizingatia kuwa Wilaya nufaika na mradi huu upatikanaji wa maji upo chini ya asilimia 50.

Pili ni kuhusu mradi wa kutoa maji Mto Ruvuma na kupeleka Mtwara Manispaa, mradi huu ni wa muda mrefu na bado haujaanza kutekelezwa. Mradi huu utanufaisha Halmashauri ya Nanyamba, Mtwara na Manispaa ya Mtwara, mradi huu sasa utengewe fedha ili uanze kutekelezwa.