Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maji

Hon. Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maji

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Spika, kwa sababu ya ufinyu wa muda sikuweza kumaliza mambo machache ambayo nilitaka kuyasema hususan mahitaji ya visima virefu, kwa hiyo, kwa ridhaa yako naomba maandishi haya yawe sehemu ya mchango wangu.

Mheshimiwa Spika, tuna uhitaji mkubwa wa visima virefu katika vijiji vfuatavyo; Kijiji cha Oldonyongiro ambako pia kuna kituo kipya cha afya cha Mareu Kata ya Kingori; Kijiji cha Ngyani Kata ya Nkoaranga; Kijiji cha Nkoaranga; Kijiji cha Kilinga; na Kijiji cha Poli.

Mheshimiwa Spika, miundombinu ya kuwapatia maji wananchi walioko katika vijiji ambavyo bomba kubwa la mradi mkubwa wa shilingi bilioni 520 Mradi wa AUWSA linapita Makiba, Mbuguni, Msitu wa Mbogo, Karangai Maweni, Kikwe na Nambala.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.