Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maji

Hon. Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maji

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Spika, kwanza niwapongeze kwa kazi kubwa inayofanywa na Wizara ya Maji chini ya Waziri Aweso, kipekee sana kwa heshima na taadhima wananchi wa Iringa tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa unayofanya ya kuliongoza Taifa letu, na kusimamia maendeleo ya Taifa letu, na hususani katika Manispaa yetu ya Iringa. Tunashukuru kwa kuwa maji ndani ya Jimbo la Iringa imekidhi utekelezaji wa Ilani.

Mheshimiwa Spika, maombi; kwanza, tunaomba maji yafikishwe kwenye maeneo ya vijijini ndani ya Jimbo la Iringa ambayo ni eneo la Ugele, Kata ya Mkimbizi na Mosi Kata ya Kitwiru. Pia ninaomba kisima katika eneo letu la Uwanja wa Samora pale tulipofanyia mkutano ulipotuahidi kutuletea visima, siku ya ziara ya Rais, pamoja na zile shule tulizoomba kuchimbiwa visima.

Mheshimiwa Spika, Mkurugenzi wako IRUWASA amesema maji yapo kwenye shule hizo, na wamefungiwa prepaid, lakini hawatumii kwa kuwa bills hawawezi kulipia.

Pili, ninatoa ushauri kuwa katika bill ya maji muongeze hata shilingi 10 au tano kwa unit ili fedha hizi zichangie huduma za maji mashuleni, kwenye zahanati na vituo vya afya. Shule hizi zinawekewa miundombinu ya kisasa sana inayohitaji matumizi ya maji. Sasa kutegemea capitation pekee yake itakuwa vigumu sana.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.