Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maji

Hon. Khadija Hassan Aboud

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maji

MHE. KHADIJA HASSAN ABOUD: Mheshimiwa Spika, kwanza nachukua fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa juhudi na hatua mbalimbali anazochukua kuhakikisha wananchi wanapata maji safi na salama.

Mheshimiwa Spika, nampongeza Mheshimiwa Waziri na watendaji wake wote kwa kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Mheshimiwa Spika, naomba kuishauri Serikali; kwanza Wizara iendelee na jitihada za kudhibiti upotevu wa maji; pili, kulinda na kuhifadhi vyanzo vya maji; na tatu, kuongeza matumizi ya mita za LUKU (prepaid meter) kwa matumizi ya majumbani ili kuepusha mtumiaji wa maji kuchelewa kulipa bili za maji pia kumsaidia mwanachi kulimbikiziwa madeni ya maji.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja, ahsante.