Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maji

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maji

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, naomba kuwapongeza Wizara kwa kazi nzuri lakini kubwa kwa ushirikishwaji wa sisi Wabunge kuanzia ngazi ya Wizara mpaka Mameneja wa RUWASA Mikoa na Wilaya na pia kwa Wakurugenzi wa Mamlaka za Maji. Tunaona team work na kwa mwendo huu sekta hii itaendelea kuimarika, tuendelee ushirikishaji wa sisi Wabunge, lakini pia katika ngazi za Wilaya kwa maAna ya Halmashauri, Madiwani na Ofisi za ma-DC wote wawe wanaelewa katika maeneo yao kuna miradi gani, itatekelezwa kwa namna gani na kwa muda gani. Hii itatusaidia kuwa wamoja. Na kwa kuwa tunatekeleza Ilani ya CCM basi ni muhimu sana viongozi wa chama katika maeneo ambako mradi unatekelezwa kuwa na ufahamu kwa maana ya ownership, vivyo hivyo viongozi wa ngazi za chini kwa maana ya Wenyeviti wa Mitaa na Vijiji. Nasema hivi kwa sababu kazi kubwa inafanyika, kwa hiyo, tusipokuwa na muunganiko wa taarifa hakika watu wengi na hasa wapotoshaji watazungumza tofauti.

Mheshimiwa Spika, kuhusu Mradi wa Miji 28 Mafinga; tunashukuru sana kazi imeanza japo wananchi wanatamani sana kuona physical works kama uchimbwaji wa mitaro na kadhalika. Tunawaelimisha kuwa mradi huu ni miezi 20 na kwamba ni design and construction, tunawafafanulia.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, matarajio ya wananchi ni kwamba mradi huu ni mkombozi wa kero ya maji, lakini kwa upande mwingine, scope ya utekelezaji kwa maana ya distribution ni kilometa 20 tu. Kwa ukuaji wa Mji wa Mafinga kutokana na viwanda vya mazao ya misitu, nashauri Serikali ianze kufikiria awamu ya pili ya mradi ambayo itajielekeza katika ujenzi wa matanki na usambazaji, nawapongeza timu yangu ya MAUWASA wanajituma sana hasa katika kuwasiliana na Wizara kuhusu fursa mbalimbali zinazojitokeza. Mradi huu wa miji 28 ni mkubwa sana, haitaleta picha nzuri ikiwa baada ya kukamilika maeneo mengi ya mji yafikiwe na huduma, sote tunatambua ambavyo signing ceremony sio tu ilihudhuriwa na Mheshimiwa Rais, lakini pia wananchi walishuhudia live, na hivyo wamejenga matumaini makubwa sana, lakini wanaposikia kuwa kuna maeneo mradi hautafika inawakatisha tamaa, ndio maana nashauri mapema, tuanze kuona kwa namna gani tutapata phase two kama mwendelezo wa mradi huu.

Mheshimiwa Spika, nafahamu kuimarisha chanzo ndio jambo kubwa, distribution na matanki sio kazi kubwa sana, tukitengewa around shilingi bilioni 10 yaani bilioni kumi kuanzia mwaka ujao wa fedha, tutaweza kufikisha maji eneo kubwa la mji.

Mheshimiwa Spika, kuhusu RUWASA; nawapongeza kwa maeneo ya vijijini, hata hivyo kilio kikubwa ni kukamilisha Mradi wa Matanana na Itimbo ambao ni wa visima, lakini kilio zaidi ni Kijiji cha Kisada, nilitaraji kuwa kitakuwepo katika mpango wa mwaka wa fedha ujao, lakini sijaona Kisada kwa hiyo naomba iwepo, lakini la pili pamoja na kuwa RUWASA ipo kiwilaya. Nashauri miradi kati ya Halmashauri mbili isichaganywe, kwa mfano kuweka vijiji vya Mafinga TC katika orodha ya vijiji vya Mufindi DC inaleta mkanganyiko, na hili lilishajitokeza mwaka jana, mradi wangu wa Kitelwasi Ugute ukaachwa kwa kile kilichotajwa kama oversight, hivyo ushauri wangu tupange mipango kwa kuzingatia kijiji kipo Halmashauri gani.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.