Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maji

Hon. Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maji

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Spika, kipekee nikushukuru kwa kunipa hii nafasi ili nichangie kwenye Wizara ya Maji. Pia nichukue nafasi hii kipekee vilevile nimshukuru sana Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kazi nyingi ambazo anazifanya. Katika Jimbo langu la Manyoni Mashariki tulikuwa na miradi mingi ya maji kichefuchefu, lakini nikwambie sasa hivi miradi mingi ya maji katika Jimbo la Manyoni Mashariki inaenda vizuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimshukuru sana Mheshimiwa Waziri Aweso, ndugu yangu, lakini na Naibu Waziri, Mheshimiwa Engineer Mary. Wengi wamesema hapa hawa vijana wetu, ndugu zetu wanafanya kazi nzuri sana. Kwangu Mheshimiwa Aweso nadhani anaenda kuweka historia kubwa sana ya kutatua kero ya maji Manyoni. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna Mradi wa Kintinku - Lusilile na siku hizi unaniita mzee wa Kintinku - Lusilile. Huu mradi una miaka 15 ulishindikana kukamilika wa bilioni 12, lakini hapa ninapovyoongea mwezi uliopita mkandarasi alipewa bilioni mbili kwa ajili ya kwenda kukamilisha Mradi wa Kintinku - Lusilile. Nimwombe Mheshimiwa Waziri, huu mradi wa bilioni 12 ni mradi mkubwa sana, ukikamilika amwombe Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia aje auzindue huu mradi kwa sababu atakuwa ameweka historia kubwa, lakini ameweka heshima kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimshukuru Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Engineer wetu, lakini nimshukuru sana Mkurugenzi wa RUWASA. Kwa kweli, huyu Mkurugenzi ni msikivu sana, anatusaidia sana na Mheshimiwa Waziri kwa kweli, ana Mkurugenzi ambaye anamfanyia kazi nzuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nina mambo mawili ambayo ningependa kuchangia leo. La kwanza, nimeshaeleza kuhusu hii miradi yangu ya maji, tuna huu Mradi wa Kintinku - Lusilile; huu mradi ulikaa miaka 15 ulikuwa umeshindikana kukamilika, mradi wa vijiji 11, lakini nimesema tumepewa bilioni mbili na mkandarasi yupo site ameshaanza kufanya ile kazi ya kumalizia. Amesaini mkataba wa kumaliza huu mradi ifikapo Oktoba mwaka huu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nikuombe sasa tuisimamie Serikali, lakini nimwombe Waziri amsimamie mkandarasi. Nimshukuru yule mkandarasi aliyenipa ni msikivu sana, anafanya kazi nzuri sana. Kazi ilikuwa ngumu, lakini ameweza kuusukuma ule mradi.

Mheshimiwa Spika, tuna Mradi pia wa Miji 28 ambao na wenyewe tulipata pale Mamlaka ya Mji Mdogo wa Manyoni. Wakandarasi walishakuja, lakini nimwombe Mheshimiwa Waziri awasukume wale wakandarasi kwa kuwa wananchi wamesubiri sana huu mradi kwa muda mrefu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna vijiji ambavyo tumechimba visima vya maji kwa muda mrefu tumekosa. Kuna Kijiji cha Mpapa, Kijiji cha Igwamadete, Kijiji cha Mazwichii, Kijiji cha Kitalalo, Kijiji cha Magasai, kwa kweli, hivi vijiji tumefanya survey ya maji muda mrefu na kwa bahati mbaya hatujapata maji. Nimwombe Waziri sasa watafute namna ya kuhakikisha kwamba, hawa wananchi ambao wamesubiri muda mrefu kupata maji, tuje na ubunifu wa kuweza kuwasaidia waweze kupata maji.

Mheshimiwa Spika, suala la pili na la mwisho ni kuhusu Mfuko wetu wa Maji wa Taifa (National Water Fund). Wabunge wengi wanaposimama hapa kuchangia wanatamani kuona tunakwenda kutatua tatizo la maji kwenye Majimbo yao, ili tuweze kutatua tatizo la maji kwenye Majimbo yao tunahitaji kuwa na financing system ambayo iko very stable and sustainable. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tunahitaji kumsaidia Mheshimiwa Waziri. Sheria ya kuanzisha Mfuko wa Maji ya 2019 inasema kwamba tutapata kutoka kwenye fuel levy angalau shilingi 50 kwa kila lita. Mimi naona tuna tatizo. Mfuko wa Maji wa Taifa ndiyo Mfuko ambao unatakiwa uwe very sustainable kwa ajili ya kusimamia miradi ya maji Tanzania. Ukiacha kwamba tunapata fedha kutoka kwa wafadhili, lakini hiki ni chanzo ambacho sisi kama Watanzania tunahitaji kukisimamia. Nadhani kuna jambo la kufanya kwenye huu Mfuko wa Maji.

Mheshimiwa Spika, ushauri wangu ni nini; kwanza tuna Jumuiya za Watumia Maji. Kwa mfano, kwa Manyoni nina Jumuiya moja ya Watumia Maji inaitwa Mkombozi, sasa hivi wana milioni 140 kwenye akaunti yao. Nina Jumuiya moja ya Watumia Maji kutoka Kijiji cha London, wana milioni 125 kwenye akaunti yao, nina jumuiya moja kutoka Sorya wana milioni 60 kwenye akaunti yao. Idea yangu ni nini kama tunataka kusaidia Mfuko wa Maji ku-expand ile financing mechanism yao tunahitaji vilevile ku-diversify, kutafuta vyanzo mbalimbali vya maji. Nashauri nini, zile fedha ambazo tunazikusanya kwa kupitia Jumuiya za Watumia Maji zinakuwa idle, kwa nini tusitengeneze mfumo zile jumuiya za maji vilevile zichangie kwenye Mfuko wa Taifa wa Maji? Ninashauri kwa kupitia hili tunaweza tukakusanya fedha nyingi ambazo hizohizo zitasaidia kwa ajili ya kuchimba visima kulekule na kwa ajili ya expand hata utoaji wa huduma ya maji vilevile. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ukiangalia kwenye Sheria ya Kuanzisha Mfuko wa Maji, imetoa provision kwamba zaidi ya asilimia 88 ya fedha itakayokusanywa iende kwenye miradi ya maji, of which mimi naona ni kitu kizuri, kwamba tunaweza tukafanya mambo makubwa sana kwenye suala la kupeleka miradi ya maji. Kwa kupitia hili nina uhakika sasa kilio hiki cha Wabunge wengi kwamba miradi haikamiliki na kadhalika, nadhani tunaweza tukatatua. Mbali ya kutegemea fedha za wahisani tu, lakini tutakuwa na uhakika wa kutegemea fedha ambazo zinatokana na miradi yetu ileile ya kule. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mwisho, mimi nirudie tena kumshukuru Waziri. Kwa kweli kwa sisi watu wa Kintinku – Lusilile kwenye ule mradi wako mkubwa wa bilioni 12 umetutendea haki sana. Ninakuombea wewe na Naibu Waziri wako muendelee kutusaidia, ule mradi wa maji ikifika Oktoba mwaka huu tukaweke historia na Mheshimiwa Rais aje auzindue ule mradi.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, naunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)