Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maji

Hon. Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maji

MHE. FRANCIS I. MTINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi niweze kuchangia katika Wizara hii ambayo ni uhai wa Watanzania, kwa sababu wote tunajua kwamba maji ni uhai. Naomba nianze kwa kumshukuru sana Waziri kwa jinsi ambavyo amekuwa akifanya kazi vizuri yeye na timu yake kazi ya kuwasikiliza Watanzania na kuwapelekea maji kama ambavyo Rais wetu amemuagiza.

Mheshimiwa Spika, nimshukuru pia watendaji wake katika ngazi ya Mkoa. Namshukuru sana Meneja wa RUWASA wa Mkoa wa Singida ni mtu rahimu sana, anasikiliza watu na hivyo wananchi wa Mkoa wa Singida wanampenda sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, aidha nimpe tena salamu Mheshimiwa Waziri kutoka Wananchi wa Mkalama uliwahamishia Meneja wao Engineer Mchunguzi. Wamenituma mimi ndiyo msemaji wao wanamuhitaji meneja wao arudi kwa sababu wana jambo lao. Kwa sababu anawasikiliza vizuri wangekuwa tayari sana kama angekuwa amepandishwa cheo wangemuacha aende lakini kwa sababu ameamishwa anaendelea kuwa Meneja kama alivyokuwa Mkalama na mimi kwa sababu ni msemaji Madiwani, Chama cha Mapinduzi na wananchi walimwambia mpaka Katibu Mkuu wa Chama kwamba wanamtaka Menejaager Mchunguzi arudi. Kwa hiyo, nimefikisha hili nijivue kwamba wanamuhitaji meneja wao Engineer Mchunguzi kwa sababu walimuelewa anafanya kazi vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sisi hatuna shaka hatujui aliyekuja lakini wenyewe wanamtaka wakwao waendelee nae. Kwa hiyo, nimeona hilo nikwambie ulijue na najua DG wa RUWASA yupo nilimpigia simu akanihaidi lakini mpaka sasa haijatekelezwa kwa hiyo nimeona niifikishe.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri nikushukuru kwamba umeendelea kutupatia pesa, umetupatia milioni 165 kumalizia mradi wa maji pale Nkalakala tunakushukuru sana, umetupatia milioni 240 kumalizia mradi wa maji pale Maraja tunakushukuru sana. Vilevile nikushukuru nimekusumbua sana ukanipatia milioni 208 kuanza mradi pale Mbigigi wakati naingia Ubunge nilikuta umefanyika upembuzi wa kina na yalipoanza kujengwa maji kule kwenye kijiji nilikozaliwa wakadhani nimehamisha hela za Mbigigi. Kwa hiyo, nakushukuru sana umezileta milioni 208 na sasa mkandarasi anakwenda kukabidhiwa kazi kwa ajili ya mradi ule nakushukuru sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, katika bajeti hii umetupitishia shilingi milioni 208 bajeti hii itakapopita kwa ajili ya kwenda kupeleka maji katika kijiji cha Matongo na Isene watu hao wamepata shida sana ya maji kwa kutumia chanzo cha Isene sasa tutajenga mradi wa tank pale umetushia milioni 208 na itahudumia vijiji viwili nikushukuru sana kwa ajili ya hilo.

Mheshimiwa Spika vilevile umetupitishia milioni 300 kwenda kujenda miundombinu na umaliziaji katika jiji cha msingi kata ya Msingi nakushukuru sana wewe ni mtu rahimu sana. Vilevile umetupitishia milioni 378 kwa ajili ya kupanua mradi wa maji wa Tumuli ambao umeishajengwa sasa kwenda kuongeza vituo na ile kata nzima iweze kupata maji safi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, haikutosha Mheshimiwa Waziri wewe ni mtu wa Mungu sana umetupitishia milioni 396 kwa ajili ya kwenda kuchimba visima kwenye vijiji vya Domoniki, Nkinto, Ilunda, Kitundili, Kisulwiga, Mwangeza, Kibii, Gumanga, Asanja na Lugongo yote hii umetupitishia katika bajeti hii na hakika bajeti hii itapita nikuombe Mheshimiwa Waziri mara tu baada ya kumaliza Bunge na tukapitisha finance bill hela hizi zianze kumwagika wananchi wa maeneo haya wameyasuburi maji haya kwa muda mrefu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba nimkumbushe Mheshimiwa Waziri tu kidogo mradi ambao umeishafanyiwa upembuzi wa kina wa kutoa maji Ziwa Victoria na kuleta Dodoma. Mradi huu utapita kwenye Jimbo langu na ukishafika kijiji cha Kisana pale Mheshimiwa Dkt. Mwigulu mradi ule unakuja kwa gravity mpaka Dodoma kwa hiyo, ni economical sana. Kwa hiyo, nikuombe huu mradi msiuweke kapuni, mradi huu uendelee najua kwa sababu utapiata kwenye jimbo langu hakika sisi wa Mkalama tutaogelea maji cha ajili ya mradi huu.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naupigia debe na kukumbusha kwa sababu upembuzi umeishafanyika na ni economical unatembea kwa gravity kuanzia Singida mpaka hapa hebu mradi hii uangalie ili tupate chanzo cha uhakika cha maji ambacho na hakika sasa wananchi wa Tanzania kama mama ambavyo anaendelea kututua ndoo tunakwenda kula matunda ya nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa jinsi ambavyo alihaidi kumtua mama ndoo na anaendelea kumtua mimi nimuombee tu Rais wangu maisha marefu mpaka ifike hiyo 2030 na hakika nchi hii sasa itakuwa iko katika hali ambayo inategemewa kuwa kwa jinsi ambavyo tuna neema nzuri katika nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sisi watu wa Singada na wananchi wa Tanzania tunacho muombea hicho kura zitamwagika, kwa sababu hatuna shaka ndiyo maana tunaongelea mpaka 2030 kwa sababu ndiyo mama yetu ambaye anatulea na Mungu ametubariki kupata viongozi wa namna hii ni bahati siyo wengi kama ambavyo wanapatikana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa kumalizia muda nikushukuru sana siyo kwamba sio muhimu lakini umekuwa Spika wa viwango mpenda haki, Spika ambaye tukiwa humu ndani tunajisikia tuko sawa form one, form two, na hata waliyo form three wote tunajiona tuna haki. Kwa sababu ya uongozi wako na weledi wako mzuri Mungu akubariki akutie nguvu ili tuendelee ku–enjoy katika Bunge hili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Ahsante sana.

SPIKA: Ahsante sana.

MBUNGE FULANI: Unga mkono hoja.

MHE. FRANCIS I. MTINGA: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja. (Makofi)