Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maji

Hon. Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maji

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi hii ili na mimi niweze kutoa mchango wangu katika hoja ya maji. Lakini kabla ya kutoa mchago wangu, kwa kuwa ni mara yangu ya kwanza kuchangia bajeti, naomba nitoe shukrani za pekee kwa Serikali yetu ya chama cha mapinduzi chini ya Mama yetu, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa fedha nyingi zilizoletwa katika Jimbo la Meatu kwa ajili ya kutekeleza miradi. Naomba niseme kwamba chini ya uongozi wa Mama Samia amwekwenda kuandika historia katika Jimbo la Meatu kwa miradi ambayo haikutekelezwa na haikuwahi kufikiriwa kwamba itatekelezwa.

Mheshimiwa Spika, nishukuru, tumepata mgao wa shilingi milioni 348.5 kwa ajili ya kujenga shule mpya ya msingi Mwanuzi “B” katika Jimbo la Meatu, nakushukuru Mheshimiwa Angela Kairuki. Lakini nashukuru pia jana tumepokea shilingi milioni 229 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa VETA ya Wilaya ya Meatu. Nawashukuru sana Mheshimiwa Waziri wa Elimu na Naibu wake. Vijana wanaenda kufurahi, vijana wanaenda kutimiza ndoto zao. Niwaombe tu masomo yatakayopelekwa yaendane na fursa zinazopatikana katika Wilaya ya Meatu. Nishukuru kwa mawaziri wote kwa ushirikiano wao wanaonipa mimi wakati natekeleza majukumu yangu.

Mheshimiwa Spika, sasa nijielekeze katika hoja. Niishukuru Serikali mwaka juzi tulipata fedha kwa ajili ya mradi wa dharura wa kuongeza maji katika Mji wa Mwanuzi, mradi wa kutoa maji Mwagwira, kwa kuongeza maji pale mjini Mwanuzi hali ni nzuri tunaendelea vizuri tofauti na miaka mitatu ilivyokuwa wananchi walikuwa wakitumia Bwawa la Mwanainya, kwa hiyo walikuwa wanatumia matope matupu. Lakini mradi huu kulingana na ukame unaoendelea bado baadaye utaanza kuonesha changamoto. Solution kubwa ni kupata mradi wa maji ya kutoka Ziwa Victoria. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, 2016 Ofisi ya Makamu wa Rais iliibua mradi wa maji wa kukabiliana na athari ya mabadiliko ya tabianchi chini ya Waziri January Makamba, lakini leo ni miaka saba bado mradi huo haujaweza kutekelezwa; na badala yake Serikali imekuwa ikitupiga danadana kila mwaka, na hata maana halisi ya kukabiliana na athari ya mabadiliko ya tabianchi inaondoka.

Mheshimiwa Spika, mwaka jana katika hotuba yake Mheshimiwa Waziri alisema kwamba mfadhiri yuko tayari kutoa fedha lakini, mpaka leo hakuna dalili yoyote; kwa sababu mwaka jana walisema anatafuta mkandarasi wa ujenzi lakini mpaka leo ni zaidi ya mwaka mmoja yule mkandarasi hajatafutwa. Mimi niliomba, kama mfadhiri ameshindwa basi akabidhi mradi huu Serikalini ili utekelezwe na fedha za Serikali kwa sababu Mheshimiwa Rais ameongeza fedha katika mfuko wa maji kupitia shilingi 100 ya kila lita ya mafuta.

Mheshimiwa Spika, mpaka leo hakuna dalili yoyote. Inawezekana kuna masharti magumu; naomba Waziri unapohitimisha uliweke wazi sisi wananchi tuelewe. Mwaka jana pia ulisema kwamba mradi huu katika awamu ya kwanza utatekelezwa mpaka Wilaya ya Meatu, bomba litafika, lakini nimezipata taarifa mradi huu wa awamu ya kwanza ya Meatu haitakuwemo.

Mheshimiwa Spika, mimi mwaka jana nilienda kifua mbele nikaitisha mkutano mkubwa, nikawaambia wananchi Meatu inaingia katika awamu ya kwanza. Leo hii Mheshimiwa Waziri tukimaliza bajeti twende ukawajibu wewe kwa nini mradi haufiki katika awamu ya kwanza. Wewe mwenyewe umekiri kuna hali ya ukame mkubwa katika Jimbo la Meatu lakini tumekuwa tukipata fedha za kusuasua katika bajeti. Kwa mfano, mwaka jana kati ya bilioni 3.1 jimbo la meatu limepata mradi mmoja wa makao shilingi milioni 600 sawa na asilimia mbili. Mwaka huu katika bilioni 5.7 tulikuwa tumepangiwa bilioni 1.4 sawa na asilimia 20 lakini nimepambana ndani ya wiki angalau tumepata asilimia 50 katika bajeti hii tunayoendelea kuitekeleza.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo tutawezesha kutekeleza mradi Mbushi Kata ya Burashi, Mwangudo, Mwakipopo, Mwanjoro.

Mheshimiwa Spika, nilikuwa na maombi yafuatayo kwa Mheshimiwa Waziri. Tunaomba gari jipya la maji. Jiografia ya Meatu unaijua. Lakini ninaleta kwako, ninaomba uniruhusu nilete maombi maalum kuweza ku-rescue hali ya maji katika Jimbo la Meatu.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri mwenyewe anaijua, na tumekuwa tukipata asilimia ndogo ya bajeti. Kwa hiyo naomba nilete maombi maalumu kwa ajili ya kulisaidia Jimbo la Meatu. Lakini ninaomba sasa katika eneo la Lukale Kata ya Bukundi ambako kuna Lake Eyasi eneo lile ni la chumvi maji yale yakipelekwa kwenye sample huwa hayakubaliwi kwa ajili ya matumizi ya binadamu

Mheshimiwa Spika, niombe; katika bajeti ya Serikali Kuu naomba bwawa moja kwa ajili ya Kijiji cha Muhabagimu ambacho kitasaidia Likale na vijiji vya jirani ili wananchi waondokane na adha ya maji ya chumvi ambayo hayaruhusiwi kwa matumizi ya binadamu. Lilijengwa bwawa la Mwanjoro limepasuka kabla ya kutumia, naomba likwarabatiwe na Wizara kwa sababu mkoa na wilaya hawalitambui, lilijengwa na Wizara. Naomba Wizara waje walikarabati ili liweze kusambaza maji.

Mheshimiwa Spika, kutokana na ukame katika Jimbo la Meatu nilitaka kutoa ushauri ufuatao;

Mheshimiwa Spika, tunapotekeleza miradi ya barabara, kwa kuwa Serikali ni moja, niombe kila baada ya kilomita kumi moramu ya kujenda barabara itoke kandokando ya barabara ili tuweze kuruhusu ile mifereji iingie katika yale mashimo yaliyojengwa. Maji yale yatasaidia mifugo, na kwa baadaye yataweza kusaidia kuchimba kisima kirefu baada ya muda mrefu ili tutafute solution ya kukabiliana na ukame ulipo katika Jimbo la Meatu. Kwa mfano kutoka Mwanuzi kwenda Mwabuzo tuchimbe pale Mwangikuru ambako hawana chanzo chochote cha maji.

Mheshimiwa Spika, niombe pia katika Bwawa la Mwanyaina basi awatume wataalau wake wakajaribu ku-test kama watapata maji kiweze kuchimbwa kisima kirefu kwa pembeni kusaidia upungufu wa maji. Niombe, kupitia mitambo iliyoletwa, kama alivyosema, kwamba inakuja Meatu, lakini gharama ya uendeshaji wa mitambo hii mikubwa ni asilimia 100 ni sawa na bei ya mkandarasi.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa mitambo hii ni ya Serikali halafu ni mipya kwa nini bei isiwe nusu? Badala ya kujenga visima vinne tutajenga vinane. Na kwa kuwa meneja wa visima ni nchi nzima ni pool, fedha zote zinaingia mle badala yake msisubiri mitambo ichakae muanze kununua mitambo michache michachemichache ili inapoharibika ile ya zamani iwepo mingine ya kuweza ku-replace kutokana na mfuko huu wa revolving.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru na ninaunga mkono hoja. (Makofi)