Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maji

Hon. Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maji

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana na mimi kwa kunipa nafasi nichangie kwenye bajeti hii ya Wizara ya Maji, Wizara ambayo ni muhimu sana kwa Watanzania kwa kuwa maji ni uhai.

Mheshimiwa Spika, niungane na wenzangu kwanza kutoa shukrani zangu na pongezi kwa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye kwa kweli anatufanyia Watanzania kazi nzuri sana na amedhamiria kwa dhati kabisa kuinua ubora wa maisha ya Watanzania, siyo kwenye sekta ya maji tu, lakini sekta zote. Na wewe pia Mheshimiwa Spika nakupongeza sana kwa kazi nzuri unaendesha hili Bunge kwa umahiri mkubwa. Sasa niende kwa Waziri, Waziri tunakupongeza, Waziri, Naibu Waziri na timu nzima pale Wizarani ni Pamoja na watendaji Wakuu kwenye Mkoa mnafanya kazi nzuri sana, kuhakikisha kwamba azma ya Mheshimiwa Rais ya kumtua mama ndoo kichwani inatimia; ile ndoto inatimia.

Mheshimiwa Spika, katika jitihada zenu na sisi kule Arumeru Mashariki tumeopata neema, kuna miradi mingi ambayo inaendelea. Miradi ambayo inandelea sasa hivi ina takribani bilioni 12. Mradi wa Patandi unaendelea vizuri, mradi wa Nkure umemalizika wananchi wanakunywa maji na wanaoga mara tatu sasa kwa siku. Mradi wa Imbaseni Maji ya Chai ambao una bilioni sita, pamoja na Kikatiti unaendelea vizuri. Mradi wakule Uwiro bilioni nne, uko kwenye taratibu za manunuzi na taratibu zinaendelea vizuri. Kwa kweli nakupongeza na nakushukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa kazi nzuri.

Mheshimiwa Spika, pamoja na pongezi hizo niweke angalizo, tumeshuhudia changamoto za mabadiliko ya tabianchi, wakati ukame ulipotokea maji yalikosekana kabisa kule Meru. Hata Mheshimiwa Waziri wa Habari alikuwa pale Kili Golf alishangaa kuona kwamba, hakuna maji Meru na mlima uko jirani pale unatoa maji mengi.

Mheshimiwa Spika, ushauri wangu ni kwamba, kwa kuwa maji yale yanakwenda kwa gravity, kuwe na matenki makubwa kwenye vyanzo vya kuhifadhi yale maji yasipotee hovyo, lakini pia matanki ya ku-reserve yawe mengi kwenye main line kwa ajili ya kuhakikisha kwamba, pressure inakuwa sawasawa mpaka kule mwisho kwenye vijiji vya mwisho. Mheshimiwa Waziri, kipekee kabisa nikushukuru, tarehe 27 Februari, 2022 alikuja Arumeru Mashariki, tukafanya kikao pale kwa DC, nikampelekea kilio cha Korongo la Mpeduwima ambalo lilikuwa limepotea kwamba, linahitaji kufukuliwa.

Mheshimiwa Spika, Waziri hakuchelewa akatuma wataalam wa Bonde la Mto Pangani tukaenda kufanya survey na badaye ile kazi ilifanyika na alikuja kuzindua. Kwa kweli, lile korongo sasa hivi limerudi kwenye hali yake. Takribani kilometa 18 lile korongo linaonekana, mvua za mwaka huu hazijaleta matatizo. Namshukuru sana ndugu yangu Waziri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kawaida ukishasafiri safari ya kwanza inaita safari ya pili. Baada ya yale maji sasa kwamba, yamepelekwa kule mwisho, yamekwenda kuishia Kata ya Majengo, sasa Kata ya Majengo ndio inateseka, maji yanakwenda kutuama kule yanawanyima wananchi kuishi kwa furaha na amani. Nimwombe Waziri sasa aweke kwenye mipango yake, tuje tujenge bwawa pale Kata ya Majengo yale maji yakusanywe pale yaunganike na mifereji ambayo itajengwa kwa kuanzia kule Kimweli Malula kwa ajili ya kuvuna maji ya mvua na mafuriko ambayo yanatokea. Hata juzi kuna mafuriko yalitokea mpaka yakasomba gari. Yale maji yakusanywe yapelekwe kwenye bwawa ambalo litajengwa pale Majengo, hayo maji yatumike kwa ajili ya mifugo na kwa ajili ya irrigation. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa nafasi hii. Nilikuwa nataka kuongeza lingine, lakini kwa haya machache, kwa leo nasema ahsante, naunga mkono hoja. (Makofi)