Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara

Hon. Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Spika, natambua kazi kubwa inayofanywa na Wizara katika maeneo mbalimbali ya uwekezaji, lakini naomba kushauri yafuatayo: -

Kwanza baadhi ya maeneo yanazungukwa na rasilimali nyingi lakini kwa sababu ya kukosa mkakati wa kuzitumia bado jamii inayozunguka ni masikini. Kwa mfano Visiwa vya Ukerewe; uzalishaji wa samaki ni mkubwa lakini hakuna kiwanda cha kusindika hali inayopelekea mazao hayo kutokuwa na tija. Pia Ukerewe ndio wazalishaji wakubwa wa machungwa katika eneo lote la Uganda wa Ziwa, lakini sehemu kubwa huharibika na kutoisaidia jamii.

Mheshimiwa Spika, ombi na ushauri wangu kwa Wizara isaidie kushawishi uwekezaji wa viwanda vya kusindika samaki na matunda Wilayani Ukerewe ili kusaidia uchumi wa eneo hilo na Taifa kwa ujumla.