Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara

Hon. Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Spika, naungana na Watanzania wenzangu wote kumshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kutujalia baraka zake katika nyanja mbalimbali za ustawi wa amani, kijamii, kiuchumi, kisiasa, kiplomasia na mambo mengi katika Taifa letu.

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Mbulu Mjini nachukua nafasi ya kumpongeza sana Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, viongozi/watendaji wetu wote Serikalini kwa utekelezaji wa Ilani ya CCM 2020-2025, kwa kweli kazi nyingi zimefanyika katika jimbo langu la Mbulu Mjini kwa kila sekta, hasa yale mambo mengi ambayo yaliyoshindikana muda mrefu.

Mheshimiwa Spika, sasa naomba kutoa mchango wangu kupitia mapendekezo ya bajeti ya Wizara hii ya uwekezaji, viwanda na biashara. Nampongeza sana Mheshimiwa Waziri na watendaji wake wote Wizarani na wadau wengine.

Mheshimiwa Spika, mimi mchango wangu ni kwamba tuangalie utaratibu wa kuhakikisha maafisa wetu wa biashara ngazi za halmashauri, mikoa tuwajengee uwezo wa kuwalea na kuwajengea uwezo wawekezaji wadogo.

Mheshimiwa Spika, nasema hayo kwa sababu TAMISEMI ilipoagiza kila halmashauri nchini kuwa na viwanda 100 vingi viliyoanzishwa vilitoa ajira kwa vijana wengi, lakini hadi sasa ni vichache vinavyoendelea kufanya kazi na changamoto kubwa ni ukosefu wa wataalam washauri, mitaji ya kutosha na mazingira ya ukosefu walezi. Hivyo kuna haja kubwa kulinda na kuimarisha viwanda vidogo na vya kati kwa kuwa kundi kubwa la wananchi wataajirika kwa ajira ya muda na mikataba na wawekezaji wa viwanda vidogo watakuja kuwa wawekezaji wa ndani ambao mapato yao yataendeleza uchumi wa Taifa letu na mafanikio ya wawekezaji hawa wadogo watajenga miundombinu hapa hapa nchini.

Mheshimiwa Spika, naunga hoja mkono kwa asilimia mia moja na naomba kuwasilisha.