Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, Serikali iokoe viwanda vya mkonge, okoeni ajira.

Mheshimiwa Spika, nawapongeza Wizara kwa wasilisho la bajeti na ninaomba kuchangia kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza tuokoe zao la mkonge na viwanda vyake. Katika Ilani yetu ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020 - 2025 imetaja kuzalisha ajira milioni nane, ni wazi kuwa ajira hizi kwa kiasi kikubwa zitatokana na mnyororo wa thamani kuanzia katika malighafi za kutoka mashambani/kilimo hadi viwandani (agro-processing industry). Ajira hizi pamoja na viwandani itaendelea hadi sokoni.

Mheshimiwa Spika, ni masikitiko makubwa sana kwamba wakati tumeamua kufanya zao la mkonge kuwa zao la kimkakati, hakuna jitihada za makusudi za kulinda viwanda vya kuchakata zao la mkonge kwa maana ya kulinda soko. Ndani ya Serikali hakuna ufuatiliaji wa maagizo na maelekezo ya Waziri Mkuu Septemba, 2021 na rejea yake Novemba, 2021 kwamba Wizara inayohusika na Mazingira kwa maana ya Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira izuie importation ya kamba za plastic ambazo kwa kiasi kikubwa mbali ya kuvuruga soko la kamba za kitani, lakini pia zinaathiri mazingira.

Mheshimiwa Spika, kwa sababu hiyo, ni matarajio yangu wenzetu wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara wanayo nafasi kubwa ya kushirikiana na Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira kuhakikisha kuwa zuio hilo linasimamiwa ili kuwalinda wakulima na kulinda viwanda na ajira za Watanzania kama sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM.

Mheshimiwa Spika, industrial park Mafinga Mjini; tumetenga ekari 750 kwa ajili ya industrial park na kupitia Mradi wa TACTIC tutajenga miundombinu wezeshi na tayari EPZA walitembelea eneo hilo na kutoa ushauri, pamoja na kuwa tuko katika hatua za awali za kupanga, kupima na kumilikisha, nawaomba Wizara tufanye kazi kwa ushirikiano ili tuweze kufanikisha suala hili kwa lengo like lile la kuzalisha ajira hasa kupitia fursa ya mazao ya misitu.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.