Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara

Hon. Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi namimi niweze kuchangia Wizara hii ya Viwanda na Biashara.

Kwanza Mheshimiwa Waziri ukija kuhitimisha hoja yako sisi wananchi wa Mkoa wa Mara tunahitaji utujibu kuhusiana na viwanda vyetu vilivyokufa pale Musoma. Kiwanda cha nguo, kiwanda cha kusindika samaki na kiwanda cha maziwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, viwanda hivi vilikuwa vina mchango mkubwa sana katika kutengeneza ajira katika Mkoa wa Mara. Mheshimiwa Waziri kuna kipindi mlihamasisha sana wananchi watenge maeneo kwa ajili ya ukanda wa uwekezaji. Eneo moja wapo watu walilolitenga na wakalipwa fidia ingawa wengine wakadhulumiwa ni Wilaya ya Bunda. Ni zaidi ya miaka 10 sasa hivi hakuna hata kiwanda kilichowekezwa. Ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha maeneo yale yaliyotengwa kwa ajili ya uwekezaji yanawekezwa ili wananchi wa pale waweze kupata faida, iweze kutengenzwa ajira kutokana na malighafi zinazopatikana maeneo husika? Ni muda mrefu sana tunahitaji majibu ya Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, na mimi ningependa Mheshimiwa Waziri ukija hapa uje utueleweshe sisi Wabunge kuhusiana na hii issue ya Twiga Cement, Tanga Cement; yaani bado hatujaielewa sana. Tunaomba ukija uchukue muda mwingi sana kulielezea hili jambo ili sintofahamu ziondoke. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nilikuwa najaribu kuuliza katika hili jambo, kwamba maslahi ya taifa yakoje, nimejiuliza sana. Sasa, kuna Tanga Cement anataka kuuza sehemu ya share kwa sababu kashindwa kuendesha, kwa sababu ameshindwa kulipa kodi kwa zaidi ya miaka saba. Si kwa kupenda yeye bali ni kwa sababu hawezi tena kujiendesha. Kuna athari ya zaidi ya wanfanyakazi 3,000 kupoteza ajira hapo. Sasa yeye pamoja na wabia wenzie, maana hili la kwao, wamehamia kuuza sehemu ya share kwa Twiga ambaye yeye anataka ku-invest dola milioni 400 sawa na shilingi bilioni 930. Yeye ndiyo ameona huyu sasa anataka kutupa hizi fedha. Wamekubaliana wao, sasa sijui kizungumkuti kiko wapi.

Mheshimiwa Spika, sasa kama kuna mwingine alikuwa na fedha nyingi tulitarajia angewafuata Tanga Cement wakubaliane, kwa sababu hapa ni biashara huru. Wao wenyewe wana mamlaka ya kuchagua waende kwa nani, kwa namna gani wao wanaweza kuokoa eneo hili. Kwa hiyo tunahitaji tupewe maelezo ya kina lakini huyu ambaye anataka ku-invest hapa ni mlipakodi mzuri. Mwaka jana amelipa zaidi ya shilingi bilioni 80 lakini hapa Tanga Cement wamepata hasara zaidi ya shilingi bilioni 46, hawawezi kujiendesha, kizungumkuti kiko wapi hapa?

Mheshimiwa Spika, nilikuwa nafanya uchunguzi wangu na nikapata taarifa; nimesoma Gazeti la Jamhuri la uchunguzi la tarehe 24 mwezi wa nne. Limesema, kwa sababu kulikuwa kuna hoja, ooh! huyu akimilikishwa kuna suala la ku-dominate soko. Sasa nikaambiwa Tume yenyewe ya Haki ya Ushindani ilifanya kikao na hawa wazalishaji 12 wa saruji, na wakasema kwamba sisi hatuna nongwa, hakuna suala hapa kwamba hawa wata- dominate soko kwa sababu mazingira ya sasa hivi yamebadilika, wapo watu ambao wana uwezo wa kuzalisha zaidi ya tani 1,000,000 ya cement.

Mheshimiwa Spika, hata kama sasa hivi Twiga anaongoza, Dangote akiamua kufungulia mitambo yake naye anaweza akaongoza vile vile. Huyu mwingine naye akiamua kuongeza uzalishaji naye anaweza akampita Dangote anaweza akampita Twiga, suala la dominant hapa liko wapi? Tunaomba utuelezee. Na nikaambiwa kati ya hao wazalishaji 12 kuna wengine hawakwenda. Hawakwenda kumbe kwa sababu hawazalishi. Sasa tunahitaji tupewe maelezo ya kina hapa tujue interest ya taifa iko wapi hapa? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lazima tupewe maelezo ya kutosha; na mimi sitaki kuwa na upande na hizo siyo tabia zangu. Tunataka kujua interest ya taifa iko wapi? Mnufaika ni nani? Yaani kama wenyewe wazalishaji wamesema hakuna nongwa, tatizo linakuwa wapi?

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo Mheshimiwa Waziri uje utuambie hapa tupate maelezo ya kina ili sintofahamu ziondoke. Maana hapa isije ikawa tunaingizwa kucheza ngoma ambazo hazituhusu, na hizi ngoma inawezekana ziemanzia kwenye Wizara yako huko huko kuna, makundi kwa sababu kuna interest za watu. Tunahitaji majibu sahihi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri ukija hapa hebu tueleze hili suala la ukomo wa asilimia 35 limekaaje. Hivi, kama mtu aliomba kwenye mazingira hayo ya kipindi hicho akakataliwa, hivi ni alpha na omega? Hana room ya kuomba tena? Waliokataa hawana room ya kukubali kwamba sasa hivi mazingira ya uwekezaji yamebadilika? Ikoje hii?

Mheshimiwa Spika, lakini Mheshimiwa Waziri tunaposema tunavutia wawekezaji kuna wawekezaji ambao wameshaanza ku-invest. Tunajua mitaji yao, tunajua uwezo wao, tumewaona; hawa wanatakiwa walindwe. Nilikuwa nakumbuka kulikuwa kuna sarakasi moja hapa ya issue ya Dangote akataka kuondoka, kwa taarifa nilizonazo Serikali ikabidi mwende kumbembeleza ili abaki. Tunazungumzia hapa Liganga na Mchuchuma kuna muwekezaji amekaa pale muda mrefu, leo Serikali inabidi muende mkawalipe fidia ili muanze uzalishaji kwa sababu alikuwa hana capacity hiyo.

Mheshimiwa Spika, tunataka tuendeleze uwekezaji wa briefcase? Kama tutakuwa wakweli na tunaipenda nchi hii nyekundu iwe nyekundu, njano iwe njano, uweke historia. Mara mia uhukumiwe kwa kusema ukweli lakini siyo uhukumiwe kwa kupindisha mambo.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru. (Makofi)