Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara

Hon. Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi hii ili na mimi niweze kuchangia hotuba ya Bajeti ya Viwanda na Biashara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mabula amenipa hapa Biblia zote mbili ya Agano la Kale na Agano Jipya; yote nitayatumia kwa nafasi yake. Agano la Kale Wizara ya Kilimo ndio wazalishaji wa mazao yote. Nimetoka Iringa nimeona alizeti nyingi, nimekuwa hapa Dodoma nimeona alizeti nyingi, nimekuwa Singida nimeona alizeti nyingi, Kigoma alizeti nyingi; inaonekana mikoa zaidi ya 20 sasa inalima alizeti. Kwa hiyo kwa sababu uzalishaji upo upande wa Wizara ya Kilimo ambalo ni Agano la Kale, jipya ni Wizara ya Viwanda na Biashara. Hapa ndipo tunataka tuzungumze vizuri. Unapotaka kulinda viwanda lazima udhibiti mianya yote ya magendo na u-fix kodi ambayo itasababisha bidhaa yote ya nje isinunuliwe ili kulinda viwanda vyako.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa nataka kuzungumza nini. Mikoa ambayo inalima alizeti, wakulima wamekopa benki, TADB imewapa fedha. Wasipouza mbegu yao kwa bei nzuri, TADB inafilisika, NMB inafilisika, CRDB inafilisika na mwananchi anafilisika. Viwanda wamekopa kwenye mabenki, wasipozalisha; kwa sababu taarifa wa Mheshimiwa Waziri imesema asilimia 25 ndivyo viwanda hivi vinazalisha maana yake miezi minne kwa mwaka, viwanda hivi vinakwenda tena kufilisika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo tukiwa kama nchi tunafilisi viwanda kwa sababu ya kuachia room ya watu kuingiza bidhaa zao kutoka nje, hatuwasaidii Watanzania. Kwa hiyo Agano Jipya linapaswa litimilize Agano la Kale, kwamba wanazalisha lakini Agano Jipya linahakikisha kwamba watu wanauza. Kwa hiyo mwaka jana tuliweka kodi equity duty kwa sababu ya kuogopa mfumuko wa bei; sasa tumekwenda kuwauwa wakulima wetu. Bahati nzuri Mheshimiwa Waziri wa Viwanda na Biashara huko kwako ndiko wanakolima alizeti, kwa hiyo tunakwenda kuwafilisi wapigakura wako, lakini tunakwenda kuwafilisi wapigakura wa Mwigulu, hapo Singida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeona Mkalama wanalima alizeti nyingi. Kwa hiyo niombe hivi, mwaka huu tusiruhusu tukaondoa kodi ya mafuta ya nje, tukiruhusu tunakwenda kufilisi viwanda vyetu na wakulima wetu. Leo mkulima wa alizeti anauza shilingi 600 kwa kilo ambayo alikuwa anauza shilingi 900 mpaka 1000, hiyo huwezi kumlinda mkulima. Lakini mwenye mafuta anakwenda kuuza dumu 60,000 badala ya 70,000, maana yake huwezi kulinda viwanda. Kwa hiyo hatuwezi kulinda viwanda kama tunaruhusu magendo, tunaruhusu kuondoa kodi kwenye kwenye mafuta ya nje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo niombe sana na huu ndio ugonjwa ambao umeua viwanda vingi duniani. Hatuwezi kuendelea kukubaliana na jambo hili, lazima sasa Serikali ione namna ya kuweka kodi kwenye mafuta yanayotoka nje, kwa sababu mikoa yote 20 hii inalima alizeti. Na kwa hali hiyo ukiangalia Iramba na Singida yote, ukiangalia Dodoma hii wananchi maisha yao wamebadilisha kulingana na alizeti ambayo wanakamua ndani wanauza barabarani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo niombe sana, ili nchi iendelee lazima tuwe na wivu wa kuwaonea wivu wakulima wetu waendelee kuzalisha kuliko kuruhusu mataifa nje kuingiza mafuta. Niombe sana hili kwa mwaka huu Wabunge tusikubali kuondoa kodi kwenye mafuta ya nje, tutakuwa tunaua viwanda vyetu. Hili ni simu, ni kama vile Biblia inavyosema, kwamba asiyempenda wa nyumbani kwake ni mbaya kuliko asiyeamini. Kwa sababu sisi tunawapenda wa nje tunashindwa kuwapenda wa kwetu, tunaruhusu kuondoa kodi ili watu waingize mafuta wa kwetu wanabaki maskini, hapana. hii ni Hapana, lazima tukubaliane Waheshimiwa Wabunge. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimemsikiliza vizuri Mheshimiwa Waziri wa Viwanda na Biashara, lakini nimemsikiliza vizuri mchangiaji King, na mimi nilikuwa najiuliza, mikoa 17 inayolima pamba leo pamba yote tunaiuza nje; ni umaskini mtupu. Haiwezekani tukazalisha, tukaendelea kuuza raw material badala ya kuuza production iliyokamilika. Na hili nakwenda kuandika historia kwamba Rais mwananke ameamua kuhakikisha kwamba maghala yanatengenezwa hapa; na hii ni lazima Serikali i-set fedha kama ambavyo imependekeza. Hatuwezi kukubali kila mwaka kurudi pale pale. Nchi hii tuna miaka 60 ya uhuru hatuwezi kuwa tunauza raw material tunashindwa ku-produce material yetu hapa ndani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, na hili linakwenda kuweka rekodi, Waziri wa Viwanda na Biashara mwanamke wewe, na hili linakwenda kuweka rekodi, Spika wa Bunge mwanamke, Tulia huyu hapa. Kwa hiyo haya mambo hayatokei hivi hivi. Kwa hiyo niwapongeze sana Mheshimiwa Waziri, nimpongeze sana Mheshimiwa Rais kwa uamuzi mzuri ambao sasa anakwenda kuuchukua kwa ajili ya pamba. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, unajua tukizalisha majora hapa, kwanza tukijenga tu kiwanda hiki ni zaidi ya bilioni 500, mfanyabiashara wa kawaida hawezi kupata fedha hizi. Hata ukienda kwenye benki wanakuona kama umechanganyikiwa hivi kwa sababu mitaji ile ni midogo na wanaogopa risk kuwekeza kwa mtu mmoja. Kwa hiyo Serikali lazima i-set fedha kwa sababu kama tunajenga madaraja, tunashindwaje kujenga kiwanda? Kwa hiyo hili ni jambo zuri. Na tukiweza hiki kiwanda, kwamba bidhaa ya pamba ina vitu vingi ambavyo Mheshimiwa Lucy alikuwa anazungumza hapa; kama vile vifaa vya hospitali na vifaa tiba, vinatokana na mabaki ya pamba inayotoka kwenye majora. Kwa hiyo tunakwenda ku-save hela nyingi ya kuagiza pamba nje; dola ya kigeni itakuja badala ya kuipeleka nje (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini, kama watu watakuja hapa Afrika kununua, Afrika tukawa tunauza majora, hapa Tanzania, akija hapa Mkongo analala hoteli, anapanda taxi, anakunywa soda, anakunywa bia anapata na kamchepuko kidogo mambo yanaendelea. Kwa hiyo kuna vitu vingi ambavyo tutavifikia kuliko sasa. kwa hiyo mimi niombe Serikali iangalie wigo mpana, isiangalie tu kwamba tunakwenda kuzuia fedha za nje, tunazuia fedha kwenda nje, tunataka fedha za kigeni ziingie ndani ili zisaidie ukuaji wa kiuchumi hapa Tanzania. Na ndipo tutawafanya wakulima walime wakiwa na uhakika bei wa soko zuri la pamba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo soko la dunia hatuna uwezo nalo. Mwaka jana tumeuza pamba 1,560 mpaka 2,000 mwaka huu uki-google wewe unapata senti 0.71. Ukiondoa gharama zingine unapata senti 75. Kwa hiyo maana yake pamba inakwenda kununua kwa 1,060. Kwa hiyo tukiwekeza hiki kiwanda ndio mwarobaini na ndipo kukuza uchumi wa nchi hii. Halafu nikuombe; kwa sababu pamba inalimwa sana, mikoa 17, na tayari pale katikati Simiyu na Magu kuna eneo lipo basi muangalie namna ya kuleta maeneo hayo ili kuongeza uzalishaji wa zao la pamba. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuendelee kufanya research viwanda, vyetu hivi; kwa mfano viwanda vya miwa ambavyo vinatoa sukari, ni viwanda ambavyo wawekezaji wake wamejitahidi sana, na kwa kweli hata uzalishaji unaendelea. Nilipata kutembelea kiwanda cha Kagera sugar nikakuta wana mitambo matata ya kimarekani ambayo sijawahi kuona. Wanafyeka mapori kuongeza uzalishaji na bado wanahitaji. Sasa, yaandaliwe maeneo ambayo hayalimwi, yamebaki waongezewe kule Kagera Sugar ili waweze kulima na kuzalisha vizuri zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuendelee kuwashauri pia wafanye research nzuri. unajua kwenye miwa si tu unaweza kutoa sukari na molasses pekee, Hapana; kwenye miwa unaweza uka-produce mpaka diesel, ipo kwenye miwa, kama tuta-set vizuri viwanda. Kwa hiyo lazima Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara ifanye research ya kwamba zao hili linaweza ku-produce vitu gani ndani; huko ndiko kukuza mnyororo wa thamani. Hata ukienda kwenye mkonge, mkonge sio umera pekee, lile zao la katikati ninyi watu wa Tanga lile likisindikwa linapandwa ndani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo tunataka mfanye research kwa sababu tatizo tuna akili nyingi lakini maarifa hatuna, sasa hilo ndilo tatizo. Sasa tutumie maarifa kufanya research ili kuhakikisha kwamba tunakwenda kwenye viwanda ambavyo ni vya kisasa zaidi na ambavyo vinaweza kutoa vitu vingi kwenye mmea mmoja. Hili ndilo itakuwa ni suluhisho, kwa sababu hata ukienda Brazil kiwanda cha sukari kikikamua sukari kinatoa bidhaa nyingi mpaka kwenye mafuta lakini sisi bado tunabaki kwenye sukari, molasses na makapi mengine, tuondoke huko. Serikali iwasaidie wawekezaji wa sukari kufikia hatua hiyo ya uwekezaji wa kisasa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naunga mkono hoja.