Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara

Hon. Ahmed Mabukhut Shabiby

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Gairo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara

MHE. AHMED M. SHABIBY: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii. Nimekuwa mmoja wa wachangiaji lakini kwenye mchango wangu sitokita sana kunukuu maprofesa au watu wengine. Nitakwenda sana kuongea kwenye lugha nyepesi ambayo watanzania au Wabunge wenzangu wataielewa. Leo michango yangu ni miwili tu. Mchango wa kujiunga kwa viwanda hivyo viwili pamoja na kiwanda cha pale kibaha cha kuunganisha magari.

Mheshimiwa Spika, kwanza nitaanza na kile kiwanda cha kuunganisha magari FAO pale Kibaha. Nataka niwape maangalizo Mawaziri wetu na hasa Waziri wa Viwanda kwa sababu wewe ndio mhusika wa viwanda, lakini vilevile na Waziri wa Fedha kwa sababu katika nchi hii tunakusanya kodi mpaka kwa watu wa chini ndio maana kuna tozo kuna nini kuna nini kwa sababu hatuna mapato kwenye hii nchi ili tuajiri wafanyakazi tufanye nini yani lazima tupate mapato. Lakini unavyoona kuna kitu kinaanzishwa hakina msingi wa aina yoyote halafu tena kuna kodi inatolewa pale bila manufaa yoyote.

Mheshimiwa Spika, kwa mfano kile kiwanda cha kuunganisha magari cha assembly pale Kibaha. Kile sio kiwanda cha assembly kile kiwanda cha kuchukua gari ambalo limefunguliwa kutoka China pale wanakuja kuliunganisha yaani sawasawa na gari lako unalichukua hapa Dodoma unalifungua fungua unaliweka kwenye boksi halafu unalipeleka Dar es Salaam unalichukua engine unalibandika unachukua cabin unabandika mnasema assembly, hiyo sio assembly. Halafu baada ya hapo unamwambia kwamba yule atakaye mwenye magari mengine akileta kutoka China analipa VAT ila lile linaloungwa ungwa pale halipi VAT kwa hiyo, ni kuikosesha Serikali mapato bila sababu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, maana ya assembly za Mwalimu Nyerere mpaka zimekuja kwa kina Mwinyi mpaka wakina Mkapa maana yake ni nini? Maana ya assembly gari inatengenezwa Tanzania kwa 21% ni malighafi kutoka Tanzania kwa mfano, wakati ule TAMCO imeanzishwa ilikuwa inaunganisha magari ya Scania.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, wale Afro Cooling kiwanda cha Tanzania nacho kimeajiri wafanyakazi wengi, kilikuwa kinatoa rejetor zote made in Tanzania. AFRI cable walikuwa wanatoa wire zote zinaunganishwa wire za Tanzania Yuasa zilikuwa betri za Tanzania. Kiwanda cha Tanzania mali yake inaunganisha pale, Tasia walikuwa wanatengeneza spring ndio wanaenda spring za Tanzania zinatumika, Mangula walikuwa wantengeneza letras zote zinakwenda pale zinatumika. Hawa Coast sterio walikuwa wanatengeneza ngazi na vitu vingine kwa hiyo ukiangalia 21%. General Tyle walikuwa wanatengeneza matairi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ukichukua maana ya kuongeza ajira kwa ajili ya assembly unaunganisha na hivyo viwanda vyote. Leo kwenye magari haya hakuna mali yoyote ya Tanzania inayohusika pale. Halafu mnasema tunaongeza ajira Tanzania, wale wafanyakazi wako 100 tu pale, ajira ipi? lakini ukosefu tunayokosa kwenye VAT mabilioni ya pesa. Hii utapeli wa aina huu haiwezekani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, maana yake na sisi wafanyabiashara wa mabasi tunataka na sisi, maana yake basi moja ushuru peke yake ukiuliza Tanzania ni 100,000,000 wakati lori ni 30,000,000 sasa wa mabsi nae akija kwa hiyo Serikali mtakusanya wapi pesa? Tuachane na hii Habari ya viwanda vya utapeli tapeli huu na Mheshimiwa nilishaongea nae hata kwa mdomo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kingine ni hiki kiwanda cha nilikuwa sitaki kuongea lakini nimeona ndugu yangu Mnzava amenitaja pale na mimi acha niseme. Hiki kiwanda kuungana kiwanda cha Twiga Cement na Tanga Cement sioni shida, hivi shida iko wapi? Mwenye mali mwenyewe wa Tanga cement ana 68.8% hawa mashirika yetu haya ya Mifuko ya Jamiii yana hisa 32.2% anayetaka kujitoa ni yule mwenye 68% anataka kuuza share yake mtu anataka kuuza share yake tatizo liko wapi? Hakuna shida, ukisema hivyo kwamba huyu mtaleta competition kuna viwanda 11 nchi hii na cha Tanga sasa hivi ni cha nne kwa uzalishaji wala sio cha pili kama mnavyosema, kuna viwanda 11 vya cement. Hivyo TBL ameshika soko la nchi hii asilimia ngapi? Yapombe, si Kashika Zaidi ya 90%, ukija Bakhresa asilimia ngapi za unga? Zaidi ya asilimia 80%, ukija Mtibwa Sugar, Mtibwa Sugar ndio mwenye kiwanda cha Kagera Sugar sio mtu mmoja? Kwa hiyo kama…

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Mheshimiwa Shabiby kuna taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Mnzava.

TAARIFA

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, naomba nimpe taarifa mzungumzaji sekta ya saruji ni moja kati ya non regulated sectors kwenye nchi yetu, na kwa sababu hiyo kanuni za ushindani kusimamiwa ni jambo muhimu kuliko kitu kingine chochote kile, nakushukuru. (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Shabiby unaipokea taarifa hiyo?

MHE. AHMED M. SHABIBY: Mheshimiwa Spika, naipokea kwa mikono miwili. Isipokuwa ninachozungumzia tusiwe tuna hiyo mambo kama hayo, tunachotakiwa sisi kuangalia je, Tanga Cement ana clinker nyingi Zaidi ya kuvuna miaka 100 pale kwake? Twiga cement hana clinker nyingi. Kinachotakiwa ni kusimamia kwamba hiki kiwanda kitafanya kazi? Wafanyakazi wale hawatakosa ajira? Sasa ni kazi ya Serikali muwe na mikataba ya aina ile, kiwanda kifanye kazi na wasije Twiga wakanunua wakachukua ile clinker wakaihamisha. Hicho ndio cha msingi lakini cha msingi kusema FCC, f ni nini sasa imekuja kwenye hii cement, nataka niiulize hii Serikali kwamba haina mpango maalumu wa kupanga bei?

Mheshimiwa Spika, Lazima uwe na wataalamu, waangalie je uzalishaji wa Tanzania una cost bei gani? Niwapeni mfano nchi kama Oman au Kenya tu, nchi mbili tu, cement ya aina yoyote inayozalishwa kuna wataalamu wetu tuna Maprofesa tuna manini huko Vyuo Vikuu wako wasomi wataalamu wanaangalia ina-cost bei gani? wakiweka na kodi bei gani? Wanaweka na bei ya kuuza ni hii hasa kama hii nchi kila mtu akizalisha kitu anauza anavyotaka basi itakuwa ni balaa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tusiogope kwa hilo tusiseme eti mtu kwamba mimi hapa nina mali yangu nataka kuuza eti unaniambia eti peleka kwenye mashindano, mashindano yapi hayo? Kitu changu haya, kwa mfano nimeamua kuhujumu? Sipeleki lakini taarifa ya uzalishaji umepumzika. (Kicheko)

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Mheshimiwa Shabiby kuna taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Getere.

TAARIFA

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, nataka kumpa mzungumzaji mzuri tu, Mheshimiwa Shabiby rafiki yangu mkubwa kwamba kiwanda cha Tanga Cement ni moja ya viwanda vinavyothaminiwa katika Uhuru wa Tanzania na kiwanda kilichobinafsishwa mwaka 1966 ni kiwanda cha wananchi na ni kiwanda cha Serikali kwa masharti ya kubinafsisha sio cha mtu binafsi.

SPIKA: Mheshimiwa Shabiby, unaipokea taarifa hiyo?

MHE. AHMED M. SHABIBY: Mheshimiwa Spika, taarifa naiopokea lakini naona haelewi. (Kicheko)

Mheshimiwa Spika kwa sababu kama mnataka hivyo nyumba za Serikali zote zilikuwa nyumba za Uhuru ziko hapa? si zimeuzwa? Viwanda vyote vya Nyerere vilikuwepo hapa, si vimeuzwa? Sasa mkitaka, zimeuzwa nyumba mpaka kwenye makao ya Polisi, utakuta nyumba ya Polisi ipo kwenye eneo la Polisi kauziwa RPC sasa mkitaka namna hiyo hiyo msizungumze vitu hivi. Sisi twende tuzungumze kile kitu cha kweli, hizi ni biashara tunazungumzia mambo ya biashara hatuzungumzi Habari ya sijui ilikuwa hivo ilikuwa hivo, tuzungumzie biashara. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, nawasihi ndugu zangu tusijiingize huko kwenye mambo ambayo hatuyajui tuwachie wawekezaji wawe huru sisi tuwabane tuweke vitu vya regulation kwa ajili ya kuwabana kwenye bei na vitu vingine, ahsante sana.