Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara

Hon. Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara

MHE. CHARLES J. P. MWIJAGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipatia fursa ya kuchangia Bajeti ya Wizara hii ambayo naipenda sana na ninaifahamu. Nina mambo machache ya kuzungumzia.

Mheshimiwa Spika, kabla sijaenda niunge mkono hoja ya Bajeti hii. Takataaje kuiunga mkono? Watu wa Mtelakuza hawatanielewa, na nimemwona Profesa wangu hapo, Profesa Winnie-Esther hatanielewa, kwa sababu hii ndiyo dissertation yangu ya Ph.D iko hapa. Jambo la kwanza, nimekuwa nikizungumza kwamba shughuli zote za kiuzalishaji zitueleze mauzo ya nje. Nampongeza Waziri, ameonesha kwamba Dola bilioni 8.52 anauza nje, na kwa gazeti la Citizens na tarehe 20 Aprili, limeandika, Tanzania tunauza nje shilingi bilioni 12.383. Hiyo tumekubaliana.

Mheshimiwa Spika, nizungumze kidogo kuhusu blueprint. Blueprint imefanikiwa, na mafanikio ya kwanza yalitokana na pale sisi wenyewe tulipokubali kujitathmini. Blueprint tuliiandika sisi wenyewe na ninapenda kusema, architect mkubwa alikuwa Mheshimiwa Profesa Adolf Mkenda. Niwape changamoto nyingine, na hii siyo Wizara tu, ni Serikali, ni wadau wote, ni wananchi wote, tuendelee kujitathmini na kuboresha mazingira ya ufanyaji biashara kwa sababu ina tija kubwa.

Mheshimiwa Spika, namba tatu, kulinda tasnia au kulinda viwanda. Nimemsikia Mbunge wa Tanga anazungumzia viwanda kufa. Kufa kwa viwanda mimi nakujua vizuri sana. Vingine nilijitahidi kuvifufua, aah, nikashindwa.

Mheshimiwa Spika, nitachambua ulinzi wa viwanda na Profesa Winnie-Esther yuko hapo, ananisikia, kwenye marks zangu utaniongezea, nitatumia ngeli Michaek Porter, Profesa wa Harvard Business University kuchambua ni kutumia industry strategy kuwaonesha namna ya kulinda viwanda vya nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ukiacha viwanda kuna kitu kinaitwa tasnia nitawapa mfano rahisi, chukulia viwanda vya magurudumu ya magari, kama Michelin, Bridge Stone, Ring Long, Fire Stone na Safari, assume viwanda hivyo vingekuwa hapa nchini, unapoangalia industry strategy, unaangalia kitu cha kwanza, unaingiaje kwenye ile industry structure? Unaangalia ile barrier of entry na barrier of exit, lakini unajiuliza, unakwenda kumkuta nani mle ndani? The competitions, the players, lakini unaangalia nani mteja wako (the consumer)? Unaangalia nani supplier wako mle? Unajiuliza, ushindani ukoje? Ni ushindani wa kirafiki au wa kihasama? Au wa kukatana vimeo?

Mheshimiwa Spika, unapokuwa unaangalia mambo hayo kuna watu wana maslahi. Mojawapo ya watu wenye maslahi ni Watanzania kwa kesi ya viwanda hivi nilivyovitaja ambavyo siyo vya ukweli, kwa sababu hatuna viwanda vya magurudumu. Mojawapo, kwanini tunajenga viwanda? Tunajenga viwanda: -

(i) Kutengeneza ajira;

(ii) Kutengeneza bidhaa za kutumia na bidhaa za kuuza nje na yote yanakwenda pamoja. Naipongeza Wizara, inauza nje na inaonekana.

(iii) Kuchangamsha uchumi. Pale penye viwanda, uchumi unachangamka, na ndiyo maana nasikia kilio cha Tanga; na

(iv) Kukusanya mapato ya Serikali kwa ajili ya maendeleo.

Mheshimiwa Spika, unapokuwa unaangalia ES structure ya Michael Porter wakiwemo wadau watano au sita katika ile structure, angalia wanavyofanya kazi. Ndiyo maana unakuta yanaundwa makundi ya watu kutetea wateja wale watano, wale waendeshaji wa shughuli wanaweza kulumbana au wakaungana pamoja wakamuumiza supplier. Unaleta malighafi, wanakupa bei ndogo. Au wakaungana, wakamuumiza mlaji. Wanazalisha bidhaa, wanaziuza kwa bei kubwa. Ama wakashindana wao kwa wao, kwa ushindani unaoitwa ushindani wa kukata kimeo, unakuta wawili wanakufa katika wale watano, watatu wanaobaki sasa, wana conspire, wana-collude na kuongeza bei. Kwa hiyo, walaji mnaendelea kuumia. Au waka-merge, wakaungana mtu na dada yake, unadhani ni players wengi, kumbe ni wale wale, halafu ikatokea kuja kumuumiza mlaji.

Mheshimiwa Spika, nizungumze kitu kingine. Kwanini tunatengeneza viwanda? Kutengeneza ajira. Unapo-merge hawa washindani wa matairi ninaozungumza, wanaweza kuungana watu, kwa mfano, ukitokea mtikisiko katika industry katika shughuli; hawa watano wa matairi wakapatwa na mtikisiko, industry ikafa yote, siyo kwamba mmoja akabaki, kafa. Kitatakachotokea ni nini? Ni kwamba itatokea supply itatoka nje. Mtaagiza bidhaa za matairi kutoka nje. Fikiria, mkiagiza kutoka nje, dola mtazipata wapi? Hiyo ndiyo hatari kubwa. Mnapozungumza measure na acquisition, kama industry ikitikisika na kupasuka, you will end up importing. Now, you will end up using the rare dollars you have. Yaani Dola kidogo mliozonazo mtaweza kuzitumia kwa kuagiza bidhaa. Kwa hiyo, nataka kuwaeleza katika industry unapomwangalia…

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Mheshimiwa Mwijage, kuna taarifa kutoka kwa Godwin Kunambi.

TAARIFA

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Spika, namuunga mkono mzungumzaji. Nchi inaponunua sana nje na siyo kuuza, kwenye uchumi naye ataniunga mkono, kuna terminology inaitwa cutoff right inflations, ahsante. (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Mwijage unapokea taarifa hiyo?

MHE. CHARLES J. P. MWIJAGE: Mheshimiwa Spika, naipokea taarifa ya Mheshimiwa Chifu Kunambi. Unajua maprofesa wako juu hapa, watu wanatafuta kiki ya dissertations huko kwa maprofesa.

Mheshimiwa Spika, ninachotaka kuzungumza ni kwamba, industry ina mambo matatu. Moja, players wachache wanaweza kufa, waliobaki wakaua soko, lakini industry yenyewe inaweza kufa mkaamua kuagiza kutoka nje. Kwa mfano, wa Tanga niwaeleze, industry ya cement ya Tanzania iliwahi kupata tatizo la supply. Anafahamu Profesa Muhongo. Mimi na Profesa Muhongo tulikwenda kuwahakikishia Watanzania (Industrialist) kwamba mkaa wa Tanzania ni bora duniani. Yule tajiri namba moja duniani alipotuona, cv yangu na ya Profesa Muhongo, akakubali kwamba mkaa wa mawe wa Tanzania ni mzuri. Nazungumza kuhusu hawa suppliers.

Mheshimiwa Spika, mimi na Profesa Muhongo tulikwenda kuwahakikishia watanzania, kuwahakikishia industrialist kwamba mkaa wa Tanzania ni bora duniani. Yule tajiri namba moja duniani alipotuona cv yangu na ya Profesa Muhongo akakubali kwamba mkaa wa mawe wa Tanzania ni mzuri.

Mheshimiwa Spika, nazungumza kuhusu hawa supplier matokeo yake ni nini? Hii merge, merge ya Twiga na Simba matokeo yake ni kwamba industry inaweza kufa tukaishia kununua bidhaa nje, kwa hiyo merge pamoja na kuangalia sheria huyo ni mwanasheria mimi sijasoma sheria lakini pamoja na kuangalia maslahi ya wananchi lazima tuangalie kwamba tunapoungana hakuna uwezekano wa industry nzima kufa? Ili baada ya kufa bidhaa itatoka nje na ukuzingatia kwamba Tanzania leo tunahitaji saruji kuliko maelezo.

Mheshimiwa Spika, nimeshiriki kwenye ma–group mengi na nimewashauri, niipongeze Serikali kwa kujenga reli sisi hapa tunajiandaa kwa African Continental Free Trade. Kwa hiyo, vigezo vya kuwa na market share vizingatiwe ili kwa kuwa na market share unazuia watu kukurudi, watu kupanga bei na wakawaumiza wale wadogo wanaoota, matabirio yetu sisi ni kutengeneza Tanzania industry ya cement yenye tani 25,000,000 twende mbele kama anavyosema Baba Askofu Gwajima kwamba tuangalie mbele na kuangalia mbele ni kuangalia ile industry isiweze kuyumba.

Mheshimiwa Spika, kwa hayo naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)