Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. JEREMIAH M. AMSABI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Awali ya yote nampongeza sana Rais kwa jitihada kubwa anazozifanya za kutafuta fedha nyingi kwa ajili ya maendeleo ya nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hali hii ya jitihada kubwa za Rais kutafuta fedha kwa nchi yetu kwa ajili ya maendeleo kwa ujumla, nimepata maswali mengi sana, kwa nini sekta ya mifugo inapata fedha kidogo? Nilipoendelea kusoma document yao hii ya bajeti nimeona kuna changamoto kadhaa. Moja, sioni sayansi. Sijaona sayansi kabisa katika document yao. Ukiangalia ni kiasi gani cha fedha kimeelekezwa katika Research and Development, huoni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo tunakutana na changamoto kule Ziwa Tanganyika kwamba ghafla tu ziwa lifungwe. Je, kama tulikuwa tumewekeza kiasi cha kutosha katika R & D, leo tusingekutana na changamoto hii. Kama tungekuwa tumewekeza kiasi cha kutosha katika Research and Development tungepata malisho ya kutosha kwa ajili ya mifugo wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wenzetu Kenya wana ng’ombe milioni 14 peke yake, lakini they are the second largest milk producer katika Afrika kwa ng’ombe milioni 14 tu. Nini walifanya? waliwekeza sana katika research and development. India sasa hivi wanalisha ulimwengu katika maziwa. Asilimia 24 ya maziwa yote duniani yanazalishwa India. Nini India wamefanya? Wamewekeza sana katika research and development. Kwa hiyo, bajeti hii haitoshi kwa sababu hakuna fedha ya kutosha kwenye research and development. Vyuo vyetu vya mifugo pamoja na uvuvi, unaona pesa nyingi ni kwa ajili ya uendeshaji tu, huoni fedha ya kutosha kwenye research. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sioni biashara katika bajeti hii. Ukiangalia katika ufanyaji wa biashara ya mifugo, Tanzania is highly costly. It is very cost kufanya biashara ya mifugo Tanzania. Nimeona kwa mfano biashara ya exportation ya 5 tons za mutton, nyama ya mbuzi, Tanzania gharama ni kubwa sana, ni zaidi ya Shilingi milioni 10 uki-compare na nchi ya Kenya. Kwa hiyo, ile mikoa ambayo iko pembezoni, wana-opt zaidi kufanya biashara Kenya kuliko Tanzania. Badala yake watu wa mifugo wangejielekeza kuhakikisha kwamba economies of scale inaongezeka kwa maana ya ku-encourage wafanyabiashara wengi kwa Tanzania na ndiyo ingeweza kupunguza ule utitiri wa kodi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na wenzetu wa Kenya unaweza ukatumia Shilingi bilioni 15 mpaka 16, wame-cut down zile cost nyingi kwa sababu kuna idadi kubwa ya wafanyabiashara. Kwa kufanya hivi, nchi yetu pia ingeweza kufanya vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia sijaona collection centers za maziwa. Maziwa yetu mengi hayaingii katika mfumo rasmi wa biashara kwa sababu, hakuna milk collection centers. Pale Serengeti tumejaribu kutaka kuweka kiwanda cha maziwa. Utafiti umeonesha, ni lazima mwekezaji atumie pesa nyingi sana kwa sababu bado Serikali haijawekeza kwenye collection centers. Kwa hiyo, tuiombe sana Wizara iende kuwekeza kwenye milk collection centers kwa sababu zitaongezea mapato mengi zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hatuoni miundombinu ya ufugaji. Sasa hivi kule kwetu wanyama wengi wanaingia kwenye mapori, wanaenda kwenye mapori ya akiba, wanaingia kwenye hifadhi kwa sababu hakuna maji ya kutosha, na hakuna malisho. Kwa hiyo, tunaomba sana Mheshimiwa Waziri katika bajeti hii tutengee fedha ya kutosha. Serengeti peke yake tuna zaidi ya ng’ombe 600,000, tunahitaji zaidi ya majosho 30, tunahitaji zaidi ya malambo 25, kwa sababu yaliyopo sasa hayatoshi. Tunakuomba kwa uwekezaji huu, tunaweza tukawa- boost wale wakulima ili waweze kufanya uzalishaji mkubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, bado transformation ya income ya mfugaji ni ndogo. Leo ukienda vijijini wanahitaji zaidi fedha ili waweze kuendesha maisha yao, tofauti na huko nyuma. Pamoja na kwamba pesa hii ya mkulima na mfugaji, bado ingeongeza National income pamoja na individual income. Sasa kazi ambayo wenzetu wa Wizara hii wanayo, ni kuhakikisha maziwa na mazao mengine yote ya mifugo wanaweza kuyabadilisha yakaleta fedha na waongeze ubora, lakini sasa unaona hakuna jitihada hizi zikiendelea. Kwa hiyo, tuombe sana Wizara, wenzetu vijijini nao wanahitaji maisha mazuri, wanahitaji kulipia bili za umeme, maji, wanahitaji kusafiri, wanahitaji vocha, wanahitaji simu na haya yanawezekana kama tuta-transform sekta hii ya maziwa na sekta ya mifugo kwa ujumla wake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda katika vituo vyetu vya uzalishaji wa ng’ombe, ukienda pale Mabuki unaona kazi inafanyika, lakini vifaa gani wanatumia? Teknolojia gani wanayoitumia? Bado ni very old, haiwezi kufanya watu hawa wakasonga mbele, haiwezi kufanya wazalishaji wa maziwa wakapiga hatua kwa sababu, uzalishaji huu ni mdogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiona soko la nyama, bado soko letu la nyama limeendelea kuwa na wasiwasi mkubwa duniani kwa sababu hatu-clear information. Ukiangalia kuna baadhi ya magonjwa ambayo yaliwahi kuikumba nchi yetu na mpaka leo hatujawahi kutoa taarifa katika ulimwengu juu ya magonjwa haya kwamba tumepambana nayo. Kwa hiyo, nadhani ukiangalia kwa ujumla huioni concept ya biashara, huoni jinsi gani Wizara hii imejipanga vizuri ku-trade, huoni namna gani inatafuta information ya masoko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Profesa Muhammad Yunus anadai ukienda China peke yake, mtu mmoja anatumia zaidi ya kilo 60 za nyama kwa mwaka. Ukienda Marekani mtu mmoja anatumia zaidi ya kilo 55 za nyama kwa mwaka; haya yote ni masoko. Ukienda Bangladesh kuna masoko makubwa, ukienda India kuna masoko makubwa, ukienda South Africa kuna masoko makubwa. Lakini kwa nini hatuwezi ku-trap masoko haya, ni kwa sababu hatujakaa kibiashara zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo niwaombe sana wenzetu wakae kibiashara. Tunaomba wawekeze uwekezaji mkubwa, matokeo makubwa ya kufanya vizuri…

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa Amsabi, muda wako umekwisha.

MHE. JEREMIAH M. AMSABI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naunga mkono hoja.