Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Dr. Josephat Mathias Gwajima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kawe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nami nikushukuru sana wewe binafsi kwa kunipa nafasi kuchangia hii hoja iliyoko mbele yetu, ya Wizara ya Uvuvi na Ufugaji. Pia namshukuru Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa bidii yake anayofanya katika kuhakikisha Taifa la Tanzania linajengwa na linabaki salama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia namshukuru Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa ujasiri wake wa kumchagua ndugu yangu Mheshimiwa Ulega pamoja na ndugu yake Mheshimiwa David Silinde kuwa Mawaziri wenye dhamana kwa Wizara hii. Hongereni sana. We have so many good Ministers, and you are one of them. Mungu awabariki sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine, napenda kumpongeza Mheshimiwa Kitandula kwenye mchango wake pamoja na Mheshimiwa Kaijage na Mheshimiwa Mathayo, Mbunge wa Musoma Mjini. Nikuhakikishie Waziri mwenye dhamana ya mifugo pamoja na uvuvi, mimi sitakuondolea Shilingi na ninaunga mkono hoja yako kabla sijaendelea. Nafahamu kwamba umeomba Shilingi bilioni 295.9, hizo sina neno nazo, na nitakupa na akili nyingine ya kupata zaidi ya hapo. Ahsante sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichokoze jambo. Kwenye document ya mtani wangu, Mheshimiwa Waziri Ulega, kwa niaba ya Serikali, ametuonesha kwamba, sekta ya uvuvi inachangia asilimia moja ya pato la Taifa. Hili jambo ni hatari sana kulisikia au kusemwa mbele ya watu wenye akili timamu. Nichokoze jambo ambalo litamfanya kila mtu afikiri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania ukianzia kwenye maji ya chumvi; tuna mikoa ambayo imezungukwa na maji ya chumvi. Kwanza ni Dar es Salaam, Mkoa wa Pwani, Mkoa wa Lindi, Mkoa wa Mtwara, Mkoa wa Tanga na Zanzibar yote. Hii ni mikoa almost mitano pamoja na Zanzibar, yote imezungukwa na maji. Ukiamua kuangalia maziwa tuliyonayo, tunayo mikoa ambayo na yenyewe imezungukwa na maji ya maziwa, siyo kwa maana ya maziwa ya kunywa, ni kwa maana ya lakes. Mkoa wa Mwanza umezungukwa na maji, Mkoa wa Mara, Mkoa wa Simiyu, Geita, Kagera, Mbeya, Kigoma, Katavi, Rukwa, Ruvuma, Arusha kuna Natron, mpaka kuna Ziwa Jipe Kilimanjaro, kuna Manyara, mpaka kwa Wagogo hapa kuna Mtera, tumezungukwa na maji mpaka Njombe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukijaribu kuunganisha hizi dots za hii mikoa 16 niliyoitaja yote iko kando ya maziwa. Unaunganisha na hii mikoa mingine niliyoitaja ambayo iko kando ya maji ya chumvi, unakuta mikoa 22 yote imezungukwa na maji. Sasa kwa akili ya kawaida, it doesn’t hold water kugundua kwamba liko tatizo tunaloli-face ambalo tunahitaji kulitatua kwa pamoja ili kuongeza mapato ya Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nijaribu kufanya troubleshooting kidogo. Kwanza, haikubaliki kwa namna yoyote ile kwamba uvuvi uchangie asilimia moja peke yake kwenye pato la Taifa, haiwezekani ukilinganisha na resources tulizonazo. Sasa ushauri wangu wa kwanza ambao umesemwa na wale niliowashukuru; kwanza, ni muhimu sana kufanya sekta ya uvuvi kuwa mamlaka. Kama ambavyo tumefanya kwenye Wakala wa Misitu, tumefanya TANAPA, wote hao wako chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii, lakini mamlaka itaongeza chachu ya namna ya kutumia maji yetu ambayo tumepewa na Mwenyezi Mungu kwa ajili ya kuongeza pato la Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ambalo nashauri, sasa wakati umefika Wizara hii ya Uvuvi pamoja na Mifugo kuwa na vision ya muda mrefu ya nchi. Nilipata faraja sana nilipoona ule mchakato wa Uzinduzi wa Mpango wa Taifa. Nilikuwa disappointed tu kuona kwamba ni miaka 25 peke yake tunawaza, nilifikiri tungewaza miaka 50 ya Mpango wa Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kinachotupa shida hapa sisi, kwa mfano, tunasema tuna idadi ya ng’ombe milioni 36.6, tuna idadi ya mbuzi milioni 26.6, tuna idadi ya kondoo milioni 9.1, lakini wakati huo huo tumesema tunazalisha maziwa lita bilioni 3.6, maziwa tunayozalisha kwetu. Wakati huo huo tuna idadi ya mifugo wote hao na maziwa yote haya, lakini tumetoa vibali vya watu kuleta maziwa tena hapa nchini kutoka nchi nyingine. Tumetoa vibali 605 vya kuingiza maziwa na lita tulizoingiza ni lita milioni 11.6 za maziwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa unaweza kuwaza, tuna mifugo hapa mingi sana, tuna lita za maziwa nyingi sana, tunatoa vibali vingine tena 605 vya watu wengine nao walete maziwa hapa. Inawezekana labda hayatoshi kwa maana ya ku-compensate, lakini thamani ya maziwa yaliyoingizwa ilikuwa ni Shilingi bilioni 22.7 thamani ya maziwa ambayo tumeingiza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, it doesn’t make sense kama tumetumia fedha ya kigeni kununua maziwa kwa 22.7 billion. Kwa nini tusi-reserve hizi fedha za kigeni, tukaamua kuwa na vision kabisa ya muda mrefu inayohusu uvuvi. Tukasema, uvuvi tuupe vision ya miaka 50 na mifugo tuipe vision ya miaka 50, kuwe na blue print kabisa ya uvuvi na blue print kabisa ya mifugo, ili kila Waziri anapoingia kwenye Wizara hii aikute hii blue print imekaa tayari. Tutajikuta tuna continuation kwenye hizi Wizara na pato litaongezeka. Nachelea sana mtani wangu, kama huna blue print siyo muda mrefu utaanza na wewe kupima samaki pale kwenye restaurant ya Bunge hapo kwa sababu, utakosa cha kufanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishukuru sana Wizara ya Fedha na Mipango walipoanza kuzindua ule mpango wao wa kuwa na vision ya muda mrefu. Kwa sababu, it doesn’t make sense kwamba tuna TANAPA, ni mamlaka, lakini iko chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii; tuna TFS ni mamlaka iko chini ya Wizara hiyo hiyo; why not uvuvi, tukawa na mamlaka, na hiyo mamlaka ikatengeneza vision ya uvuvi ya muda mrefu, ili kila Waziri anayeingia anatembea kwenye hiyo hiyo vision tukaongeza fedha katika nchi yetu? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesikia watu wengi sana wanamtia moyo mtani wangu kwamba, pesa aliyopewa ni kidogo. Nikupe siri ya kupata sealing kubwa kwenye hiyo pesa yako. Unless unapeleka vision kubwa kwa mamlaka, mamlaka haiwezi kukupa sealing kubwa. Ukiipelekea mamlaka maono makubwa kwamba, mimi bwana kwenye Wizara yangu, katika eneo la uvuvi nataka kuwa na vision hii hapa. Hii vision italeta asilimia 10 ya pato la Taifa. Hiyo mamlaka itaona hiyo vision yako itakuongezea sealing yako, itakuwa ni rahisi sana, kuliko ile kusema tu kwamba, uongezewe. Za nini? Hata kama ningekuwa ni mimi, nataka kukuongezea mtani wangu, za nini? You don’t lay your plan; you have to lay your plan. It is a proposal that attracts finances. Kwa hiyo, lazima uweke mpango wako wa muda mrefu. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Naomba kuunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)