Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa nafasi, naomba nianze kwanza kwa kusema ninaunga mkono hoja. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimesoma kwa kweli pia maandiko mbalimbali ambayo Mheshimiwa Waziri amewasilisha na nimemsikiliza vizuri kwenye hotuba yake ambapo kuna wakati alikuwa anaacha kusoma anatuelezea anachokifikiria kufanyika. Ninampongeza kwa maoni hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri amesema kwamba uvuvi mpaka leo unachangia pato la Taifa kwa asilimia 1.8. Ukitazama namna ambavyo nchi yetu imebarikiwa, namna ambavyo tumezungukwa na maji karibu nchi nzima ukianzia Ziwa Victoria, ukaenda Tanganyika, ukaenda Nyasa, ukaenda baharini na vibwawa vidogovidogo vilivyopo katikati ya nchi, ungetamani kuona mchango wa sekta ya uvuvi unafika asilimia 10 kwenye Pato la Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na tumefeli wapi; amezungumza hapa mzungumzaji aliyetangulia kwamba sisi tungeweza kuwa tunaongoza katika mauzo lakini pia tungeweza kutawala soko la Maziwa Makuu. Jambo kubwa ambalo Mheshimiwa Waziri nataka kukuhakikishia kwamba tumefeli; kwanza, tumekuwa na usimamizi mbaya wa rasilimali hizi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa nini sasa hivi tunazungumzia kushamiri kwa uvuvi haramu; miaka michache nyuma tulifaidika na takwimu za mauzo makubwa nje – amesema Mheshimiwa Mwijage – tukafaidika na takwimu za ongezeko dogo la samaki Ziwa Victoria, kwa sababu tulitumia nguvu kubwa ya operesheni kwenye kufikisha ujumbe wa namna ya kutunza maliasili.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa matokeo ya operesheni ni yapi. Kwanza, tulipata ongezeko la muda la mauzo ya samaki nje, tukaongeza mapato kutokana na faini kwa sababu tulikuwa tunapiga sana faini. Sasa matokeo yake ni kwamba wavuvi wakubwa wote waliokuwa Ziwa Victoria wakaacha kufanya hiyo kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na wanapoacha kufanya hiyo kazi kutokana na kufilisika – na kwa kweli walifilisiwa na Serikali, maana yake ni kwamba wanaokuja ni wavuvi wadogowadogo ambao hawana uwezo wa ku-access gharama kubwa ya zana za uvuvi na lazima watavua kwa uvuvi haramu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hatuwezi kuja leo tunashangaa kupungua kwa samaki, genesis yake tuliitoa huko. Tulipaswa kuja na programu ambayo itadumu ya kudhibiti uvuvi haramu na kuhakikisha kwamba tunalinda maliasili katika maziwa yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tukaja na zimamoto ya operesheni ambayo ninafikiri Mheshimiwa Waziri usipozingatia ndio utakuwa ushauri wako utakaopewa na wataalamu, na operesheni iliwafaidisha zaidi watu wako wa chini ambao walitumia operesheni hiyo kuonea watu na matokeo yake watu wote wakaona uvuvi siyo kazi ya mtu mwenye akili timamu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, leo Mheshimiwa Mwijage amezungumza habari ya ongezeko la illegal fishing, amezungumzia ongezeko la bycatch. Bycatch kwa nini ni nyingi; ni nyingi kwa sababu watu wa BMU hawafanyi kazi huko chini tulikuwa na BMU zamani na kazi yao kubwa ilikuwa ni kuhakikisha wanamlinda mvuvi wao wenyewe, Wavuvi wenyewe wanalindana.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini la pili, hatuna wataalam. Ukiangalia ajira za Serikali zote zinazotoka ni kama vile uvuvi tume u-abandon, yaani kama si jambo muhimu. Watu wanasoma kwenye vyuo hawaajiriwi. Unatembea mialo kumi afisa uvuvi mmoja, halafu unategemea kudhibiti Uvuvi haramu, unaudhibiti vipi? Haiwezekani; uvuvi haramu unatoka wapi; ni kutokana na dhana kupanda, wasimamizi hawapo, na ukianzisha operation unakwenda kuonea watu.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nilitaka kushauri; uwepo wa, kuzungungukwa na maji katika nchi yetu bado haijawa baraka, bado sisi tunaona kama vile ni laana. Tunachotaka ukifanye sasa hivi, hakikisha tunapata dhana za uvuvi kwanza kwa bei nafuu, lakini watu wako walioko huko chini waimarishe zaidi kwenye kutoa elimu kuliko kwenye kufanya operation kwa sababu mtu akipata elimu ataambukiza kizazi chake na kizazi kingine.

Mheshimiwa Naibu Spika, na jambo lingine ni lazima to control hizi breeding areas. Maeneo yote ambayo zamani yalikuwa ni mazalia ya samaki sasa hivi yamevamiwa. Hii ni kwa sababu ile operation baada ya operation namna tena mtu anafanya kazi kule ziwani. Mimi nataka nikuhakikishie Mheshimiwa Waziri ukilisimamia hili samaki watarudi ziwa Victoria, lakini yako mambo ambayo lazima tufanye.

Mheshimiwa Naibu Spika, duniani sasa hivi hawategemei tu mazalia ya samaki ya natural kutokana na uharibifu wa mazingira, ndiyo maana unaona watu wana-invest kwenye cages kwenye uvuvi wa vizimba, ufugaji wa vizimba. Lile Ziwa Victoria na ukubwa wake ukiweka vizimbaa kila kona hatuwezi kuwa na kilio cha samaki.

Mheshimiwa Naibu Spika, soko la samaki liko obvious Tanzania kuna soko la samaki na nje ya nchi kuna soko la samaki. Hatuwezi kuendelea kutegemea kwamba wale wanaozaliwa mle kwa sababu ya asili ndio tuendelee kuwategemee kuuza nje haitawezekana. Ukienda nchi zote ambazo ni leading export wa samaki wanatumia vizimba, kwa hiyo weka fedha nyingi hapo. Shida tuliyonayo Tanzania sasa hivi vizimba ni bei ghali sana, chakula cha kuku ni bei ghali sana; lakini kuna urasimu mkubwa kwenye kufikia malengo hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kwa sababu ya muda na kwa sababu sitaki kuacha kuzungumza habari ya mifugo, nataka nikushauri hapo kwamba lazima utakapoamua kulisimamia jambo hili huko chini watu wako miiko ambayo wanapelekewa; lazima tuongeze idadi ya staff lakini watu walitumia vibaya sana madaraka yao na matokeo yake tukawa na mafanikio ya muda yaliyopelekea watu wengi kuwa maskini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili ni kuhusu suala la mifugo. Nimeangalia takwimu zako za mapato ya mifugo, kwa mtu akikusikiliza ambaye haijui Tanzania…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)