Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa nafasi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ninamshukuru Mwenyezi Mungu kwa afya njema ambayo ametujalia na ninampongeze Mheshimiwa Daktari Samia Suluhu Hassan, kwa kazi kubwa ambayo anaendelea kuifanya kwa nchi yetu. Kipekee kabisa kwa niaba ya wananchi wa Kiteto, Wizara ya Mifugo imetuletea majosho karibu Nane, bwawa kubwa la karibu Milioni 500. Tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais na tunaendelea kumuombea Mwenyezi Mungu aendelee kumpa afya njema aongoze Taifa letu vizuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pili nampongeza Mheshimiwa Makamu wa Rais Mheshimiwa Dkt. Isdory Mpango kwa kuendelea kumsaidia Mheshimiwa Rais, nampongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu Mheshimiwa Majaliwa Kassim Majaliwa kwa kuendelea kumsaidia Rais kutekeleza majukumu yake.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninampongeza Waziri wa Mifugo, rafiki yangu Mheshimiwa Ulega, kwanza ninampongeza kwa kuaminiwa na Mheshimiwa Rais kuongoza Wizara hii ya Mifugo na ninakupongeza kwa ziara mbili ulizofanya Kiteto. Umekwenda mpaka huko kabisa machungani, ulitutembelea wakati wa majanga ya ukame na uliona mifugo na ukatutembelea tena wakati tunatembelea Bwawa la Kawa, nakushukuru sana Mheshimiwa Waziri. Pia ninampongeza Mheshimiwa Naibu Waziri, Mheshimiwa Silinde, nampongeza Katibu Mkuu na timu nzima ya Wizara ya Mifugo kwa kuendelea kumshauri Mheshimiwa Rais. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine niipongeze Timu ya Wananchi ya Yanga kwa kazi kubwa waliyoifanya na kuijengea heshima nchi yetu.(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo sasa naomba nijadili changamoto zinazotokana na Wizara hii ya Mifugo. Moja ni mabwawa na majosho. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Ilani ya Chama cha Mapinduzi ukurasa wa 50, 51 na 53 tuliahidi Watanzania kwamba tutajenga mabwawa karibu 454 maana yake mwaka ni mabwawa 92. Ninaomba sana Serikali iiongezee Wizara hii pesa nyingi sana ili tuweze kutimiza ahadi hizi kwa Watanzania. Nachelea kusema kwamba Wizara hii inapata pesa kidogo sana, ninamuomba sana Mheshimiwa Rais na Serikali waongeze bajeti kwenye Wizara hii, angalau hata Bilioni 500 itasaidia ili Wizara hii iweze kutimiza yale yote ambayo tuliyasema.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano majosho, tulisema kila kijiji chenye mifugo kiwe na josho. Kwa Wilaya ya Kiteto peke yake idadi ya mabwawa tuna upungufu wa mabwawa karibu 44, majosho 48. Pamoja na nguvu alizotusaidia Mheshimiwa Waziri hii inaonesha kwamba bado upungufu ni kubwa, mabwawa kama ya Dosidosi, Sunya, Njoro, Kinyungu, Matui, Sunya yote ni mabovu na kwa kweli Mheshimiwa Naibu Waziri tunaomba pesa kwa ajili ya mabwawa haya.

Mabwawa kama ya Dosi, dosi, ya Sunya, Njoro, kijungu, Matui. Sunya, yote ni mabovu na kwa kweli, Mheshimiwa Naibu Waziri, tunaomba pesa kwa ajili ya mabwawa haya na Bwawa la Kaiwang Mheshimiwa Waziri endelea kufuatilia ili Watanzania wale wapate kunufaika na nguvu za Mheshimiwa Rais. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pili, ni maeneo ya malisho. Salama ya wafugaji nchi hii ni kuwa na maeneo salama ambayo yamelindwa kisheria. Kwa hiyo, naipongeza Wizara kwa kuendelea kufanya hivyo, lakini tuendeleze kasi. Hii itaondoa migogoro baina ya wafugaji na watumiaji wa ardhi wengine. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tatu, ni suala la umasikini kwa wafugaji. Mheshimiwa Waziri alikuja Kiteto. Ukame ule kwa Kiteto peke yake tulipoteza ng’ombe karibu 25,000 na sasa tafiti zinasema; kwa sababu kuna dhana fulani watu wanafikiri wafugaji ni matajiri tu, lakini tafiti zinasema, asilimia 20 ya watu wanaomiliki mifugo; asilimia 20 wanamiliki asilimia 80 ya mifugo iliyopo. Kwa hiyo, hii ni picha tu inayoonesha kwamba gap lililopo, na siyo kwa sekta ya mifugo peke yake, hata kilimo. Kwa hiyo, vizuri Mheshimiwa Waziri hebu mlifanyie utafiti ili dhana zinazojengeka kwamba wafugaji ni matajiri ifahamike kwamba siyo kweli.

Mheshimiwa Naibu Spika, ufugaji wa kisasa unaozungumzwa kila wakati, kila Mtanzania angependa kufanya kitu chenye tija zaidi, lakini lazima tufahamu kwamba sekta ya mifugo tuna makundi matatu; kuna watu wanaofuga kiasili na kibiashara na ni sehemu ya maisha yao, ambao ndio Watanzania walio wengi, lakini kuna watu wanataka kujifunza biashara ya kufuga ng’ombe na kunenepesaha, na hapa wakiwemo Serikali. Serikali wanafanya biashara. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunapotengeneza mikakati lazima tufahamu kwamba haya makundi matatu yapo. Kufanya biashara ya kunenepesha siyo kitu kidogo. In fact nimewatembelea wafugaji wawili ambao wanajaribu kufanya ufugaji huu unaoitwa ni wa kisasa. Mmoja mwenye hekta 100 amepiga fence, na miundombinu ame-develop, na kuweka ng’ombe hawa mnaowaita wa kisasa, ni karibu Shilingi milioni 400 mpaka 500, investment.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikamtembelea mfugaji mwingine mdogo sana, ana hekta 20, anajaribu kutengeneza shamba. Hata hiyo, tunayosema ni kidogo ni Shilingi milioni 50.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, at times tukisema kwamba tufuge kisasa, mjue mkituletea hizo pesa, tuko tayari. Otherwise mfahamu kwamba mifugo ni sehemu ya maisha ya wananchi. Wakati mwingine tukisema tufuge kisasa bila kutuwezesha na tukapata nyenzo zinazohitajika, tunafikiri kama hamtufahamu vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kukamatwa kwa mifugo kwenye maeneo ya hifadhi, imekuwa ni kero kubwa sana. Namshukuru hapa Mheshimiwa Waziri Mkuu, kauli aliyoitoa Mheshimiwa Waziri Mkuu hapa, hebu fuatilieni vizuri sana kwa sababu kukamatwa kwa mifugo katika maeneo haya, imeanza kuwa kero kubwa sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, watu wanakamata tu ng’ombe, watu wanakwenda Mahakamani, wanashinda kesi, lakini hawapewi mifigo yao. Nina mwananchi wangu anaitwa Lenina, mpaka leo ni karibu miaka mitatu hajapata haki zake.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ni vizuri mwangalie, mzungumze na Waziri wa Maliasili na Utalii, make, mtengeneze. Kama anapenda kukamata ng’ombe zaidi, aambiwe kuna kanuni zilitengenezwa na Wizara ya Mifugo chini ya Sheria inaitwa The Animal Welfare Empowerment Animals Regulations of 2020. Kama anaweza ku-afford kwenda kuwatunza hao ng’ombe kwenye maeneo ya hifadhi, afanye hivyo, lakini kama hawezi, aachie ng’ombe, awakamate wafugaji. Kwa sababu tunawafanya wafugaji wanakuwa masikini unnecessarily. Ni jambo la kukaa na kuzungumza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la mikopo na benki, Mheshimiwa Waziri amezungumza hapa kwamba twende kwenye benki. Kama kuna mradi ambao unafeli ni wa benki. Mfugaji anakwenda anataka mkopo, halafu unamwambia lete security, eti lete nyumba. Sasa kwani huyu mfugaji anafanya real estate? Kwa nini mifugo isiwe security? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mifugo ni mali kama mali nyingine. Kama kuna haja ya kutengeneza insurance ama bima kwa ajili ya mifugo ili tupate security tufanye hivyo, lakini hatupendi sana. Unakwenda una mifugo wazuri tu, eti mtu anakwambia nenda kalete hati ya nyumba au kalete shamba. Huyu hafanyi real estate, wala Halimi. Eeh, mtengeneze module ambayo inamfanya mfugaji aweze kukopesheka. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la chanjo. Ilani imezungumza habari ya chanjo hizi za magonjwa 13, lakini wakati mwingine tunahisi kama haiji kwa wakati. Kwa hiyo, lazima Serikali iweke mkakati wa kuleta chanjo hizi kwa wakati ili wafugaji wapate huduma hizi kwa haraka zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho kabisa, nataka Mheshimiwa Waziri atengeneze wafugaji mabilionea. Wengine wametengeneza mipango mingi. Omba tu Mheshimiwa Rais akupe Shilingi bilioni 27,600,000,000/=, utapeleka katika majimbo yote 184. Karibu Shilingi milioni 150 watapewa vijana Hamsini Hamsini, watakuwa ni vijana 9,200 baada ya miaka miwili, utarudishiwa hizo pesa.

Mheshimiwa Naibu Spika, unajua lazima tuwe practical. Hii habari ya kufanya tafiti na kufanya workshop, sijui na kufanya ma-interview ambayo yanapoteza muda, tafuta hizo hela, ukipeleka hiyo milioni 150 kila jimbo, mtuachie kazi ya ku-recruit vijana ambao wanafanya hizi kazi za mifugo. Ukifanya hivyo, baada ya miaka miwili hiyo pesa itarudi, lazima tuwe practical. Hatutaki tena mambo ya kusoma mavitabu haya na matafiti. We have spent time, sixty years down the line, tunasoma tu ma-documents. Tunataka tuwe practical. Kwa hiyo, ifike mahali, nakuombea pesa nyingi zaidi, ukipata nadhani itatusaidia sana kutekeleza hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, kwa ahili ya interest ya muda, naunga mkono hoja. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsanteni sana. (Makofi)