Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Katiba na Sheria

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba nikushukuru kwa nafasi, pia nimshukuru Mwenyezi Mungu kutupa nafasi hii tena, kutupa afya njema kuendelea kutekeleza wajibu wetu katika wizara hii. Nimshukuru Mheshimiwa Waziri kwa maelekezo yake, Mheshimiwa Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan kwa jinsi ambavyo ameendelea kutupa imani sisi wasaidizi wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nita-respond kwenye mambo machache. Jambo la kwanza nimshukuru Mheshimiwa Neema Lugangira kwa mchango wake. Ametoa ushauri mzuri kwa Wizara yetu; na kubwa zaidi ametoa ushauri kwamba wakati tunarekebisha sheria hizi za vyama vya siasa basi Tume yetu ifanye kasi kuleta marekebisho hayo na tuweze kuyaleta. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba ukiangalia bajeti zetu hapa miongoni mwa kasma ambazo zimetuongezea fedha katika Tume yetu hii ya kurekebisha sheria ni pamoja na kazi hizi kumalizika na Tume yetu ilishamaliza utafiti katika sheria hizi za uchaguzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Neema, Mbunge, mawazo yako hayo ni mazuri na yataendelea kuzingatiwa pale ambako tutaleta sasa marekebisho haya basi tutaendelea kuboresha; lakini kwa sasa kama wizara tumechukulia serious na ndio maana katika bajeti ya Tume kumekuwa na ongezeko la fedha ili kazi hizi ziendelee. Pia tunawapa kipaumbele kwa kuwa tunaelekea kwenye mwaka wa uchaguzi wa Serikali za mitaa na uchaguzi mkuu sheria hizi ziangaliwe kwa jicho la karibu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge pia ametushauri katika suala zima la katiba mpya kwamba ushirikishwaji wawe wazi, asasi mbalimbali zishirikishwe, NGO’s na taasisi zingine na wananchi kwa ujumla washirikishwe. Hili ni la msingi, ndiyo maana tumekuja kwenye Bunge hili mkiona kwenye bajeti zetu kuna ongezeko kwa ajili ya kazi hii ya mchakato wa katiba na ni fedha kubwa. Tushukuru Bunge hili kwamba mmeliona hilo kuanzia kwenye kamati lakini Mheshimiwa Rais wetu Mama yetu Mama Samia Suluhu Hassan. Kazi hii itakapoanza tutashirikisha kote Bara pamoja na zenzetu wa Zanzibar, wananchi watatoa maoni yao mchakato utakuwa wa wazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni suala la viongozi wetu wa Serikali za Mitaa, Mheshimiwa Mbunge amelizungumzia; kwamba wasiondolewe kienyeji. Kwa sasa taratibu ziko wazi kabisa chini ya Serikali zetu za Mitaa, chini ya Ofisi ya DC akisadiwa na makatibu tarafa jambo hili limekuwa likifanyika kwa kufuata taratibu, Mwenyekiti wa Kijiji au Mtaa haondolewi tu bila utaratibu. Lakini katika marekebisho na maboresho haya ambayo yanaletwa na Tume basi tutaliangalia kama kuna mapungufu, lakini kwa sasa utaratibu uko vizuri na wananchi wanashirikishwa. Tunafahamu mkutano mkuu wa kijiji unakuwepo lakini taratibu hizo zinasimamiwa na ofisi zetu za wakuu wa wilaya na mambo haya yamekuwa yakifanyika kwa uwazi ili mtu pia ajitetee kama anatuhumiwa kwa jambo lolote lile.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Jesca amechangia kwenye Tume yetu ya Haki za Binadamu na umuhimu wa Tume hii. Tume hii ni muhimu kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge amesema. Tume hii imekuwa ikifanya kazi zake. Naomba nimrifae (to refer) Mheshimiwa Mbunge katika ukurasa wa randama yetu kazi ambazo tume imefanya ukurasa wa sita mpaka saba, pale utaona kazi ambazo Tume imefanya. Pale ambako kuna ukiukwaji wowote wa haki za binadamu Tume hii haijafungwa mikono na imekuwa ikifanya kazi zake siku zote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, good enough taarifa zake tumeshazikabidhi kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu zitaletwa kwenye Bunge hili hakuna ambaye anazuia Tume hii isilete taarifa katika Bunge hili. kwa hiyo baada ya Tume kutukabidhi hizi taarifa kama Wizara taarifa hii tumekabidhi Ofisi ya Waziri Mkuu na taarifa hizi zitaletwa katika Bunge hili Tukufu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jingine ni suala la bajeti ya Tume hii. Mheshimiwa Mbunge Agnesta amelizungumzia kwa kina, kwamba tume hii haipati fedha ipasavyo. Ukiona kwenye disbursement ya fedha kwa mwaka huu unaondelea Tume imepata zaidi ya asilimia 60, yaani kwenye disbursement wamepata fedha na ndiyo maana wamefanya kazi hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia katika increment za bajeti kwa miaka mitatu mfululizo Tume hii imekuwa ikiongezewa fedha ili iweze kufanya kazi zake ipasavyo. Na tumeona, miaka mitatu mfululizo bajeti yao ilikuwa five billion, lakini mwaka uliofuata six billion, mwaka huu Bunge lako Tukufu litakaporidhia, na tunashukuru kamati zimeridhia bajeti hii ya ongezeko kwa Tume, Tume imepitishiwa zaidi ya eight billion ambayo kwa kweli sisi kama wizara tunafahamu umuhimu wake. Kimsingi ndiyo maana tunaona katika nyongeza za bajeti Tume hii haijaachwa. Kwa hiyo nimwakikishie Mheshimiwa Jesca kwamba Tume hii itaendelea kufanya kazi zake kwa umakini pia Serikali na Wizara tumekuwa tukiangalia kwamba inapata fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kwamba fedha za maendeleo ni kweli lakini Tume haisimami peke yake. Wizara hii tuna taasisi nyingi tumekuwa tukishirikiana katika miundombinu. Tume haijakwama kazi zake kwa kuwa haina miundombinu, ndiyo maana hata kwa upande wa Zanzibar Tume ina ofisi zake. Kwa hiyo kadri tunavyoendelea kupata fedha na kutenga fedha kwa ajili ya Tume hii na hata miundombinu tutaendelea kurekebisha vile ambavyo bajeti itaendelea kuruhusu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante naomba kuunga mkono hoja.