Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua nafasi hii kuungana na Watanzania wenzangu wote kumshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kutujalia baraka zake katika Taifa letu nyakati zote kwa kutujalia amani, upendo, mshikamano na kutuepusha katika majanga mbalimbali makubwa nyakati zote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya wananchi wa jimbo langu nachukua nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na viongozi wetu wote kwa jinsi wanavyoliongoza Taifa letu na walivyosimamia utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa kipindi cha mwaka 2020 – 2025, kwani kuna mafanikio makubwa sana katika nyanja za kidiplomasia, kiuchumi, maridhiano ya kisiasa, ustawi wa jamii na utatuzi wa kero mbalimbali kwa kutekeleza miradi ya maendeleo kwenye sekta zote nchini. Aidha tunaendelea kuiombea nchi yetu baraka za Mwenyezi Mungu katika ulinzi, amani, mafanikio na mshikamano kitaifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunamwombea kwa Mwenyezi Mungu Mheshimiwa Rais wetu, viongozi na watendaji wetu wote awajaalie mafanikio mbalimbali katika kuliongoza Taifa letu wakati wote wanapotekeleza majukumu yao wakati wote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba kutoa mchango wangu kupitia hotuba ya mapendekezo ya bajeti ya Wizara hii ya Katiba na Sheria iliyowasilishwa katika Bunge letu hivi punde.

Pia Serikali iangalie mpango wa kufufua Mahakama za Mwanzo katika ngazi za tarafa ambazo zilianzishwa toka enzi za mkoloni ili kurahisisha wananchi kupata huduma za mahakama kwa ukaribu zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iangalie uwezekano wa kujenga mahakama zote kongwe zilizoanzishwa toka enzi za mkoloni ambayo majengo yake yote ni chakavu sana kwa sasa, mfano wake ni Mahakama ya Wilaya ya Mbulu ambayo ilijengwa na mkoloni toka mwaka 1934 ambayo kwa sasa ni chakavu sana na iko ndani ya mita kumi ya hifadhi ya barabara kuu hali inayosababisha kelele nyingi sana za magari yanayopita wakati shughuli za mahakama zikiendelea na kuhatarisha usalama wa wananchi waliokuja kusikiliza mashauri ya ndugu zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo basi nawasilisha maombi mahususi Wizarani kutupatia fedha za ujenzi wa jengo hilo la mahakama katika bajeti hiyo na tayari uwanja umeshapatikana, pia nitashukuru sana kama Wizara itatuma wataalamu wa Wizara kuja kuona hali halisi ya jengo hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iangalie utaratibu wa uteuzi wa wazee wa mahakama nchini kwa kuwekwa wazi kwa wananchi wa wanaopokea huduma katika eneo hilo na namna ya kuwahudumia kwani uwepo wao ni muhimu na kutaisaidia mahakama kutekeleza majukumu yake kwa uwazi zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaiomba Serikali itoe kwa asilimia 100% fedha za ujenzi wa mahakama zinazoombwa katika kila mwaka wa bajeti nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja kwa 100% na naomba kuwasilisha.