Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Eric James Shigongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. ERIC J. SHIGONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niamini kwamba tunachangia kwa dakika 10 na ninataka nizitumie dakika 10 hizi kwa kutoa mchango wangu kwa kifupi tu na ninaomba Wabunge mnisikilize kwa makini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ibara ya 144 imetamka juu ya Security of Tenure. Security of tenure ya kwamba ziko nyadhifa katika taifa hili lazima watu walindwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitasoma kidogo Ibara ya 144(1); Bila kuathiri masharti mengine yaliyomo katika ibara hii, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu wa Jamhuri ya Muungano atalazimika kuacha kazi yake atakapotimiza umri wa miaka sitini au umri mwingine wowote utakaotajwa na Sheria iliyotungwa na Bunge.

(2) Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu aweza tu kuondolewa katika madaraka ya kazi yake kwa sababu ya kushindwa kutekeleza kazi zake (ama kutokana na maradhi au sababu nyingine yeyote).

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesoma ibara hii kuonyesha ya kwamba Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kwamba CAG awe protected na hiyo security of tenure.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuko katika vita dhidi ya rushwa kwenye Taifa letu. Mara ya mwisho niliposimama hapa nilisema kwamba watu wanaiba, wanaiba, wanaib. CAG ameleta ripoti tena hapa bado wizi unaendelea na unazidi kuongezeka. Sasa, kwa nini nimesimama kuzungumza, nimesimama hapa kwa sababu ya mtu mmoja ambaye ninamwona ni wa muhimu sana kwenye vita dhidi ya rushwa kwenye Taifa langu; mtu huyu ni Mkurugenzi wa TAKUKURU.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkurugenzi wa TAKUKURU ambaye CAG akikamilisha kazi yake anamkabidhi mafaili yote anapata kibali cha Mwanasheria Mkuu wa Serikali, anaenda kufungua kesi mahakamani kuwashitaki watu lakini hawi protected na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kazi yake ni kubwa anashughulika na watu wakubwa, watu wenye uwezo lakini hana protection yoyote kama mwenzake CAG.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa najiuliza, kwamba jambo hili lilifanyika kwa bahati mbaya au lilifanyika kwa lengo gani? Kwamba yule anayechukua kazi kwa CAG na kupeleka mahakamani na kupata kibali cha mwendesha mashtaka na kushitaki watu hawi protected. Ukienda upande wa pili wa Tanzania Zanzibar iko protected, Kenya yuko protected, Sierra Leone yuko protected, analindwa. Naongea hapa kwa sababu ya confidence, mtu huyu anahitaji confidence, awe na uhakika wa kazi yake alindwe na sheria ili iweze kutimiza majukumu yake sawasawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukatae tukubali wako watu kwa simu moja tu mambo yanaweza yakabadilika, ushahidi unaweza ukabadilishwa na vitu vikabadilika kabisa na kesi isifike hata mahakamani, kwa simu moja tu. Nitatoa mfano mmoja mfupi tu, Yesu alipokufa siku ya Ijumaa, Maria alipoenda kuomba mwili wake kwa Pilato, Pilato alikataa kutoa ule mwili. Mtu mmoja aitwaye Joseph Halimataya mtu mwenye nguvu na ushawishi, Maria alipoenda kwake kulia akamwambia twende, walipofika ofisini kwa Pilato akauliza mzee yupo akaambiwa yupo lakini ana mgeni, akasema ngoja nichungulie kidogo tu anione, alipofungua mlango hivi Pilato alivyomwona akasimama akamwambia karibu mzee, mgeni aliyekuwepo ndani akaambiwa subiri kwanza niongee na Joseph wewe usubiri. Kwa nini natoa huu mfano, wako watu wana nguvu, wako watu wana ushawishi, wanaweza kumpigia simu moja tu Mkurugenzi wa TAKUKURU na mambo yakabadilika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka tumpe uhakika Mkurugenzi wa TAKUKURU ili afanye kazi zake kwa confidence, afanye kazi yake vizuri bila hofu ya kwamba nitafukuzwa kazi kesho, ukishamteua iwe kazi kumwondoa. Maana yangu ni nini, mimi mwenyewe hapa namkumbuka kaka yangu mmoja, sitaki kumtaja jina hapa, aliwahi kusema msinitilie kitumbua changu mchanga. Hata yeye Mkurugenzi wa TAKUKURU ana watoto, ana familia kuna mambo mengine anaweza akaacha kuyashughulikia kwa sababu tu anaogopa kazi yake inaweza ikapotea. Nani hataki heshima, nani hataki kutembea kwenye hiyo shangingi kila mtu anataka hata mimi nataka. Niko tayari ku-compromise wakati mwingine ili nibaki ofisini. Wako watu wamedhurika kwa sababu walishindwa kutekeleza maelekezo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nachokiomba wakati umefika wa sisi kufikiria sasa jinsi ya kum-protect Mkurugenzi wa TAKUKURU. Jambo hili si geni, Zanzibar inafanyika nimesema, Sierra Leone wanafanya na Kenya wanafanya kwa nini Tanzania hatuwezi kum-protect mtu huyu? Umem-protect CAG, anafanya vizuri, lakini Mkurugenzi wa TAKUKURU hana
protection.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niishie hapo niunge mkono hoja, ahsante sana kwa kunisikiliza. (Makofi)