Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Rashid Abdalla Rashid

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiwani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. RASHID ABDALLA RASHID: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi hii na mimi leo niweze kuchangia hotuba hii ya Waziri Mkuu. Kwanza na mimi niungane na wenzangu kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuwatumikia wananchi; lakini hii ni moja kati ya kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi. Kadhalika nimpongeze Mheshimiwa Rais Dkt. Hussein Ali Mwinyi naye kwa kazi kubwa anayoifanya ya kutekeleza miradi mikubwa ya maendeleo kwa upande wa Zanzibar.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze mchango wangu kuhusiana na hotuba hii ya Waziri Mkuu kwa kuanza na TASAF. Kwanza nishukuru Serikali kwa kazi kubwa iliyofanya katika jimbo langu la kuniletea shilingi milioni 475 kwa ujenzi wa kituo kikubwa cha daraja la pili, kitu ambacho kitawasaidia wananchi wa Jimbo la Kiwani pamoja na jimbo jirani. Kituo hiki kilipata baraka kubwa kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu kuweka jiwe la msingi lakini na Mheshimiwa Makamo wa Rais Dkt. Mpango kwenda kukifungua. Hata hivyo, changamoto kubwa ya kituo hiki kwa sasa ambayo wananchi tunakabiliana nacho ni vifaa tiba, wakati Makamo wa Rais anafungua kituo kile aliagiza kwamba vifaa tiba kwenye kituo kile vipatikane ili lile lengo la Serikali la kujenga kituo kile na wananchi kupata huduma liweze kupatikana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwombe Waziri ambaye anahusika, kwamba sasa hivi vitu ambavyo tunahitaji pale kituoni ni ultra sound X-ray pamoja na kile kiti cha meno, tukianza hivyo vitu kile kituo kitafanya kazi na wananchi wataweza kunufaika na kile kituo na zile ahadi ambazo tuliziweka za kuimarisha huduma za afya tutakuwa tumeweza kuzitekeleza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande huo huo wa TASAF nishukuru huu mpango wa ajira za muda ambao ni programu maalum iliyotekelezwa na TASAF ya kuwapatia wananchi wetu ajira za muda lakini sambamba na kutengeneza miundo mbinu ya barabara kwa kiwango cha udongo. Hata hivyo hapa napo kuna changamoto ndogo ambayo napenda TASAF kwa mara nyingine waweze kuongeza bajeti ili zile kazi ziweze kufanikiwa na kuleta ufanisi wa hali ya juu na zile fedha ambazo zimetumika kwa kuwalipa wananchi ziweze kufanya kazi inavyopaswa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikija kwa upande wa mazingira pia nishukuru Serikali hii ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutupatia mradi mmoja mkubwa sana wa shilingi zaidi ya bilioni moja na nusu za ujenzi wa tuta la kuzuia maji ya chumvi katika jimbo langu na jimbo jirani la Mtambile.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii kazi ni kubwa na kazi hii kwa kweli lazima tushukuru kwamba imewasaidia sana wananchi na wanafunzi ambao walikuwa wanatumia kivuko cha maji, lakini sasa tunapata daraja hili la kuzuia maji lakini kadhalika tunapata njia za kutumia. Nishukuru kwa kuleta fedha hizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa Wizara wa Mambo ya Ndani, nishukuru kwamba tumepiga kelele hapa na nimshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri alifanya ziara kwenye Kituo cha Polisi Kengeja na juzi katika kujibu swali hapa alituahidi kwamba tayari wameshatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa kituo kile. Haya yatakuwa ni mapinduzi makubwa kwenye kituo kile ambacho kilijengwa tangu enzi za wakoloni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nije katika suala la zima hili la habari ushoga. Suala hili ilikuwa niseme kwamba, mpango ule wa akinamama wajawazito kuwa ni lazima kupimwa ni mpango mzuri na umeleta matokeo mazuri sana na mafanikio makubwa yamepatikana. Ninachoomba sasa, sisi tunapiga kelele sana juu ya jambo hili, lakini ninachosema kama kuna taratibu za sheria, kanuni kwamba Bunge liamue sasa kwanza Wabunge wote wapimwe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakipimwa hawa Wabunge tutaweza kujua kwamba Wabunge sasa tunatoka tunakwenda kufanya kazi hii ya kuhakikisha tunawalinda wananchi wetu baada ya sisi kuwa tumeshatangulia kupimwa. Sasa kama humu wamo, tunajua kwamba wale watu wa unga kulikuwa kuna Sober house wanaweka na kama humu ndani watakuwa wamo Wasenge na Wasagaji, nao sasa iwepo namna ya kuhakikisha kwamba tunawaweka kwenye Sober house. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi/Kicheko)