Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana nashukuru kwa kuniona pia niweze kumshukuru sana Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema aliyeweza kunisimamisha hapa niweze kuongea na kuchangia Hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze sana Waziri Mkuu kwa hotuba yake nzuri yenye mashiko ambayo mengi yamesemwa mule ndani na mengi yanaonekana yakifanyika kwa yale machache basi ninaamini kama Bunge tutaweza kuyafanyia kazi yaweze kuendelea kufanya kazi zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze sana Mheshimiwa wangu Mama Samia kwa kazi nzuri ambayo ameifanya na anaendelea kuifanya, amekuwa ni mama bora na amekuwa ni mama ambaye hakika mimi amenikosha sana kuifanya demokrasia sasa inafanya kazi nzuri kwa ajili ya mustakabali mzima wa nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mama Samia ameweza kuleta fedha nyingi sana kwenye Jimbo letu la Temeke naweza kusema kwamba ni mabilioni nikianza kutaja moja moja hapa; kwa kweli ninasema inawezekana ni upendeleo mkubwa kwa sababu ni jimbo la mama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile tumeweza kujenga mambo mengi, shule za sekondari na kama siku zote tunavyolalamika kwamba tuna watoto wengi kwenye jimbo letu lakini sasa hivi hakuna mtoto anayebaki kuanza shule darasa la kwanza au shule ya awali. Kwa hiyo, ninampongeza sana Mheshimiwa Rais kwa kazi nzuri hii ambayo anaendelea kuifanya na ninaamini bado ataendelea kuifanya kwa miaka inayokuja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niende sasa katika Jimbo langu la Temeke. Jimbo langu la Temeke hasa upande wa eneo la Kurasini. Kurasini imekuwa kama ni eneo ambalo la uwekezaji lakini yapo mambo ambayo kidogo hayafurahishi. Tumekuwa na eneo lile DAWASA ambalo wanakwenda kumwaga maji taka, watu wako pale ambao eneo lile sasa hivi limekuwa kwa kweli ni kero kwa eneo letu la Jimbo la Temeke hasa upande wa Kurasini. Wameweza kulipa fidia kidogo sana na watu bado hawajaondoka kwa sababu hawajamaliziwa fidia zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niombe sana Serikali waliangalie hili tena upya. DAWASA naamini wanalifahamu vizuri na walishapelekana mpaka mahakamani lakini

walivyoambiwa kwamba wamalizie wale watu mpaka sasa hawajaweza kumaliza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini sio eneo hilo tu Kurasini kama ninavyosema katika Jimbo letu la Temeke ni eneo la uwekezaji. Wako hawa ndugu zetu wa eneo la EPZ wana eneo kubwa sana ambalo sasa hivi limekaa wazi halifanyiwi kazi. Lakini wako wananchi waliopewa fedha ambazo kuanzia mwaka 2015 wamelipwa mpaka sasa 2023 bado mapunjo yao hayajakuwa sawasawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niombe Serikali yangu Serikali sikivu waangalie sasa wananchi hawa kwenye mapunjo haya waweze kufidiwa ili waweze kuondoka katika maeneo hayo hasa lile eneo la DAWASA kwa sababu ni kero, kwa sababu hata DAWASA wenyewe sasa hivi hawalitengenezi hawalifanyii kazi yoyote nzuri ili wananchi wale waweze kukaa mahali salama. Kwa hiyo, niombe sasa Serikali iweze kuwalipa waweze kuondoka kwa kadri ambavyo afya zao siyo nzuri kwa sasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu kwamba yapo maeneo mengine ambayo tunatamani sisi kama Jimbo la Temeke tuweze kupatiwa hasa lile eneo la EPZ hawajalifanyia kazi mpaka sasa, sisi wenyewe tunalitamani kama Jimbo la Temeke au Halmashauri yetu ya Temeke tuweze kufanyia kazi. Zaidi ya hayo niombe basi Serikali kama inaweza kuifanyia kazi kwa mapema kuweka uwekezaji pale ninaamini vijana wetu wa Jimbo la Temeke na hasa halmashauri yetu watapata ajira kuliko linavyokaa wazi hivi bila kufanyiwa kazi yoyote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho kabisa niombe Waziri wa Maji pamoja na Waziri wa Ardhi tuweze kwenda pamoja jimboni tukawasikilize wananchi hawa jinsi gani wanavyolalamika ili tutoe msimamo sasa au Serikali itoe namna gani ya kuweza kuwaondoa wale watu pale kwa fedha ambazo zimebaki ili wananchi wale waende kukaa sehemu zingine nae neo lile Serikali iweze kuendelea kwa mustakabali wanaoweza kuufanyia kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu kwamba wananchi wangu wa Jimbo la Temeke wamenituma nimwambie Mheshimiwa Rais tumeweza kuomba na maombi haya tunaomba sana sana Wananchi wa Temeke Mungu azidi kumpa hekima, maono, mafunuo ili aweze kuendelea kuiongoza nchi yetu kwa jinsi anavyoendelea kuiongoza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho niombe pia kwamba Jimbo letu la Temeke na Wananchi wangu wa Temeke wamenituma na kusema sisi kama wana Temeke tunalaani vitendo vya ubakaji, ushoga, usagaji na mambo mengine yote yanayofanana na hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo naunga mkono hoja nashukuru sana. (Makofi)