Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Dr. Alice Karungi Kaijage

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahante sana, na mimi namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia afya, lakini pia naungana na wenzangu kumpongeza Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayofanya ya kulitumikia Taifa letu la Tanzania. Pia nampongeza Waziri Mkuu pamoja na timu ya mawaziri katika Sekta ile pamoja na watendaji kwa kazi nzuri wanayofanya kwa Taifa letu la Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nachangia fungu 65, ilani ya Chama Cha Mapinduzi Ibara ya 168 imeendelea kutambua mchango muhimu sana wa wafanya kazi na vyama vya wafanyakazi na waajiri kwenye uchumi wa nchi yetu. Si hivyo tu, hata kwenye hotuba ya Waziri Mkuu ukurasa wa 65 pia imeeleza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini nasema hayo, haina ubishi kabisa kwamba vyama vya wafanyakazi ndivyo vinavyohusika kuwaunganisha na kuleta harmony kati ya waajiri na wafanya kazi. Kupitia mabaraza yao wanajadili mambo mbalimbali ambayo yanawagusa na ambayo yanawasumbua sana wafanyakazi; lakini pia ndiyo forum sahihi. Hatutegemei wafanyakazi wakose vikao waende kwenye waandishi wa habari na kwenye platforms za siasa zinaendelea sasa hivi kueleza mambo yao; wana mabaraza yao kamili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini nazungumzia hayo? Fungu 65 ndipo mahala sahihi kuhusiana na mambo ya vyama vya wafanyakazi na wafanyakazi. Nashauri, watakapokuja watueleze, kwenye Fungu 65 mpaka sasa, kitengo cha wafanyakazi na vyama vya wafanyakazi kumefanyika nini na bajeti ijayo wanampango gani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema kwa sababu idara ina Idara ya Msajili wa Vyama vya Wafanyakazi ambaye ndiye anayehusika kwenda kufuatilia masuala mbalimbali na utendaji wa vyama vya wafanyakazi kule pembezoni mikoani ambako kuna matawi ya wafanyakazi. Kwamba wanaendeshaje mambo yao kutokana na utaratibu na kanuni walizojiwekea. Kama Idara hii ya Msajiri wa Vyama vya Wafanyakazi itakuwa haina baketi itakwendaje kufanya shughuli hizo? Lazima tusikilize matataizo yao na tumuwezeshe Msajiri aende akafuatilie kwenye mikoa na pembezoni, kule ambako kuna matawi ya vyama vya wafanyakazi, akaangalie wanavyofanya kazi zao kulingana na taratibu walizojiwekea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala la wakala wa huduma za ajira nchini (TaESA). Hili baraza linahusika na kuwaunganisha watafuta kazi na waajiri. Nipongeze sana Serikali, sasa hivi kupitia ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi na Utawala Bora imeshirikiana sasa hivi na Ofisi ya Waziri Mkuu kuanzisha Mfumo wa Taifa wa Kusimamia Ajira. Hii itasaidia kwa sababu mfumo huu utakuwa na taarifa za nafasi za kazi zote nchini na utakuwa na takwimu kamili za soko la ajira nchini. Kwa hivyo nipongeze Serikali kujua kwamba kuna umuhimu wa wao kuungana na Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi. Katika muunganiko huo TaESA inahusika na suala la usimamizi wa kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu ukoje hapo? Kwamba hii TaESA ijulikane, TaESA iongezewe nguvu. Kama alivyosema mjumbe mwenzangu, kwenye Skill Development Leavy kwenye SDL iongezewe bajeti. Hii TaESA inahusika kutafuta ajira, inahusika kuwapeleka vijana kwenye mazoezi ya vitendo, lakini bajeti yake ni ndogo na pia haijulikani na haitoki. Watoto hawaifahamu na hata wazazi hawaifahamu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nipongeze kwamba sasa kuna ushirikiano kati ya ofisi ya utumishi na ajira lakini sasa TaESA Ifanye kazi iende ikatafute hizi nafasi, iende mikoani,
kwenye viwanda ikae na waajiri, itapata hizi nafasi kwa hiyo itasaidia kupata nafasi kwa ajili ya wananchi wetu.

Kuna Baraza la Uchumi, na hili baraza liko kwa mujibu wa Sheria. Tunabaraza lingine kwenye hii ofisi linaitwa LESCO, hili linaitwa Baraza la Uchumi na Jamii. Baraza hili linaishauri Serikali kupitia Ofisi ya Waziri wa Kazi, inamshauri Waziri wa Kazi juu ya mambo mablimbali ikiwepo Sera ya Taifa ya Soko la Ajira, njia tofauti mbalimbali za kupunguza ukosefu wa ajira pamoja na pia kutoa takwimu za usimamizi wa sheria ya ajira nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mabaraza yote yapo kwenye ofisi, hatusikii kazi zake hatuoni ripoti yake tunakazana kutafuta ajira za vijana. Kama kuna mabaraza yapo kwa mujibu wa sheria yawezeshwe; kama ni bajeti ya ESDL iongezwe ili haya mabaraza kwa kusaidiana na juhudi mbalimbali za Rais mpaka analeta mashamba vijana walime basi hayo mabaraza yawe active, yaongezewe bajeti yatoke yajulikane yafanye kazi inayotakiwa kufanywa. Wanapokuja watuambie hayo mabaraza yamefanya nini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hayo nipongeze Serikali kwa kuja na ongezeko la Mshahara wa kima cha chini hasa kwa sekta binafsi. Sensa ya mwaka jana imeonesha kabisa kuwa sekta binafsi ndiyo inayoongeza kuwa na watumishi wengi sana. Sheria ya Kazi inaonesha kwamba Bodi ya Ajira Sekta Binafsi inatakiwa iongezewe bajeti ili tunapopandisha safari hii iwe ndio mwanzo wa mchakato kwa sababu upandishaji wa kima cha chini umechelewa sana. Iwezeshwe, ianze mchakato mapema kwa sababu maisha kila mwaka yanabadilika, kwa hiyo ni lazima kima cha chini kipande kila mwaka. Kwa hiyo Bodi hii iwezeshwe, iongezewe bajeti ili ianze mapema mchakato wa kufatilia kima cha chini hasa cha watu wa sekta binafsi ndio wengi katika utumishi wa Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada hayo nasema naunga mkono hoja ahsante. (Makofi)