Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Ahmed Juma Ngwali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ziwani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. AHMED JUMA NGWALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru, na nikuombe tu niende moja kwa moja kwenye hoja. Na hoja yangu itahusiana na maadili (LGBTQ).

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania tuna Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora. Chombo hiki ni cha Kikatiba. Kimeanzishwa na kimetajwa katika Katiba, Ibara ya 131(1)(2).

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kusikitisha kabisa ni kuona kwamba chombo hiki ambacho ndicho chenye haki ya kutupa taarifa za uhakika kimedharauliwa, hakifanyi kazi, kimekaa tu kinatoa taarifa ambazo zinamalizia huko. Kwa mujibu wa Katiba, naomba ninukuu, Ibara ya 131(3)(b) inasema;

(3) Kila mwaka wa fedha Tume itatayarisha na kuwasilisha kwa Waziri anayesimamia haki za binadamu taarifa kuhusu-

(a) shughuli za Tume katika mwaka uliotangulia;

(b) hali ya utekelezaji wa hifadhi ya haki za binadamu katika Jamhuri ya Muungano,

Na Waziri atawasilisha mbele ya Bunge kila taarifa iliyowasilishwa kwake na Tume mapema iwezekanavyo baada ya kuipokea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tangu 2011 taarifa haijawasilishwa na sijui kama inafika kwa Waziri. Tume inatoa taarifa lakini taarifa ile inakaliwa, haiji. Maana yake ni nini? Maana yake ni kwamba hali iliyokuwepo Tanzania kuhusu haki za binadamu ni mbaya kuliko tunavyofikiria lakini hatupati taarifa. Eti leo tunategemea taarifa kutoka kwa NGO tunategemea taarifa kutoka kwa mtu atuelezee habari ya human right katika nchi yetu? Haiwezekani. Sasa, kama hatuitaki Tume basi tuifute. Tume haina wafanyakazi, haina
bajeti, bajeti yake ndogo sana, haiwezi kufanya chochote, na tumeianzisha kikatiba kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii kwanza ni kuvunja Katiba lakini pia kuvunja katiba ibara ya 18(2) kwa Tume kushindwa kutoa taarifa zinazoendelea kwa wananchi. Kwa wale wenye watoto nje ya nchi Amerika au Ulaya au Asia, kumlea mtoto nje ya nchi siku hizi ni bora na ni salama zaidi kuliko kumlea katika nchi yetu ya Tanzania. Hii ni kwa sababu watoto wa nje ya nchi wanaharibika, Ulaya na Amerika, sisi watoto tunawaharibu. Style ya maisha yetu ya kuishi, tutaishi na jamaa ndani ya nyumba huyu mjomba, kaka, shangazi, sijui nani, wale ndio wanaoharibu Watoto. Tume inaripoti kuhusu jambo hili na hizi ripoti hazitolewi kwa sababu wazee wenyewe wanaficha ripoti kwa sababu wanaona aibu, lakini hali ni mbaya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, halafu inashangaza, zamani ilikuwa kumtwaza mwanamke taabu sana, mpaka uandike barua, mwalimu aikamate, taabu sana. Siku hizi unapeleka simu unawekewa namba lakini zamani vitendo hivyo vilikuwa hakuna, leo vitendo hivyo vinatokea wapi? Na bado tume tumeitelekeza; hili sio jambo jema. Niombe Serikali kwamba, kwa hali ilivyo mbaya ni bora tuache taarifa ya CAG tusome taarifa ya Tume.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili niseme kuhusu Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali. Tumeanzisha hiyo Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali lakini ipo chini ya Wizara. Tunashukuru Serikali imepeleka fedha kule kiwanda cha Dodoma, bilioni nane, vilevile tumepeleka kama bilioni sita kwa ajili ya kununua mashine. Sasa hawa watu lazima wawe wakala, lazima wajitegemee. Huwezi ukapeleka pesa ukaanzisha hiyo biashara halafu wakategemea OC kipuri kikiharibika wasubiri miezi mitatu wamemuandikia Katibu mkuu. Nafikiri tuuharakishe mchakato unaoendelea ili kumfanya huyu Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali awe wakala, na pia tumpe mapato na watumishi ambao wanaweza kufanya hiyo kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, inasikitisha sana; wakati wa ziara ya Kamati tulivyokuwa tukienda kukagua miradi. Jengo la Msajiri wa Vyama vya Siasa ambaye anasajiri chama cha kisiasa kimoja kwa miaka mitano linajengwa kwa bilioni 20. Kwa hiyo jengo linajengwa kwa bilioni 20, kwani bilioni mbili haiwezi kujenga jengo? kwani bilioni tano hawezi? Jengo la TAKUKURU ni bilioni 24; tunaharibu fedha za Serikali badala ya kuziweka katika mambo ya maana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kiwanda kile ambacho ni cha Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali kinatumia bilioni nane tu, na mashine yake ni bilioni sita tu lakini ita-generate fund kwa bilioni 20 kwa mwaka. Lakini pia kama tutakiwezesha vizurini zaidi ya bilioni 40 hapo itafanya asilimia 55, lakini leo unachukua fedha unazipeleka kwa mtu anakaa na kiyoyozi anasajiri chama cha siasa, sijui anafanya nini, haiwezekani. Hatuwezi kutumia hivyo fedha za Serikali, fedha za Serikali lazima zitumiwe kwa utaratibu, kwa utaratibu huo hauelekei kama sisi ni nchi maskini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna majengo hapa yamejengwa kwa bilioni 100, tunayajua sasa haiwezekani. ingekuwa jengo hilo linajengwa ndani yake lina biashara hiyo sawa, lakini halifanyi biashara, jengo limekaa tu halafu nani ataliendesha? Halafu sie tupitishe bajeti hapa tukaliendeshe tena hilo jengo la bilioni 20 pamoja na maintenance yake, tupitishe hapa likafanye kazi? Haiwezekani hizo fedha sisi tuna haribu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.