Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi mchana huu ili kuchangia hoja ya hotuba ya Waziri Mkuu. Kwanza naunga mkono kwa asilimia 100.

Pili, naomba nimshukuru Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kazi kubwa aliyoifanya kwenye maeneo ya Jimbo la Tunduru Kusini na Tunduru kwa ujumla kwa miradi ya afya, elimu pamoja na miundombinu ambayo imerahisisha maisha ya Watanzania kwa maana ya wakazi wa Tunduru Kusini.

Mheshimiwa Spika, pamoja na shukrani hizo nitaongea mambo matatu. Jambo la kwanza ni suala la kilimo. Jambo la pili suala la elimu na jambo la tatu ni miundombinu ya barabara.

Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru Rais wetu kwa kutupatia mahindi ya bei nafuu kwa Wilaya ya Tunduru. Baada ya maombi yetu kupelekwa kwenye RCC tunashukuru tulipata mahindi na yamesambazwa kwa kiasi kikubwa katika eneo letu ila tunaomba nafasi hii kwa safari ijayo uweke utaratibu tofauti ulivyofanywa sasa.

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa katiba Ibara ya 35 inasema bayana kwamba shughuli zote za utendaji wa Serikali ya Jamuhuri ya Muungano zitatekelezwa na Utumishi wa Serikali kwa niaba ya Rais, na kwamba utaratibu wa masharti ya kutoa fedha za Seriakli, pengine kutoka hata Mfuko Mkuu wa Hazina unabainishwa katika Ibara ya 136, Ibara ya 137 na hata Ibara ya 40 inabainisha pale ambapo Rais ametajwa kwamba anaweza kushughulikia mambo haya ya fedha lakini ni Rais au Waziri aliyemteua.

Mheshimiwa Spika, sasa tunaposema kwamba malipo haya yanapaswa au yanapitiwa na Rais ili yaweze kulipwa, ili hali Rais mwenyewe juzi amesimama na kutoa malalamiko yake jinsi ambavyo hakuridhishwa baadhi ya wakandarasi wanapokuwa wanarundikiwa, wanacheleweshwa kulipwa na kusababisha riba zaidi ya shilingi bilioni 400.

Mheshimiwa Spika, sasa ninajiuliza kama ingekuwa Rais ndio anaidhinisha malipo haya na sio wale ambao amewakasimu madaraka kwa mujibu wa katiba, leo uzembe unapotokea na ufisadi unaotokea kwa tafsiri ya maelezo ya Waziri, ninavyoyaona maana yake yote yana idhini ya Rais jambo ambalo si kweli hata kidogo, vinginevyo ufisadi huu, tusingekuwa tunawa-attack wale ambao ni maafisa masuhuli na mlipaji mkuu wa Serikali ambaye tunamsimamia na Waziri mwenye dhamana ya fedha.

Mheshimiwa Spika, je, ni sahihi kutumika kwa jina la Rais katika mazingira hayo kama ambavyo kanuni ya 71(9) inavyoeleza. Nilikuwa najaribu kuliona jambo hili linapeleka taswira ambayo sio njema kwamba Rais lazima aidhinishe fedha hizo ndipo ziweze kulipwa katika kipindi hiki ambacho wimbi la ufisadi limeweza kubainishwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali.

Mheshimiwa Spika, nilikuwa naomba mwongozo wako kama ni sahihi kutumika kwa maneno aliyoyatumia Waziri katika eneo hilo. Wakati Wabunge wanaeleza masikitiko ya baadhi ya malipo ambayo hayajakaa vizuri, ahsante.