Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuimarisha demokrasia nchini na kukuza diplomasia ya uchumi

Hon. Salome Wycliffe Makamba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Bunge la kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuimarisha demokrasia nchini na kukuza diplomasia ya uchumi

MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Nami niungane na hoja ya Mheshimiwa Mbunge ya kumpongeza Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuimarisha demokrasia na sera ya mambo ya nje kwa maana ya foreign policy.

Mheshimiwa Spika, nianze kwa kusema kwamba nafikiri hatumuelewi vizuri Mheshimiwa Rais ukiniambia niseme kwa neno moja nitasema Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni Balozi wa nchi za Afrika. Nitoe mfano mdogo, pamoja na mambo mengi aliyoyafanya, juzi alizungumzia kuhusiana na sheria iliyotungwa huko Marekani inayozipa nchi za Afrika fursa ya kupeleka bidhaa, huduma na utaalam kwenye nchi ya Marekani, hiyo sheria ilipitishwa mwaka 2000 na haijawahi kutekelezwa kwa miaka 23 sasa, lakini juzi Makamu wa Rais wa Marekani alipokuja Tanzania pamoja na kutembelea nchi zote Mheshimiwa Rais aliamua kusimama kwa Afrika, akaomba nchi za Afrika mkataba ule utekelezwe, pamoja na hilo pia aliomba Visa ya Watanzania kwenda Marekani iongezwe muda isiwe na ukomo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, maana ya Mheshimiwa Rais kuifungua Afrika au kuifungua Tanzania kwenye nchi za ulimwengu wa Kwanza ni kwamba Watanzania tuweze kwenda kupeleka bidhaa zetu kwenye nchi za ulimwengu wa Kwanza ikiwemo Marekani. Tupeleke utaalam wetu, tupeleke Wakandarasi wetu wakafanye kazi kule kama ambayo Wakandarasi na bidhaa za kule zinakuja Afrika.

Mheshimiwa Spika, sasa ili hayo mambo yaweze kutekelezeka kwa vitendo ni lazima tumsaidie Mheshimiwa Rais kuwaandaa watu wetu, kuandaa vyombo vyetu, kuandaa mazao yetu raw materials zote ziweze kupelekwa kwenye maeneo hayo. Sasa ili hayo yafanyike ni lazima Bunge na Serikali tushirikiane katika kuhakikisha taratibu, sheria, kanuni, mienendo na mfumo wa nchi unaweza kuwandaa Watanzania kukimbilia fursa hizo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hivi tunawezaje kupeleka wataalam wa kitanzania ambao wanaweza kwenda kufanyakazi kwenye nchi za ulimwengu wa kwanza, kama tangu Bunge hili mimi ninakaribia miaka Nane kwenye Bunge hili, tumeomba tubadilishe mitaala ili wanafunzi wetu waweze kwenda kufanya kazi katika nchi za nje mpaka leo mitaala haijabadilishwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niliwahi kutoka agizo ndani ya Bunge hili tukufu kwamba vitabu vya kiingereza vyote vibadilishwe viwe vya Kiswahili, agizo hili lilitimizwa ndani ya miezi mitatu tu leo tuna miaka miwili ya Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mtaala wa Elimu wa Tanzania haujabadilika.

Mheshimiwa Spika, tunawezaje?

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO: Mheshimiwa Spika, Taarifa.

SPIKA: Mheshimiwa Salome Makamba kuna taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Husna Sekiboko.

T A A R I F A

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO: Mheshimiwa Spika, naomba kumpa taarifa Mheshimiwa Salome Makamba kwamba agizo la Mheshimiwa Rais la kuboresha mitaala limeshafanyika na hivi juzi Wizara ya Elimu imeipitisha Kamati kwenye mabadiliko hayo na muda siyo mrefu hata Bunge litapata fursa ya kuweza kupitishwa kwenye mabadiliko hayo, na kwa taarifa tu ni kwamba maboresho yaliyofanyika ni makubwa yenye tija kubwa kwa nchi yetu, tusubiri muda ufike tuyapitishe ili tuweze kunufaika na mabadiliko hayo.

Mheshimiwa Spika, nashukuru sana.

SPIKA: Mheshimiwa Salome Makamba unaipokea Taarifa hiyo?

MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Spika, taarifa hiyo siipokei, habari ya kusema hivi karibuni, Bungeni humu taarifa bado haijaingia kwa hiyo ninavyozungumza hivi sasa
ni kwamba Bunge halijapitisha mtaala mpya wa Serikali unaohusiana na elimu, bado hatujapitisha hilo ni moja.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili, tumejadili hapa kuhusiana na namna ya kutengeneza mazingira rafiki ya uwekezaji, tulipitisha habari ya blueprint economy, kwamba tuwe na one stop center kwa ajili ya kumsaidia Mwekezaji anapokuja Tanzania asihangaike kukimbia huku na kule, lilikuwa Azimio la Bunge Serikali mpaka leo hakuna yaliyotekelezwa.

Mheshimiwa Spika, tulipitisha kuhusiana na mabadiliko ya Sheria ya Habari ili tupate uhuru wa Vyombo vya Habari, sheria imeletwa vipande vipande, zote za Habari bado zinamapungufu jambo ambalo linatutia doa! Mmesema tuwaoneshe watu mlango wa kupitia hiyo ndiyo milango sasa nawaonyesha. (Kicheko)

Mheshimiwa Spika, Waziri wa Fedha...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)