Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuimarisha demokrasia nchini na kukuza diplomasia ya uchumi

Hon. Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuimarisha demokrasia nchini na kukuza diplomasia ya uchumi

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa fursa ili na mimi niweze kuchangia azimio hili, na kabla sijaongea niseme moja kwa moja kwamba naunga mkono azimio hili. Ni azimio ambalo limekuja kwa wakati na ni azimio ambalo limebeba uhalisia.

Mheshimiwa Spika, sisi kwa upande wa Wizara ya Fedha tunavitu vingi vya kusema ambavyo vimeshajitokeza katika kipindi cha miaka miwili ambavyo vina beba uzito wa azimio hili. Hivi tunavyoongea katika bajeti hii tunayoitekeleza kwa jitihada za Mheshimiwa Rais za kukuza Demokrasia pamoja na Diplomasia ya Uchumi Kwenye bajeti yetu tulipata dola 500, sawa na trilioni 1.2 katika mwaka wa fedha huu ambao tunaendelea kutekeleza; na hii ni kupitia dirisha la Development Policy Operation, DPO ambayo inatolewa na World Bank. Dirisha hili lilikuwa limefungwa kwa miaka Takribani saba, Tanzania ilikuwa imetolewa katika dirisha hili kwa sababu vigezo vyake vinapatikana kwa good governance, transparency na kwa juhudi za kupambana na masuala ya rushwa. Sasa hivi tuko kwenye programme hiyo ambayo jumla yake ni dola bilioni moja. Milioni 500 zimeingia katika mwaka huu wa fedha na milioni 500 zinaingia katika mwaka wa fedha unaokuja. Kwa hiyo hii ni jambo ambalo tayari limeshafanyika na dirisha ambalo lilikuwa limefungwa.

Mheshimiwa Spika, lakini sio hilo tu tuko kwenye programme mbili na IMF, mojawapo tulifanya ile ya RCF lakini ya pili tumefanya ile ya ECF ambayo ni takribani dola bilioni 1.1. Kwa mwaka wa fedha huu tayari tumeshapata dola milioni 152 quarter ya kwanza na quarter hii kabla ya mwisho wa mwaka huu wa fedha tunaoendelea nao tutapata dola milioni 152 nyingine. Fedha hizi ni za recovery programme ndizo ambazo zinaenda kwenye kilimo, umwagiliaji, modernization kwenye mifugo na kwenye uvuvi, hili ni jambo ambalo limeshafanyika na ni programme ya takribani miezi 40. Kwa hiyo tutaendelea na programme hii ambayo ni ya recovery na zinakwenda kwenye sekta za uzalishaji. Na hii inapewa nchi ambayo inakidhi vigezo. Na vigezo vyenyewe vinahusiana na good governance pamoja na matumizi bora ya rasilimali.

Mheshimiwa Spika, kuna hatua zingine ambazo ni kubwa ambazo tunaziendea ambazo mataifa makubwa yamefanya. Moja, tuko kwenye hatua za mwisho za credit rating, tumeshaonana na magwiji wa kufanya credit rating kwenye mataifa, walikuja Mood’s na wengine tumemaliza nao wiki iliyopita. Credit rating inafanyika kwa Taifa ambalo linakidhi vigezo na vigezo vyenyewe ni vya demokrasia pamoja na good governance, na diplomasia ya kiuchumi ambayo hiyo Mheshimiwa Rais amefanya na kwenye ukanda wetu huu Tanzania ndiyo ilikuwa na score kubwa.

Mheshimiwa Spika, tunatarajia watakapotoa report tutakuwa tumepanda juu zaidi, na hii inafanyika na tayari tumeshamaliza tunajua tu report itatoka hivi karibuni. Lakini si hilo tuna lingine ambalo tuko hatua za mwisho ni kuweza kupata fedha za Climate Change RST. Si hilo tu tunatarajia tupate accreditation ya institution zetu. Hivi tunavyoenda accreditation ilikuwa kwenye baadhi ya sekta binafsi lakini sasa hivi tuko hatua za mwisho ili ofisi ya Rais TAMISEMI ipate accreditation na Wizara ya Fedha ipate accreditation,tutaweza kupata fedha ambazo zinatumika katika kupambana na mabadiliko ya tabia ya nchi na kuweka ustahimilivu wa uchumi pamoja na kuweka sawa kwenye masuala ya balance of payment.

Mheshimiwa Spika, lakini si hivyo tu tuko kwenye hatua za mwisho pia kuangalia na kukamilisha urejeshwaji wa MCC. MCC na yenyewe ilikuwa programme ambayo ilikuwa inatekelezwa na imesaidia sana katika kutekeleza miradi ya maendeleo. Tuko hatua za mwisho naamini walivyotoa report iliyopita walitumia vigezo vya zamani, tunaamini sasa hivi wakirejea hivyo vigezo ambavyo tunaamini kila mwaka wanakuwa wanatoa hivyo vigezo, tunaamini Tanzania itakuwa imeshafuzu, na hii ni kwa sababu ya hatua kubwa ambazo zimeshafanyika. Vigezo vyenyewe ni vya mikutano ya hadhara ilisharuhusiwa, masuala ya uhuru wa habari ilisharuhusiwa, masuala ya data protection ilisharuhusiwa, protection of investment tulishafanya hivyo vitu.

Mheshimiwa Spika, sio hayo tu ni pamoja na masuala ya kupambana na matumizi bora ya rasilimali. Kuweka misingi bora ya matumizi ya rasilimali. Mheshimiwa Rais amepiga hatua kubwa, Mwaka jana tumeongeza fedha kwa CAG tumeongeza afanye late time audit. Tumeweka fedha kwa Mkaguzi Mkuu wa Ndani. Haya yote ambayo mnaweza mkaona ni kwa sababu ya Mheshimiwa Rais kuweka meno kwa CAG lakini pia na kuweka rasilimali kwa ajili ya ufatiliaji na ukaguzi ambao ndio unatoa majibu na kuweza kusaidia Bunge. Kwa hiyo, haya yote yanayofanywa yanaweka uzito kwamba tunatakiwa tumpongeze Mheshimiwa Rais, tumuunge mkono na kila mtu atimize wajibu wake. Sasa dada yangu, namshukuru Mheshimiwa Chumi amemjibu vizuri alipokuwa anasema kwamba watu wanauliza hii ilifikaje ilifikaje, hayo maswali ni ya kila mtu.

Mheshimiwa Spika, tumefika hapa baada ya Mheshimiwa Rais kwenda kwenye maridhiano na akaweka 4R hizo zote ni za kuweka misingi ya platform kwenye uwanja. Uwanja ukiwa rough lazima opponents awe tough, wewe unategemea watu wawe rough rough halafu umepewa jukumu la nchi uachie? Hamna nchi inayoweza ikaenda hivyo. Kwa hiyo, kwa kuwa Mheshimiwa Rais amekaa na pande zote, tukakubaliana tuendeshe vipi mambo ya nchi hii, hicho ndicho ambacho na CCM inaunga mkono kwa sababu CCM ndio kiongozi wa ustaarabu wa kuendesha nchi hii, ndio maana tangu uhuru mpaka sasa nchi hii haijawahi kupata dosari yoyote ya kukiuka masuala ya haki za binadamu wala hata yale ambayo yanasimuliwa kwenye hizo nchi nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tumuunge mkono Mheshimiwa Rais na ameongea vizuri nadhani Mheshimiwa Ole-sendeka ama Mheshimiwa Mwakasaka kwamba haya tunayoyaweka na haya ambayo tunayokubaliana tuyaheshimu na twende nayo na hiyo ndiyo itakayokuwa dira na hiyo ndiyo itakayotupa sustainability. Maana yake aliuza kwamba kwa hiyo sasa baadaye itakuwaje? Baadaye itakuwa hivi hivi, tuyaheshimu tu haya ambayo tunakubaliana. Hiyo ndiyo misingi ya demokrasia na hiyo ndiyo misingi ya utawala bora na hiyo ndiyo misingi bora ya uendeshaji wa nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hata hivyo tukishaweka mifumo ikafanya kazi tutakuwa tumejihakikishia masuala ya uendeshaji wa nchi yetu na hivi tuko kwenye utengenezaji wa dira mpya na nawahakikishia kwa haya ambayo Mheshimiwa Rais anayajengea sasa hivi, tuna uhakika dira mpya itakapopinduka kwamba tumeshamaliza miaka mingine hiyo ambayo itakuwa ya utekelezaji wa dira, nchi yetu itakuwa imekwishaenda kwenye nchi zilizoendelea na Watanzania watapata manufaa makubwa ya kubadilisha maisha yao na haya ni mambo ambayo Mheshimiwa Rais anayapigania.

Mheshimiwa Spika, nimpongeze Engineer Chilewesa aliyeleta Azimio hili na Mheshimiwa Mbunge tunaliunga mkono mia kwa mia na tunamtakia kila la heri Mheshimiwa Rais katika kuendeleza haya mambo mazuri. Mengine tutaendelea kuyasema katika bajeti za kisekta na mengine tutayasema katika Bajeti Kuu ya Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja. (Makofi)