Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuimarisha demokrasia nchini na kukuza diplomasia ya uchumi

Hon. Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Bunge la kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuimarisha demokrasia nchini na kukuza diplomasia ya uchumi

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kunipa nafasi niweze kuchangia Azimio hili la Bunge. Nianze kwanza kwa kumpongeza Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuwa miongoni mwa Marais wachache sana hapa duniani wanaoheshimu Katiba. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Katiba ya nchi yoyote ile huwa inakuwa na mapungufu yake. Na katika mapungufu hayo kwa kwaida wengi wa viongozi huwa wanaziogopa Katiba zao, lakini mama ameweza kuwa shujaa wa sasa kuruhusu hata mikutano ya vyama vingi, sio kitu rahisi kabisa, kukaa kiti kimoja na mtu ambaye ni hasimu wako huwa ni kitu kigumu sana. Tunaona hata katika michezo Yanga na Simba tu ni michezo ya kawaida, lakini watu wanavyoweza kupigana vijembe, sasa katika hilo nampongeza sana Mheshimiwa Rais kwa kuheshimu Katiba. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Katiba yetu iko wazi, inasema nchi hii ni ya vyama vingi kwa hiyo, kwenda kinyume cha hapo ni kwamba, mtu anakuwa haheshimu Katiba. Kwa hiyo, namshukuru na ninampongeza sana Mheshimiwa Rais.

Mheshimiwa Spika, lakini nchi hii imeingia kwenye mikataba mingi ya haki za binadamu, ikiwemo ile ya human rights ya mwaka 1984 ambayo Tanzania tulisaini mkataba ule. Sasa kwenda kinyume na mikataba ile tunakuwa hatutendi haki kwa hiyo, nampongeza sana Mheshimiwa Rais, lakini Mheshimiwa Rais amekuwa kimataifa sasa anajulikana kila pembe kwa namna anavyofanya kazi yake katika kuhakikisha sisi sasa tunajikomboa kiuchumi na tunasonga mbele.

Mheshimiwa Spika, hivi karibuni unakumbuka Mheshimiwa Rais alipata tuzo ambayo ilitolewa kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu, tuzo ile inaitwa BABAKAR NDIAYE AWARD. Alipata ile tuzo kwa sababu, ya ule mchango wake unajulikana sasa kimataifa jinsi anavyofufua uchumi wa nchi yetu kwa hiyo, nampongeza sana Mheshimiwa Rais Samia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini lingine, hivi juzi tu tulikuwa kwenye Kamati ya PAC, tumezunguka sehemu nyingi tumeona miradi mingi ambayo sasa inaendeshwa ten ana wenzetu wawekezaji kutoka nje wengi sana sasa wanakuja Tanzania kwa sababu, sasa Mheshimiwa Rais ameifungua nchi na kila siku tunaona vikwazo vinaendelea kuondolewa kwa ajili ya wawekezaji kutoka nje. Kwa hiyo, tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini na wengine wamesema hapa, Mheshimiwa Rais juzijuzi hapa alikuwa ametuletea ugeni mkubwa sana wa Makamu wa Rais wa Marekani. Nchi ya marekeni kupata ugeni mkubwa kama ule, yeye Mheshimiwa Makamu wa Rais kufika tu hapa Tanzania, ujio wake sisi Tanzania tumejulikana dunia nzima kwa sababu, Marekani kiongozi wake anapokwenda mahali popote duniani ni karibu dunia nzima inafuatilia kwa hiyo, tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa ujio wa Makamu wa Rais wa Marekani.

Mheshimiwa Spika, lakini pia na yale ambayo wameweza kuzungumza kuhusiana na mambo ya kiuchumi na namna ambavyo Marekani wanaweza kusaidia katika kuendeleza uchumi wa nchi yetu, tunamshukuru sana Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini nimalizie kwa kusema Katiba, ambayo nimesema Mheshimiwa Rais anaiheshimu sana, nchi nyingi hata ambazo zimekuwa zikisifiwa kwamba, zina Katiba nzuri tumeona hata majirani zetu fulani hapa, siwezi kuwataja jina lao, siwezi kutaja hiyo nchi, pamoja na kusifu kwamba, Katiba yao ni nzuri, watu wanaendelea na maandamano. Kwa hiyo, narudia kusema Mheshimiwa Rais kuruhusu maridhiano ya kisiasa hapa Tanzania ule ni ushujaa mkubwa sana kauonesha na sisi tutamuunga mkono, kilichobaki sasa hivi tuendelee kushindana kwa hoja, tuende tuwapalekee wananchi nini kimefanyika katika awamu zetu zote katika utawala wetu wa Tanzania. Tukashindane kwa hoja milango kwa kuwa iko wazi sasa hakuna vile visingizio vya kwenda kutukanana hadharani.

Tuendelee kushindana kwa hoja, twende tuwapelekee wananchi nini kimefanyika katika awamu zetu zote katika utawala wetu wa Tanzania. Tukashindane kwa hoja, milango kwa kuwa iko wazi sasa hakuna vile visingizio vya kwenda kutukanana hadharani.

Mheshimiwa Spika, nimalizie kwa kusema kwamba na mimi naunga mkono hoja azimio hili kwa asilimia mia moja. Ahsante sana.