Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuimarisha demokrasia nchini na kukuza diplomasia ya uchumi

Hon. Amber. Mbarouk Nassor Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuimarisha demokrasia nchini na kukuza diplomasia ya uchumi

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Mheshimiwa Spika, naomba nikushukuru sana kwa kunipa hii fursa na mimi niweze kuchangia kidogo katika hii hoja. Sisi kwa Wizara ya Mambo ya Nje, jukumu letu moja kubwa ni kuhakikisha kwamba, diplomasia ya uchumi inaendelezwa kwa nguvu zote, lakini nashukuru kwamba, kazi hii sasa imekuwa rahisi kwa sababu, hapo kabla kidogo tulikuwa tunasuasua, lakini sasa kwa kweli tunafanya kazi vizuri sana na hii yote ni kutokana na Rais wetu Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kusafisha njia na huko tunakopita sasahivi tunapita vizuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nifahamishe kwamba, hivi sasa katika balozi zetu kuna msururu mkubwa sana wa wawekezaji ambao wanataka kuja kuwekeza nchini Tanzania. List ni kubwa sana na tunafanya kila juhudi kuhakikisha kwamba, wawekezaji hawa wanakuja Tanzania na kuchangia uchumi wa nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lingine, katika kipindi hiki tumeshuhudia biashara na nchi jirani imeongezeka sana mpaka kufikia kipindi kwamba, wengine wanalalamika, mbona bidhaa nyingi zaidi zinakuja kutoka Tanzania kuliko sisi tunavyopeleka Tanzania? Na hizi zote ni juhudu za Mheshimiwa Rais.

Mheshimiwa Spika, na suala jingine ni kwamba, hizi ziara ambazo Mheshimiwa Rais anafanya tayari zimeanza kuleta matunda na zimekuwa zikizidisha ufanisi wa Wizara yetu. Kwanza, nitataja mfano mmoja tu; ziara yam waka jana ya Mheshimiwa Rais ambayo aliifanya China, makubaliano 15 ya ushirikiano walikubaliana na tayari utekelezaji wa makubaliano hayo umeshaanza na hasa ikiwemo upelekaji wa bidhaa nyingi kwenda nchini China. Hizi zote ni fursa ambazo nchi yetu inatakiwa izitumie kikamilifu.

Mheshimiwa Spika, na kwa kumalizia niingine sasa kidogo katika maridhiano ya kisiasa; hili pia limeturahisishia sana kwa sababu, wenzetu wanapokuja katika Wizara zetu suala hili kila siku lilikuwa ndio gumzo, lakini hivi sasa hawalisemi tena kwa sababu, wanaona kwamba, siasa zetu zimekuwa ni za kirafiki, za kindugu, sio tena siasa za ugomvi na sio tena siasa za chuki. Na hii yote inasaidia katika kupaisha diplomasia ya uchumi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. (Makofi)