Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Afya

Hon. Kabula Enock Shitobela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Afya

MHE. KABULA E. SHITOBELA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii na mimi niweze kuchangia katika Wizara hii. Kwanza kabisa napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa afya njema na kutupa amani katika Taifa letu. Pili; napenda kumpongeza Mheshimiwa Rais, Samia Suluhu Hassan kwa kuongeza na kuiboresha sana Wizara ya Afya. Pia napenda kumpongeza Mheshimiwa Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya na Makamu wake, Mheshimiwa Naibu Waziri Dkt. Mollel na watu wote kwa kuongoza vizuri na kwa kuchapa kazi nzuri. Pia ningependa kuwapongeza sana wafanyakazi wote wa Wizara ya Afya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pamoja na jitihada za Serikali, mwaka 2015 Serikali iliweza kupunguza wastani wa vifo kutoka akina mama 11,000; mpaka kufikia 2020 Serikali iliweza kupunguza vifo 3,000 kwa taifa zima. Nakiangalia takwimu ya Kanda ya Ziwa mwaka 2019 akina mama 448 walipoteza maisha kutokana na uzazi, na mwaka 2020 akina mama 410 walipoteza maisha pia. Mwaka 2021 vifo 374 pia kupoteza maisha mwaka huo, 2020/2021. Hali hii bado si nzuri japo namba zinaonesha kupungua. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ushauri wangu kwa Serikali ni kuendelea kuimarisha upatikanaji wa dawa zote zinazotibu magonjwa haya yanayosababisha vifo hivi vya akina mama, kama vile magonjwa ya kifafa cha mimba, chinikizo la damu kutoka damu nyingi kabla na baada ya kujingua na uambukizo wa vimelea kwenye mfumo wa uzazi. Pili; kupeleka madaktari bingwa na waganga wa akina mama, hasa katika hospitali za wilaya na mikoa. Hii itasaidia sana kubaini matatizo mapema na kumaliza kabisa tatizo hili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Mwanza Wilaya ya Buchosa Visiwani kuna tatizo kubwa hasa Visiwa vya Maisome, Migingo, Lubalagazi pamoja na Buzikimba. Visiwa hivi vinachangamoto kubwa ya boti maji au ambulance ya kwenye maji. Naiomba sana Serikali itupelekee kule ambulance kwasababu akina mama wengi wanafariki dunia kwa kukosa huduma za haraka.

Mheshimiwa Spika, pia katika Visiwa vya Ukerewe kuna upungufu wa asilimia 56 ya watumishi wa afya, Wilaya nzima ya Ukerewe pamoja na kuwa ni visiwani hakuna x-ray machine; iliyopo kwa sasa niyakizamani sana imekuwa na tatizo la kuharibika mara kwa mara na inapelekea usumbufu wa wagonjwa kutoka pale Ukerewe wapande boti mpaka Mwanza Mjini ndipo waende kutibiwa. Kwa hiyo, naiomba sana Serikali iangalie sana hasa kwenye miundombinu migumu kama Ukerewe kwasababu hakuna usafiri mwingine zaidi ya kupanda meli au boti. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, namuomba sana Wizara Ummy Mwalimu, namwamini kabisa, ni dada jemedari, hodari sana, ni jembe. Kwa hiyo naomba sana uangalie, hasa akina mama wenzangu kule Ukerewe na huku Bushosa Visiwani ambako kwakweli shida ni kubwa mno. Akina mama wanajifungulia njiani boti ikiharibika kidogo, mabapo inabidi wasubirie mpaka boti nyingine ifike ndiyo waweze kupata usafiri kuelekea Mwanza.(Makofi)

Mheshimiwa Spika, nikiangalia tena katika Wilaya ya Kwimba kijiji cha Nyambiti Kituo cha Afya cha Nyambiti hakina jengo la upasuaji. Wananchi wamenunua vifaa kwa kuchanga wao wenyewe. Sasa naiomba Serikali iharakishe kutusaidia kutuwekea japo hilo jengo kwasababu wananchi wameshatumia nguvu zao wenyewe kununua vifaa. Kwa hiyo, ninaomba sana, nakuomba sana ndugu yangu mtani wangu Ummy Mwalimu uwaangalie watani zako wa Kijiji cha Nyambiti na uwajengee hilo jengo ikiwezekana hata mwaka huu tutashukuru sana.

Mheshimiwa Spika, sasa napenda kumwongelea mtoto njiti, ndani ya miezi minne watoto 1,000 huwa wanalazwa hospitalini kwa magonjwa ya aina mbalimbali, lakini asilimia 50 ya watoto hao huwa ni watoto njiti na asilimia 25 katika watoto hao kwenye 50 percent, asilimia 25 ya vifo hivi ni mtoto njiti kwa sababu hawana kinga mwilini. Ushauri wangu kwa Serikali wawekeze upatikanaji lishe inayotolewa kwa njia ya mpira, upatikanaji wa vifaa vya kutunza joto la mwili (incubator) hasa kwenye Vituo vya Afya vya Vijijini kwa sababu sehemu za wilaya nyingi hazina vyumba maalum kwa ajili mtoto njiti. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Kengele imeshagonga Mheshimiwa.

MHE.KABULA E. SHITOBELO: Mheshimiwa Spika, ahsante na naunga mkono hoja. (Makofi)