Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maji

Hon. Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maji

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO: Mheshimiwa Spika, kwanza nampongeza Mheshimiwa Waziri pamoja na Naibu Waziri, Katibu Mkuu na watendaji wa Wizara yake.

Mheshimiwa Spika, jana nilichangia bajeti yako na kwa msisitizo, nimesikitika sana kuona Mradi wa Maji kutoka Ziwa Victoria kwa ajili ya Kata za Gwanseli, Magata Karutanga, Muleba, Bureza, Kikuku na Kagoma. Mradi huu ulianza kuasisiwa mwaka 2009. Upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ulikamilika mwaka 2020. Nimeulizia mara mbili juu ya mradi huu majibu yalikuwa ni ya kutia moyo kwamba mradi huu utakuwa kwenye bajeti ya mwaka 2022/2023. Mradi huu, haupo kwenye bajeti yako. Nimesikitika sana, Muleba imesikitika sana. Nakuomba uangalie kwenye bajeti yako, mradi huu ni muhimu sana kwa Muleba.