Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hoja ya Dharura (Changamoto ya Kupanda kwa bei za Mafuta ya Petroli, Dizeli na Mafuta ya Taa)

Hon. Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hoja ya Dharura (Changamoto ya Kupanda kwa bei za Mafuta ya Petroli, Dizeli na Mafuta ya Taa)

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Ni ukweli usiopingika kwamba Watanzania na dunia nzima wanajua kwamba kuna changamoto ya kupanda kwa haraka sana kwa mafuta ya petrol, diesel pamoja na mafuta ya taa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ukipandisha bei ya mafuta ya taa, petrol na diesel umepandisha kila kitu.

MBUNGE FULANI: Amen!

MHE. OMARI M. KIGUA: Jambo hili Tanzania nzima sasa hivi kelele ni suala la mafuta. Sasa sisi kama Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tunao wajibu mkubwa sana wa kuisimamia na kuishauri Serikali katika jambo hili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa kweli isingekuwa busara kama wananchi ambao wametupa dhamana kubwa ya kuweza kuwasemea hapa Bungeni tusiposema jambo hili na Serikali isiposimama hapa kusema jambo lolote lile maana yake tunakuwa hatuwatendei haki wananchi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wenzetu wa EWURA juzi wametoa bei elekezi ambazo zimeanza jana tarehe 4 Mei. Nilikuwa natazama hapa petrol Kagera ni shilingi 3,385/=. Jambo hili ni lazima sasa tusimame kama Wabunge, tuzungumze na tuishauri Serikali. Nina uhakika Serikali hii ya Chama cha Mapinduzi chini ya uongozi wa Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ina uwezo wa kufanya jambo kama ambavyo Serikali nyingine katika dunia wanafanya, kwa sababu wananchi hawawezi kuzungumza, wananchi hawawezi kulalamika, halafu Serikali haisemi jambo lolote.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nilikuwa naomba ridhaa yako kutoa hoja kwamba Waheshimiwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tuzungumzie hoja hii ili tusikilize Serikali inasema nini juu ya ongezeko la mafuta?

Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja.

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Spika, naafiki.