Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Na mimi niungane na wote ambao wanazungumzia utumishi wa umma, wanazungumzia wafanyakazi wanapoajiriwa, suala la umri; ukisema umri miaka 25 wakati Wabunge wengi hapa wanasema tuwaangalie wale ambao walikuwa wameshaanza kujitolea, then nadhani itakuwa hai-make sense. Kwa hiyo, naamini Waziri wakati anajibu yale masharti ya umri yatakuja kutolewa kulingana na mazingira yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili, yamekuwa yakizungumzwa masuala mengi sana kuhusiana na kustaafu. Waziri Jenista atasema yeye anahusika na watumishi wa umma, lakini vilevile atasema masuala ya kustaafu yako Wizara ya Vijana kwa sababu inasimamia mifuko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini ni ukweli hivi vitu haviwezi kutenganishwa. Nimesema mtumishi anaanza pale anapoajiriwa, pale anapofanya kazi, pale anapostaafu. Sasa unapokuwa na mtumishi sasahivi yuko kazini halafu hajui mustakabali wake baada ya ajira, akiwa mtu mzima wakati viungo vya mwili vimechoka hana uwezo wa kufanya kazi, hiyo si sawa. Na kwa sababu Serikali ni moja ninatarajia kabla Mheshimiwa Jenista hajajibu Waziri anayehusika na mifuko atueleze Watanzania hali ya mifuko ya umma ikoje? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jana kazungumza Mheshimiwa Bulaya hapa, akasema, tathmini iliyofanyika inaonesha mfuko wa PSSF uko below average, una hali mbaya. Unatakiwa kwa wastani kwa kiwango cha chini iwe asilimia 40, leo iko asilimia 22, tunataka mtujibu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilipitia Taarifa ya CAG kidogo. Shirika la Reli, kwa mfano, unaambiwa makato ya Mfuko wa Pension kwa Watumishi wa Umma ya thamani ya shilingi bilioni 99.6 hayajapelekwa PSSF. Yani kuanzia mwaka 2015 mpaka mwaka 2021 watumishi wa Shirika la Reli, shirika la umma, makato yao hayajapelekwa. Hivi mtasema hamtakiwi kujibu? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo tunajenga reli ya SGR. Reli ya SGR ikikamilika na matawi yake yote ambayo hili Shirika la Reli ndilo linasimamia itaigharimu Taifa shilingi trilioni 32, SGR na matawi yake yote. Hivi kweli tukiwaambia kwa nini msiwajibike kutoa taarifa hapa ili watumishi wa nchi hii wajue hali yao? Tunataka Waziri wa Kazi ukija hapa, hii ni Serikali, tunazungumza na Serikali, mmelipa trilioni mbili sijui point moja hatifungani sio cash. Tunataka ile trilioni 2.58 iliyobaki ilipwe sasa ili mfuko uwepo kwenye uhai. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Jenista niliwahi kuuliza hapa, kwa sababu mfuko huu unalipa wale wafanyakazi kabla yam waka 99 waliokuwa hawachangii. Kwa hiyo, hatushangai Wabunge wanavyosema wastaafu wanastaafu mafao yanachelewa kwa sababu lile kapu halina hela, huo ndio ukweli.

Kwa hiyo tunataka Mheshimiwa tujibiwe, hiki kikombe ulikikimbia ulivyoondoka ile Wizara, hiki kikombe tunataka kijibiwe leo na Serikali kwa sababu tunazungumza na Serikali. Hilo la kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, Wakala wa Ndege Mheshimiwa Jenista. Wakala wa ndege uko chini yako, ATCL wanasema sababu ya kushindwa kufanya kazi ni kwa sababu wanawalipa Wakala wa Ndege tozo ya kukodi na pesa ya marekebisho ya ndege, ukarabati wa ndege. Na wanasema zimelipwa milioni 159, wanasema hivi wanawalipa nyie fedha za ukarabati, lakini ikija kwenye ukarabati hamtoi pesa. (Makofi)

Mheshimiwa Jenista ukurasa wa 41 wa hotuba yako inasema wazi kabisa…

MWENYEKITI: Unaongea na Kiti ee.

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naongea na…

MWENYEKITI: Unaongea na Kiti. Usimu-address Waziri.

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naongea na wewe ndiyo, huku namu-address Mheshimiwa Jenista Mhagama. Unasimamia Wakala wa Ndege, kwenye mipango yako ya mwaka huu, unasema wazi kabisa utafanya matengenezo ya ndege ya viongozi wakuu, utafanya matengenezo ya ndege ambayo ni aina ya Forker 50, hakuna ndege yoyote kati ya hizi ambazo ni zile ndege 16 za ATCL, hapa ndipo ulipo mzizi wa fitina.

Sasa nataka ukinijibu uje ueleze kwa namna gani zile fedha ambazo kwa akili ambayo kwa kawaida hai-make mantiki mmekodisha ndugu zenu shilingi bilioni 159 ambazo kati ya hizo milioni 59.4 ni za matengenezo ya ndege. Kwa nini mnaliachia shirika la ndege likarabati na kufanya matengenezo ya ndege zake peke yake? (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini mwisho, na si kwa umuhimu. Tunaambiwa kwamba…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. (Makofi)