Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2022

Hon. Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2022

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi jioni hii ili niweze kuchangia hoja za kamati mbili; Kamati ya Bajeti na Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mchango wangu nitajikita zaidi kwenye Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama. Nikianza kwa kupongeza kwa dhati kabisa viongozi wa wanaoongoza Wizara zinazosimamiwa na Kamati yetu hii ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama; nikianza na Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Nje, mama mchapakazi Mheshimiwa Tax pongezi sana kazi nzuri na kwenye kamati kwa kweli umeonesha ushirikiano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Mheshimiwa Balozi Mbarouk Naibu Waziri ameonesha ushirikiano wa kutosha kwenye Kamati na yote ambayo tumeyaleta kwenye Bunge ni mchango wa pamoja kati ya sisi Wanakamati pamoja na viongozi wetu hawa wakisaidiana na watendaji wao. Lakini Mheshimiwa Waziri, rafiki yangu wa Ulinzi Bashungwa naye ameonesha uwezo mkubwa sana. Nadhani katika historia ya nchi hii anaweza akawa labda ni Waziri wa pili kijana kuongoza Wizara hii nyeti na ameonesha kumudu. Nikupongeze sana ndugu yangu Bashungwa wewe pamoja na watendaji wako Wizara inakwenda vyema na sisi wanakamati hatuna shaka na wewe kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nipongeze vyombo vyetu vya ulinzi na usalama kwa kuendelea kutekeleza majumu yao kiasi kwamba Watanzania tumeshazoea kuwa nchi yetu ni nchi shwari, nchi yetu ni nchi ya amani, nchi yetu ni nchi yenye mtangamano, haina shida yoyote mashaka yoyote ukilinganisha na baadhi ya nchi katika bara letu la Afrika au kwingineko duniani. Haya yote hayajafika hapa Tanzania kwa bahati nasibu isipokuwa ni kazi ya dhati kabisa inayofanywa na vyombo vyetu vya ulinzi na usalama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na pongezi hizi mimi nitandoa kwa uchache sana katika maeneo machache ambayo yamelegalega katika wizara zetu mbili hizi; kwa maana ya Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki pia pamoja na Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na maeneo haya kimsingi hayakulegalega kwa sababu ya utendaji usioridhisha wa Waziri au watendaji katika Wizara isipokuwa ni kwa kukosa ushirikiano miongoni mwa Wizara zingine ambazo zilipaswa zisaidie kuwezesha kazi za Wizara hizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikianza na Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, kulikuwa nae neo la kulegalega kwa utekelezaji wa diplomasia ya uchumi kama ambavyo taarifa yetu imesema. Eneo hili limelegalega kwa sababu ya kukosekana kwa coordination. Nitoe ushauri kabisa katika Bunge hili, kwamba ili diplomasia ya uchumi iweze kutekelezwa ipasavyo lazima kuwe na utaratibu wa ku-coordinate miongoni mwa Wizara, kwa maana ya Wizara za Uzalishaji pamoja na Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia katika Wizara hiyo ya Mambo ya Nchi za Nje kumekuwa na kulegalega katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Kwa mfano katika balozi zetu kuna majengo 47 yanahitaji ukarabati mkubwa. Pia kuna majengo tisa yamechakaa, pia kuna majengo 11 hayako katika hali nzuri kabisa kiasi kwamba yanatweza hadhi ya nchi yetu Tanzania huko nchi za nje. Haya yote hayakufanywa kwa sababu ya uzembe katika wizara isipokuwa ni kwa sababu wizara haikuwezeshwa kutoa fedha za kutosha kwa wakati kutekeleza miradi hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano kwa kipindi cha kuanzia Julai 2022 hadi Januari 2023, wakati taarifa yetu sisi ndiyo tunaijadili kwenye Kamati yetu hakukuwa na fedha yoyote iliyopelekwa kutekeleza miradi hiyo. Huu ni msiba na ni si jambo ambalo linatakiwa watanzania au Wabunge tulitazame kwa mtazamo mwepesi mwepesi lazima tutazame kwa mtazamo mzito katika eneo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na kwa kukosekana hivyo jambo hili limeikumba pia Jeshi la Magereza. Bajeti ambayo tuliipitisha mwaka jana kwenye Jeshi la Magereza mwaka 2023 ni bilioni 21.369 lakini mpaka tunajadili taarifa ya Wizara ya kuanzia Julai 2022 mpaka Desemba 2022 hakuna fedha yoyote iliyopelekwa kwenye Jeshi letu la Magereza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na kwa kufanya hivyo tafsiri yake ni tafsiri yake ni kwamba Jeshi la Magereza limeshindwa kutekeleza mipango yake ya usalama, mipango ya Ofisi za Magereza, mipango ya ujenzi au uanzishaji wa mashamba ya magereza pamoja na mpango wa kuboresha upatikanaji wa maji katikamagereza yetu. Hali hii si hali ambayo inaridhisha na inapendeza katika nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, na kwamba haitoshi Jeshi la Zimamoto na Uokoaji ambayo fungu lake la fedha ni fungu 14, bajeti ambayo Bunge hili liliidhinisha ilikuwa ni shilingi bilioni 9 .93, lakini mpaka Julai Desemba hakuna fedha yoyote iliyopelekwa kwa ajili ya Jeshi la Uokoaji na Zimamoto. Huu ni msiba mkubwa. Inapotokea majanga ya moto au majanga mengine ambayo yanahitaji msaada wa jeshi hili Watanzania tumebaki tukiwa tunalaumu kuwa Zimamoto wameshindwa kufika kwa wakati, lakini kumbe ni kwa sababu hawajawezeshwa kupata vifaa vya kisasa kuweza kuokoa majanga kwa kipindi yanapotokea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie na Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, lakini hapa nitagusia fungu moja tu ambalo ni Fungu 39 katika kamandi ile ya Jeshi la Kujenga Taifa. Kamandi ya Jeshi la Kujenga Taifa kwa kipindi cha Julai mpaka Desemba hakuna hata senti tano ambayo imepelekwa kwenye Kamandi hii ya Jeshi la Kujenga Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maswali ya kujiuliza ni kama ifuatavyo; kwa nini sasa Wizara hii inaitwa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa ilhali hatuwezeshi JKT kufanya majukumu yake? Kwa nini Jeshi limeweka Kamandi ya Jeshi la Kujenga Taifa ilhali hatuwezeshi JKT kufanya majukumu yake? Kwa nini kila mwaka tunachukua vijana ili waende JKT wakafanye National Service kule ilhali JKT haijawezeshwa kufanya yake? Huu ni msiba na kama ni msiba si jambo ambalo tunatakiwa tulijadili kwa wepesi wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho nitoe assignment question kwa Serikali; is Tanzania, the United Republic a country or Nation state discuss. If it is a country, it is well and good to leave these armed forces without to incapacitate them. But if it is a National state should you, the Government please provide enough fund to the National Service, enough fund to armed forces, provide enough fund to the immigration forces in order for Tanzania to be a country a National state, United Republic and Sovereign State. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja.