Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2022

Hon. Vincent Paul Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2022

MHE. VINCENT P. MBOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi niweze kuchangia hoja iliyoko mbele yetu, ya Kamati ya Kudumu ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama. Kipekee nimpongeze sana Mheshimiwa Rais kwa kazi anayoifanya, amekuwa kinara kwa matendo kukuza diplomasia ya uchumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, elimu kuhusu diplomasia ya uchumi kwa wananchi bado iko chini, hakuna uelewa, kuanzia wizarani, mikoani, wilayani mpaka vijijini, hasa maeneo ya mipaka ambako wafanyabiashara wengi hawajapewa elimu kuhusu diplomasi ya uchumi, kwahiyo bado wanafanya shughuli zao za kiuchumi kienyeji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kukuza diplomasia ya uchumi, Wizara ya Kilimo, Viwanda na Biashara, Wizara ya Ulinzi pamoja na Maliasili lazima viwe coordinated pamoja na Wizara ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano Wizara ya Kilimo ina mpango wa kuanza hizi block farming ambazo zinaenda kuanzishwa nchi nzima, ndio mwanzo pekee ambao tunahangaika vijana hawana ajira. Wale vijana wanaotoka JKT kwa sababu watakuwa tayari wameshajifunza kilimo, kufanya kazi kwa bidii, wakishatoka JKT wapelekwe kwenye hizi block farming ambazo zinaanzishwa na Wizara ya Kilimo. Na hii Wizara ifanye tathmini kwa yale mazao ambayo yana soko. kwa mfano kwa upande wa Nyanda za Juu Kusini waje waanzishe block za kulima mahindi kwa sababu tayari wananchi wana uelewa wa uzalishaji wa mahindi. Waje na block za kuanzisha ngano, soya, alizeti pamoja na Ukanda wa Ziwa Rukwa na Ziwa Tanganyika wafanye utafiti kuanza hizi block hata kilimo cha miwa. Na kwenye hizo block waanzishe kutengeneza viwanda vidogo vodogo ambazo block wakishatoa mazao yao tusiuze mazao ghafi, tuweke mashine, viwanda ili ziweze ku-process tuuze nje mazao yanye thamani kamili, tusiuze mazao ambayo yamelimwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye hizo block farming ifike mahali tupangiwe taratibu na kanuni, hizi block farming ziwe connected na Jeshi la Kujenga Taifa kwa ajili ya watu wakitoka JKT.

Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha nyingi Mheshimiwa Rais atazipeleka kwenye block farming, ukishazipeleka kule watapelekewa raia ambao hawana utaalamu na hivyo hizi block farming zitageuka kama ndiyo sehemu ya kujifunzia. Kwa hiyo JKT waunganishwe na hizi block farming ili waende kuwa wasimamizi wa hizi block farming, kwa sababu fedha nyingi zitaenda, wataenda kuanza kujifunza kulima. Lakini zikiunganishwa na Jeshi la Ulinzi tutapata mazao, mashine zitapelekwa viwanda vidogo vidogo wananchi wa kule wakiungana na wanajeshi kazi itafanyika vizuri kwa bidii. Wizara ya Viwanda na Biashara itafute masoko. Kwa hiyo hizi block farming zitengenezwe kulingana na aina ya masoko ya mazao yanayohitajika na nchi jirani ili kukuza diplomasia ya uchumi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa imeongelea kuhusu mipaka. Ukitaka kutazama kwa undani kabisa Wabunge wengi wamelalamika uzalendo unapungua na tukiona nchi jirani kuna changamoto ya uhalifu hasa maeneo ya buffer zone. Maeneo ya mipakani kuna uhalifu unaojirudiarudia. Wizara ya Ujenzi na Wizara ya Ardhi watengewe bajeti ili waweze kwenda kuimarisha miundombinu ya kuweka bicon kwenye mipaka na barabara zile za kiuchumi pamoja na za kiulinzi ili vyombo vyetu vya ulinzi vinapofanya kazi ya ulinzi mawasiliano yaweze kufika kwa urahisi, kwa sababu wahalifu wengi wanakaa maeneo ya buffer zone maeneo ambayo ndiyo vichaka vya uhalifu unaoendelea, hasa katika maeneo yale ambayo shughuli za kiuchumi zinafanyika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili wafanyabiashara wafanye vizuri maeneo ya mipaka Wizara ya Ardhi pamoja na Miundombinu watenge na waainishe barabara za kiuchumi, beacon ziwekwe ili mambo yaende vizuri. Kwa sababu hizi wizara; kwanza nizipongeze kwanza, zinafanya kazi kubwa mno; Wizara ya Ulinzi, vyombo vya ulinzi vyote kwa pamoja amani na utulivu tulionao Tanzania ni kwa sababu haya majeshi yetu, Jeshi la Polisi, vyombo vya ulinzi vinafanya kazi usiku kucha; na hata sisi wenyewe Bungeni tunakaa kwa usalama kwa sababu ya vyombo vya ulinzi vinafanya kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndio maana naendelea kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa sababu anaendelea kutoa ajira kwenye hivi vyombo ili viendelee kufanya kazi kwa ufanisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukisoma kwenye Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Mambo ya Nje na Usalama hizi wizara bado zina bajeti finyu sana. Nashauri Wizara ya Fedha itenge bajeti ili iweze kuipatia hivi vyombo vya ulinzi pamoja na Wizara ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama. Sehemu kubwa ina changamoto kubwa sana. Mheshimiwa Rais anahangaika huko nje kutafuta masoko lakini ukiangalia hata makazi ya balozi pamoja na ofisi zetu huko nje, pamoja na viwanja vingi havijaboreshwa. Muonekano wa kuvutia diplomasia ya uchumi pamoja na watalii ianze kuonekana nje. Kwa hiyo wizara hii ipewe fedha ili iweze kujenga miundombinu mizuri na kuweza kutangaza Tanzania nje kwa muonekano wa viwanja vyetu pamoja na ofisi.

MHE. ALI JUMA MOHAMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Ali taarifa.

T A A R I F A

MHE. ALI JUMA MOHAMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpe taarifa mchangiaji kuwa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita Wizara hii ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ilitengewa takribani bilioni 48.5; lakini mpaka tunafikia sasa katika kipindii chote cha miaka 5 wizara hii ilikabidhiwa bilioni tisa tu.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Mbogo unaipokea taarifa.

MHE. VINCENT P. MBOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipokea kwa mikono miwili. Hii Wizara ya Mambo ya Nje haijapata fedha kwa muda mrefu, imesahaulika. Kamati ilienda Ethiopia tukakuta kuna viwanja ambavyo bado havijajengwa, Kamati ikaomba miadi na Mheshimiwa Rais wa Ethiopia, Mheshimiwa Rais kwa kuheshimu diplomasia na nchi yetu akaahirisha safari zake akakutana na Kamati. Akaturuhusu na akatuhakikishia viwanja hivyo ambavyo vingeweza kuchukuliwa virejeshwe na akashauri pajengwe ubalozi mzuri ambao utarudisha mahusiano kati ya Tanzania na Ethiopia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.