Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya Mkataba wa Umoja wa Nchi Huru za Afrika wa Kuzuia na Kupambana na Ugaidi ya Mwaka 2004

Hon. Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya Mkataba wa Umoja wa Nchi Huru za Afrika wa Kuzuia na Kupambana na Ugaidi ya Mwaka 2004

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru nami kwa kupata nafasi hii ya kuweza kuchangia hoja iliyopo Mezani inayohusu Itifaki ya Mkataba wa Umoja wa Nchi Huru za Afrika ya Kuzuia na Kupambana na Ugaidi ya Mwaka 2004.

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nami nipongeze sana Wizara hii, nikianza na Mheshimiwa Waziri, ndugu yangu, Mheshimiwa Eng. Masauni, kwa kazi nzuri ambayo anaifanya katika Wizara hii; na Naibu Waziri, kaka yangu, Mheshimiwa Sagini, ambao kimsingi sisi kama Kamati tumeshirikiana nao vizuri sana katika kuchakata itifaki hii mpaka leo inawasilishwa hapa Bungeni, nasi Wabunge tunapata nafasi ya kuchangia kwa lengo la kuomba Wabunge wenzetu waweze kuridhia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze na nimshukuru pia Mwenyekiti wangu wa Kamati, kaka yangu Mheshimiwa Vita Kawawa kwa namna ambavyo ametuwakilisha vizuri sisi Wanakamati wenzie katika kuwasilisha yale ambayo tulipokuwa kwenye Kamati ndiyo tumekubaliana kama Maoni ya Kamati ya kuwasilishwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mchango wangu nitakuwa na mambo machache sana ya kuchangia ambayo yataongozwa na swali moja tu kwamba kwa nini sisi Tanzania kupitia Bunge lako hili tuweke Azimio hili la kuridhia itifaki hii. Jambo la kwanza nature ya ugaidi wenyewe. Kimsingi dhana ya ugaidi si dhana ambayo inafanyika katika utaratibu wa kindani kwa maana locally, kinyume chake ni dhana ambayo inavuka Taifa moja mpaka Taifa lingine kwa maana ni dhana ya kimataifa. Kwa maana hiyo, kama ni jambo la kimataifa hatuwezi sisi Tanzania ambao tunajiita nchi iliyo kamili tukabaki wenyewe bila kushirikiana na nchi zingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, sisi Watanzania tukiridhia Itifaki hii, tutakuwa na fursa ya kuweza kushirikiana na nchi zingine za Afrika. Tukumbuke katika wasilisho ambalo Mheshimiwa Waziri amewasilisha hapa ni kwamba nchi 45 za Afrika zimesaini Mkataba huu ikiwemo Tanzania. Katika nchi hizo 45 ni nchi 21 ambazo zimeridhia na kwa maana hiyo sisi Watanzania tukiuungana au tukiridhia tutakuwa tumeungana na nchi zingine za Afrika 21 ikiwa ni pamoja na jirani zetu wa nchi kama za Rwanda, South Africa, Burundi, Lesotho, pamoja na nchi nyingine za Afrika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu, kwa nini turidhie? Itakuwa imetupa nafasi au fursa ya kufanya marekebisho ya Sheria yetu iliyotungwa mwaka 2002, Sura Na. 19 ambayo tunasema ni Sheria ya Kuzuia Ugaidi na kwa maana hiyo tutakaporidhia Itifaki hii tutaweza kuwa na fursa ya kubadilisha Sheria yetu na kuwa Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Ugaidi ambapo sababu sheria zinatungwa hapa Bungeni, Wabunge tutakuwa na nafasi pana zaidi ya kutoa mawanda ya maelezo yetu maana wazoefu katika kuchangia sheria ambayo itakuwa na maslahi kwa nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, kwa nini turidhie? Viashiria vya matukio ya kigaidi ni viashiria ambavyo katika nchi yetu tumeanza kuvisikiasikia kipindi kifupi kilichopita, lakini pia miaka kadhaa imepita nchi jirani siyo tu viashiria badala yake ni matukio ya kigaidi yameweza kutokea. Wote tunakumbua matukio ambayo yametokea Kenya miaka kadhaa iliyopita. Hivyo basi, hatuwezi kuwa salama kama jirani zetu au hata ndani ya nchi viashiria hivi vinatokea na sisi tuone kwamba tuko radhi hatuwezi kuridhia Itifaki hii, tukabaki salama hapana. Niombe sana Waheshimiwa Wabunge tuunge mkono Itifaki hii ili nchi yetu iweze kusaini na kuridhia ili tuungane na nchi zingine za Afrika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja. (Makofi)